Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 2,797
- 11,959
Jamii Forums inakukaribisha kushiriki kwenye Mjadala kuhusu Maambukizi ya #COVID19 pamoja na Utoaji wa Chanjo nchini Tanzania
Mjadala huu unafanyika Agosti 6, 2021 kupitia Twitter Spaces (JamiiForums) kuanzia Saa 12 jioni na utahusisha Wataalamu wa Afya watakaozungumzia Masuala anuani kuhusu Janga hili
====
UPDATES;1800hrs
======
Kufuatilia mjadala huu, fungua hii link.
#UVIKO3
Je, ni lazima Mtu avae Gloves wakati wa kuchanja mtu?
Dr. Francis& Dr. Mariam: Kuvaa Gloves unatakiwa kila Gloves moja mtu mmoja, kwahiyo kwa siku mtu anayetoa chanjo anatakiwa avae Gloves 400. Hivyo kutokuvaa gloves ni rahisi hata kusafisha mikono kila baada ya kuchanja kuliko kuvua na kuvaa gloves. Pia muongozo wa Kuchanja unaruhusu kuchanja bila gloves.
Je, ni asilimia ngapi ya Watanzania Wachanje tuseme watu wengi wana kinga?
Dr. Mariam: Asilimia 70 hadi 80 ndo inashauriwa.
Dkt. Maryam: Watu wengi wanapokuwa hawana Chanjo ndivyo ambavyo Kirusi kinavyopata nafasi zaidi ya kuweza kubadilika
Hadi tutakapofikia 70% - 80% ya Watu waliopata Chanjo ndipo tunaweza kusema tumefanikiwa katika kupunguza Maambukizi
Dkt. Francis: Tunapozungumzia UVIKO19 kuna athari kubwa kwa Mtu na inaongeza mzigo kwenye utoaji huduma za Kiafya ikiwemo ICU na Oksijeni
Kwa hiyo wote tunaingia gharama kwasababu kuna Mtu atakosa Oksijeni akiwa na Magonjwa mengine sababu ya Mtu mwenye COVID19
Dkt. Maryam: Watu wengi wanapokuwa hawana Chanjo ndivyo Kirusi kinavyopata nafasi zaidi ya kuweza kubadilika
Hadi tutakapofikia 70% - 80% ya Watu kuwa wamepata Chanjo ndipo tunaweza kusema tumefanikiwa katika kupunguza Maambukizi
Dkt. Elisha: Nimeridhika na mwamko wa Watanzania kwenda kuchanjwa na naweza kusema mpaka hapa tulipofika ni 'success'
Tulipotoka Watu hata walikuwa hawaruhusiwi kuongelea #COVID19 huku wengine wakiwa kwenye Lockdown
Dkt. Francis: Watu wengi wanaogopa kwenda kuchanjwa kwasababu ya Uoga. Mitandao ya kijamii ina taarifa nyingi ambazo zimepotosha Watu
Mbele ni kuzuri ila cha msingi tuendelee kuwapa Watu taarifa sahihi. Mtu akiona mwenzie hajapata tatizo naye atakwenda kuchanjwa
Dkt. Norman: Ni ngumu kusema tumeridhika na mwamko wa Watanzania kwasababu hatuna Data za Dawa ngapi zilikuwepo na ngapi zimetoka
Ni matarajio yangu mpaka mwisho wa Mwaka Watu wote kwenye makundi Maalum watakuwa wamekuwa 'Covered'
Dkt. Norman: Kwa Dunia kasi ya uchanjaji inaendelea vizuri ambapo Mpaka Machi zilikuwa zimeshatoka dozi takriban bilioni 1.3
Kwetu tujitahidi ku-cover makundi Maalum. Afrika bado hakuna Nchi ambayo imeshafikia 5% ya Uchanjaji kwasababu Kampuni nyingi wanahodhi Chanjo
Dkt. Sajjad: Nimeridhika kwa kiasi fulani lakini bado tuna safari ndefu. Nimeridhika kwasababu kulikuwa a upotishaji. Baadhi ya Viongoxi walikuwa wanapotosha Jamii
Kuna mwamko sasa hivi, angalau tumefika sehemu nzuri. Ni jukumu letu sote kuelimisha jamii
Dkt. Maryam: Mtu ambaye ni Mgonjwa na yupo hoi Hospital hatakiwi kupata chanjo wakati huo bali asubiri mpaka Wiki 4 ndio apate Chanjo
Mtu anapokuwa anaumwa Mwili wake unakuwa unapambana na Maambukizi, akipewa Chanjo inakuwa inazidisha hali yake kuwa mbaya
