Yalitaka kutokea mauaji ya Halaiki Hapa Magomeni muda huu

Mtu Asiyejulikana

JF-Expert Member
Sep 11, 2017
1,694
3,981
Leo nimeamka nikiwa simple tu nilipigiwa simu ofisini nielekee sehemu moja Magomeni kwa shughuli za kikazi. Nilivaa vazi ambalo wengi husema asili yake ni uarabuni. Lakini mimi nilinunua duka la kihindi wanaita Punjab Style.

Ni mpenzi wa kuvaa hivyo huvaa nguo tofauti tofauti za tamaduni mbalimbali.Kuna siku unaweza nikuta nimevaa kimasai.

Nikiwa navuta muda kuweza onana na mtu wangu nikaona nishuke kwenye gari nikae sehemu moja wanauza chakula na nikaagiza soup ya mbuzi na chapati nne na maziwa fresh.

Nimekaa nakula akaja jamaa mmoja ananiita mimi kobe? Sukumwelewa anamaanisha nini.Baadaye mwingine pembeni ndo akanambia kwanini nakula hadharani? Nilimjibu ni haki yangu kula popote kwa wakati wowote.

Jamaa yule wa kwanza alitoka akaja na wenzie watatu wameshika bakora etu kuniadabisha kwa kuudhalilisha Uislamu. Jamaa wamekomaa hasa na bakora zao na imekuwa zogo.

Niliwaambia nataka nimwone wa kwanza kunichapa bakora.Nikasimama maana ndani ya ile nguo nimevaa kisuruali ambacho kina mifuko.Nikatoa silaha maana nilihisi wale jamaa wanataka kuhatarisha maisha yangu.

Hiyo ndo imekuwa ponea yangu sababu jamaa waliona nipo serious nami ningelazimika kufanya mauaji ya halaiki kwa wale jamaa maana walisha paniki bila sababu wanataka kuniadhibu for no reason.

Nauliza waungwana kuna kosa gani mimi kula mchana nikiwa nimevaa mavazi ambayo leo nimeambiwa ni ya kiislamu?mimi nafahamu wayahudi wanavaa hivi huko Israel. Nafahamu kuna wakristo wa kiarabu wanavaa hivi.

Kwanini hili vazi lionekane ni la dini fulani? Mimi binafsi sifungwi na dini nina imani yangu kwa Mungu lakini sibanwi na dini, sipendi unafiki.

Why waone nadhalilisha uislam wakati sikuongea neno lolote la kiislamu au sikufanya ishara yoyote ya kuonesha mimi ni mkristo au muislam?

Hizi akili hawa jamaa walitoa wapi kuona wanastahili kuniadhibu acha kuniita kobe sikuona issue sababu hata ukiniita shetani ikiwa najua mi si shetani siwezi gombana nawe.

Mi nadhani tuheshimiane na tuheshimu haki za watu wengine. Mimi nimekulia ktk mazingira ya kiislam naufahamu uislamu some how naufahamu ukristo some how. Tusitake kuendesheana maisha.

Leo kweli ngemchapa mtu risasi ya mguuni na ingekuwa gumzo. Najua kuna watu watakuwa wamechukua video tukio hilo. I dont care but nawaambia watu wasio na ustaarabu wasitumie dini vibaya.
 
Nakuwa wa kwanza ku comment. Heri yako uliye na paja la kuku na siye ambao hatutembei hata na mawe tungefanyaje? Watu waelewe kuwa nchi haina dini!!! Dini ni wewe na Mungu wako. Wengine hatujui hata makanisa na misikiti. Kuna Miti mikubwa tunaenda abudu inaitwa Ebigabilo hapo ndo yupo tunayemwomba.
 
Wajinga Sana Majamaa..

Mmoja alinikuta nimebeba likitabu lao la kijani kijani na maurembo wananaloliita Korani/Kuruani. Eti vile anajua Mimi Ni Mfuasi Wa Yesu aliyehai akaanza Kuhamaki na kuninyang'anya.

Nikamuambia kitabu Ni changu na nimenunua kwa hela yangu. Wakajikusanya pale mwanangu. Nikawauliza Uislamu Ni dini Ya Watu Wote? Wakajibu ndiyo.. nikawaambia basi Korani Pia ya Watu Wote!

Polisi walitokea pale ikabidi kila mmoja apite hivi kimya kimya.
 
Huyu mwanzishie uzi wake. Sababu mimi sidhani pia waliomkamata walikuwa ni wakristo sababu wangekuwa ni wapumbavu.ukristo haukatazi mtu aseme anachoamini. Ila unampa mkristo nafasi achambue jema na ovu.

Lakini siyo issue huyo deal naye yeye. Ila naamini alikamatwa kimakosa ikiwa sababu ni dini otherwise alikamatwa sababu ya kupotosha maadili ya kawaida tu wala si dini.

Kamtetee kwanza Nabii Tito maana kakamatwa wakati anahubiri kupitia Dini yake naye ni
Mchungaji kwenye kanisa lake.
 
huwezi kula supu (ya nyama) na maziwa fresh usiharishe. Huwa haishauriwi.
ni kama kulamba asali na muda huohuo utafune tango, lazima uage dunia.
E bwana ee hiv imekaaje hii ya kula tango halaf ukalamba sukari.logic yake ikoje na hiw is explained?
Maana kuna wakat huwa napata hofu wanangu wadogo wasio jua lolote ikatokea wamechanganya haya ma file halaf nikapata tabu mm
 
Aiseee.... Hapa ulitumia logic sijui kama walikuelewa.... Mimi hawa watu wanaodhani wanazijua dini sana kuliko wengine


Wajinga Sana Majamaa..

Mmoja alinikuta nimebeba likitabu la la kijani kijani na maurembo eanaoiita Korani/Kuruani eti vile anajua Mimi Ni Mfuasi Wa Yesu aliyehai akaanza Kuhamaki na kuninyang'anya.

Nikamuambia kitabu Ni change nimenunua kwa hela yangu wakajikusanya pale mwanangu. Nikawauliza Uislamu Ni Fini Ya Watu Wote? Wakajibu ndiyo.. nikawaambia basi Korani Pia ya Watu Wote!

Polisi walitokea pale ikabidi kila mmoja apite hivi kimya kimya.
 
92 Reactions
Reply
Back
Top Bottom