Dkt. @amour_maryam: Mgonjwa mwenye maambukizi hai (active) yaani ana dalili za wazi hatakiwi kupata chanjo wakati huo bali asubiri mpaka Wiki 4
Kwa wakati huo mwili unakuwa unapambana na Maambukizi, akipewa Chanjo inakuwa inazidisha hali yake kuwa mbaya
Dkt. @furia_francis: Watu wanaopewa chanjo ni ambao hawana dalili, ukiwa mgonjwa huwezi kupata chanjo
Hakuna utaratibu kwamba tunawapima watu kabla ya kuwapa chanjo. Tunachoangalia ni dalili za ugonjwa, na tunauliza. Kama hauna dalili unaweza kupewa chanjo
Dkt. Maryam: Ukishapata Chanjo hakikisha unaendelea na taratibu zote za kujilinda ikiwemo kuvaa Barakoa
Kupata Chanjo haimaanishi uanze kujiachia. Ukikuta foleni kwenye Chanjo jitahidi kukaa mbali kidogo na Watu unapoendelea kusubiri
Dkt. @amour_maryam: Ukishapata Chanjo hakikisha unaendelea na taratibu zote za kujilinda ikiwemo kuvaa #Barakoa
Kupata Chanjo haimaanishi uanze kujiachia. Ukikuta foleni kwenye Chanjo jitahidi kukaa mbali kidogo na Watu unapoendelea kusubiri
Dkt. @SajjadFazel: Chanjo ya Johnson & Johnson ilisitishwa Marekani kwa muda ili kuangalia madhara waliyopata Watu ni kiasi gani
Baada ya utafiti waliridhika iko salama na imeendelea kutumika. Kusema tumeletea Chanjo iliyokataliwa sio sawa. WHO pia imeikubali ni salama
Dkt. Maryam: Ukishapata Chanjo hakikisha unaendelea na taratibu zote za kujilinda ikiwemo kuvaa Barakoa
Kupata Chanjo haimaanishi uanze kujiachia. Ukikuta foleni kwenye Chanjo jitahidi kukaa mbali kidogo na Watu unapoendelea kusubiri
Dkt. @amour_maryam: Ukishapata Chanjo hakikisha unaendelea na taratibu zote za kujilinda ikiwemo kuvaa #Barakoa
Kupata Chanjo haimaanishi uanze kujiachia. Ukikuta foleni kwenye Chanjo jitahidi kukaa mbali kidogo na Watu unapoendelea kusubiri
Dkt. Sajjad: Chanjo ya Johnson & Johnson ilisitishwa Marekani kwa muda ili kuangalia madhara waliyopata Watu ni kwa kiasi gani
Baada ya utafiti waliridhika iko salama na imeendelea kutumika. Kusema tumeletea Chanjo iliyokataliwa sio sawa. WHO pia imeikubali ni salama
Dkt. Norman: Chanjo inaenda kusisimua mwili, mara nyingi side effects zinaweza kutokea. Kuna baadhi ya watu kichwa kitauma, watasijikia kuchoka
Dalili hizi mara nyingi zinaisha ndani ya siku chache, zikiendelea ni vyema mtu akarudi kituo alichopata chanjo
Dkt. Sajjad: Sio kila anayepata Chanjo ya Coronavirus atapata tatizo la kuganda. Kuna sababu nyingi za Damu kuganda
Ukishapata Chanjo ikafika siku 6 - 15 tangu uchanjwe ukianza kuona dalili za kutokuona vizuri na maumivu kwenye Kifua ni vizuri kwenda Hospital haraka
Dkt. @SajjadFazel: Utafiti mbalimbali unafanyika duniani kuangalia hizi chanjo zinatoa kinga kwa kiasi gani dhidi ya Kirusi cha Corona aina ya Delta
Baadhi ya Chanjo mfano Johnson & Johnson inaweza kukupa kinga asilimia 60-70
Dkt. Maryam: Utafiti wa hivi karibuni unaonesha Effectiveness ya Chanjo ya Johnson&Johnson unaweza kufikia mpaka asilimia 80
Kuwepo kwa Kirusi Delta hakumaanishi vile Virusi vingine havipo
Mjadala huu unafanyika Agosti 6, 2021 kupitia Twitter Spaces (JamiiForums) kuanzia Saa 12 jioni na utahusisha Wataalamu wa Afya watakaozungumzia Masuala anuani kuhusu Janga hili
====
UPDATES;1800hrs
======
Kufuatilia mjadala huu, fungua hii link.
#UVIKO3
Je, ni lazima Mtu avae Gloves wakati wa kuchanja mtu?
Dr. Francis& Dr. Mariam: Kuvaa Gloves unatakiwa kila Gloves moja mtu mmoja, kwahiyo kwa siku mtu anayetoa chanjo anatakiwa avae Gloves 400. Hivyo kutokuvaa gloves ni rahisi hata kusafisha mikono kila baada ya kuchanja kuliko kuvua na kuvaa gloves. Pia muongozo wa Kuchanja unaruhusu kuchanja bila gloves.
Je, ni asilimia ngapi ya Watanzania Wachanje tuseme watu wengi wana kinga?
Dr. Mariam: Asilimia 70 hadi 80 ndo inashauriwa.
Dkt. Maryam: Watu wengi wanapokuwa hawana Chanjo ndivyo ambavyo Kirusi kinavyopata nafasi zaidi ya kuweza kubadilika
Hadi tutakapofikia 70% - 80% ya Watu waliopata Chanjo ndipo tunaweza kusema tumefanikiwa katika kupunguza Maambukizi
Dkt. Francis: Tunapozungumzia UVIKO19 kuna athari kubwa kwa Mtu na inaongeza mzigo kwenye utoaji huduma za Kiafya ikiwemo ICU na Oksijeni
Kwa hiyo wote tunaingia gharama kwasababu kuna Mtu atakosa Oksijeni akiwa na Magonjwa mengine sababu ya Mtu mwenye COVID19
Dkt. Maryam: Watu wengi wanapokuwa hawana Chanjo ndivyo Kirusi kinavyopata nafasi zaidi ya kuweza kubadilika
Hadi tutakapofikia 70% - 80% ya Watu kuwa wamepata Chanjo ndipo tunaweza kusema tumefanikiwa katika kupunguza Maambukizi
Dkt. Elisha: Nimeridhika na mwamko wa Watanzania kwenda kuchanjwa na naweza kusema mpaka hapa tulipofika ni 'success'
Tulipotoka Watu hata walikuwa hawaruhusiwi kuongelea #COVID19 huku wengine wakiwa kwenye Lockdown
Dkt. Francis: Watu wengi wanaogopa kwenda kuchanjwa kwasababu ya Uoga. Mitandao ya kijamii ina taarifa nyingi ambazo zimepotosha Watu
Mbele ni kuzuri ila cha msingi tuendelee kuwapa Watu taarifa sahihi. Mtu akiona mwenzie hajapata tatizo naye atakwenda kuchanjwa
Dkt. Norman: Ni ngumu kusema tumeridhika na mwamko wa Watanzania kwasababu hatuna Data za Dawa ngapi zilikuwepo na ngapi zimetoka
Ni matarajio yangu mpaka mwisho wa Mwaka Watu wote kwenye makundi Maalum watakuwa wamekuwa 'Covered'
Dkt. Norman: Kwa Dunia kasi ya uchanjaji inaendelea vizuri ambapo Mpaka Machi zilikuwa zimeshatoka dozi takriban bilioni 1.3
Kwetu tujitahidi ku-cover makundi Maalum. Afrika bado hakuna Nchi ambayo imeshafikia 5% ya Uchanjaji kwasababu Kampuni nyingi wanahodhi Chanjo
Dkt. Sajjad: Nimeridhika kwa kiasi fulani lakini bado tuna safari ndefu. Nimeridhika kwasababu kulikuwa a upotishaji. Baadhi ya Viongoxi walikuwa wanapotosha Jamii
Kuna mwamko sasa hivi, angalau tumefika sehemu nzuri. Ni jukumu letu sote kuelimisha jamii
Dkt. Maryam: Mtu ambaye ni Mgonjwa na yupo hoi Hospital hatakiwi kupata chanjo wakati huo bali asubiri mpaka Wiki 4 ndio apate Chanjo
Mtu anapokuwa anaumwa Mwili wake unakuwa unapambana na Maambukizi, akipewa Chanjo inakuwa inazidisha hali yake kuwa mbaya
Dkt. @amour_maryam: Mgonjwa mwenye maambukizi hai (active) yaani ana dalili za wazi hatakiwi kupata chanjo wakati huo bali asubiri mpaka Wiki 4
Kwa wakati huo mwili unakuwa unapambana na Maambukizi, akipewa Chanjo inakuwa inazidisha hali yake kuwa mbaya
Dkt. @furia_francis: Watu wanaopewa chanjo ni ambao hawana dalili, ukiwa mgonjwa huwezi kupata chanjo
Hakuna utaratibu kwamba tunawapima watu kabla ya kuwapa chanjo. Tunachoangalia ni dalili za ugonjwa, na tunauliza. Kama hauna dalili unaweza kupewa chanjo
Dkt. Maryam: Ukishapata Chanjo hakikisha unaendelea na taratibu zote za kujilinda ikiwemo kuvaa Barakoa
Kupata Chanjo haimaanishi uanze kujiachia. Ukikuta foleni kwenye Chanjo jitahidi kukaa mbali kidogo na Watu unapoendelea kusubiri
Dkt. @amour_maryam: Ukishapata Chanjo hakikisha unaendelea na taratibu zote za kujilinda ikiwemo kuvaa #Barakoa
Kupata Chanjo haimaanishi uanze kujiachia. Ukikuta foleni kwenye Chanjo jitahidi kukaa mbali kidogo na Watu unapoendelea kusubiri
Dkt. @SajjadFazel: Chanjo ya Johnson & Johnson ilisitishwa Marekani kwa muda ili kuangalia madhara waliyopata Watu ni kiasi gani
Baada ya utafiti waliridhika iko salama na imeendelea kutumika. Kusema tumeletea Chanjo iliyokataliwa sio sawa. WHO pia imeikubali ni salama
Dkt. Maryam: Ukishapata Chanjo hakikisha unaendelea na taratibu zote za kujilinda ikiwemo kuvaa Barakoa
Kupata Chanjo haimaanishi uanze kujiachia. Ukikuta foleni kwenye Chanjo jitahidi kukaa mbali kidogo na Watu unapoendelea kusubiri
Dkt. @amour_maryam: Ukishapata Chanjo hakikisha unaendelea na taratibu zote za kujilinda ikiwemo kuvaa #Barakoa
Kupata Chanjo haimaanishi uanze kujiachia. Ukikuta foleni kwenye Chanjo jitahidi kukaa mbali kidogo na Watu unapoendelea kusubiri
Dkt. Sajjad: Chanjo ya Johnson & Johnson ilisitishwa Marekani kwa muda ili kuangalia madhara waliyopata Watu ni kwa kiasi gani
Baada ya utafiti waliridhika iko salama na imeendelea kutumika. Kusema tumeletea Chanjo iliyokataliwa sio sawa. WHO pia imeikubali ni salama
Dkt. Norman: Chanjo inaenda kusisimua mwili, mara nyingi side effects zinaweza kutokea. Kuna baadhi ya watu kichwa kitauma, watasijikia kuchoka
Dalili hizi mara nyingi zinaisha ndani ya siku chache, zikiendelea ni vyema mtu akarudi kituo alichopata chanjo
Dkt. Sajjad: Sio kila anayepata Chanjo ya Coronavirus atapata tatizo la kuganda. Kuna sababu nyingi za Damu kuganda
Ukishapata Chanjo ikafika siku 6 - 15 tangu uchanjwe ukianza kuona dalili za kutokuona vizuri na maumivu kwenye Kifua ni vizuri kwenda Hospital haraka
Dkt. @SajjadFazel: Utafiti mbalimbali unafanyika duniani kuangalia hizi chanjo zinatoa kinga kwa kiasi gani dhidi ya Kirusi cha Corona aina ya Delta
Baadhi ya Chanjo mfano Johnson & Johnson inaweza kukupa kinga asilimia 60-70
Dkt. Maryam: Utafiti wa hivi karibuni unaonesha Effectiveness ya Chanjo ya Johnson&Johnson unaweza kufikia mpaka asilimia 80
Kuwepo kwa Kirusi Delta hakumaanishi vile Virusi vingine havipo