MsemajiUkweli
JF-Expert Member
- Jul 5, 2012
- 13,172
- 23,975
Kwa mtu anayechanganua masuala kwa undani utagundua kuwa matamko ya Ubalozi wa Marekani kuhusu kile walichokuwa wanakiita ''Hali mbaya ya maambukizo nchini'' kimepotea baada ya tamko lao la mwisho la mwezi Mei 2020.
Nadhani Ubalozi wa Marekani umegundua kuwa matamko hayo yalikuwa hayaisaidii Marekani kwa sababu walichokuwa wanakisema kilikuwa hakionekani kwenye uhalisia lakini kikubwa zaidi, balozi zingine kama za umoja wa Ulaya zilikuwa kimya.
Matamko ya mara kwa mara ya Ubalozi wa Marekani yalimuibua mwandishi kutoka Uholanzi wa kampuni ya habari, VOICE OF AMERICA aitwaye Ruud Elmendorp kufanya uchunguzi wa kina nchini ili kujua ukweli. Alitembelea mpaka makaburi mbali mbali nchini mara kwa mara hasa yaliyopo Dar es Salaam kuona kama kuna shughuli nyingi za mazishi lakini aligundua hakuna shughuli hizo.
Ukitaka kusoma habari na kuangalia video yake ya Uchunguzi unaweza kugonga LINK hii >>>COVID-19 Diaries: Can Tanzania Really Be Coronavirus-Free?
Kuna msema usemao, ''mficha maradhi kifo humuumbua''. Hii ina maana kuwa kama serikali ya Tanzania ilikuwa inaficha maradhi yatokanayo na COVID-19 basi vifo vya watu wengi vingeiumbua serikali.
Baada ya maambukizi ya COVID-19 kuanza kusambaa kwa kasi katika nchi za Afrika, nchi nyigi za Afrika zilijikuta zikifuata mfumo uliokuwa umependekezwa na WHO katika kukabiliana na janga hili lakini Serikali ya Tanzania iliamua kufuata mfumo tofauti ambao ulizishangaza nchi nyingi duniani lakini pia umesababisha kuzolota zaidi kwa mahusiano ya serikali ya Tanzania na serikali ya Kenya.
Maamuzi ya serikali sio kwamba yalizua mjadala mkubwa na mkali kwa jumuiya za kimataifa peke yake bali pia hata hapa nchini. Jukwaa la Jamiiforums halikubaki nyuma katika mjadala huo ambapo thread hii;
GONGA LINK>>>Janga la COVID-19: Naipongeza Serikali kwa kukataa kuiga baadhi ya mbinu za ’Nchi za Magharibi’ , iliyofunguliwa mwezi wa tatu ilichochea mjadala mkubwa na mkali kuhusu maamuzi ya serikali.
Mwana Jamiiforums Nyani Ngabu alikuwa ni mmoja wa Watanzania wa mwanzo kukubaliana na mtazamo wa Rais Magufuli katika mapambano ya Korona. Mwezi wa tatu alileta mada yenye kichwa cha habari, ''Kirusi kinachotisha kuliko Corona ni uoga/hofu. Baadhi ya wanajamii walipingana naye sana kuhusu mtazamo wake wengine wakimshambulia yeye badala ya hoja yake.
Mada yake hiyo inapatikana hapa, GONGA LINK>>>Kirusi kinachotisha kuliko Corona ni uoga/ hofu
Mwanajamiiforums mwingine Mzee Mwanakijiji alileta pia mada mwezi wa tatu kuhusu kile ambacho alikuwa anakiita maamuzi ya Rais Magufuli kuhusu Corona ni bahati na nasibu lakini akamalizia kwa kuuliza ITALIPA?
Ukitaka kusoma thread hiyo GONGA LINK>>>HOJA NDANI YA HOJA: Rais Magufuli na bahati nasibu ya korona - ITALIPA?
Mijadala hii ilikuwa inakolezwa na matamko yaliyokuwa yanatolewa mara kwa mara na Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania ambayo yalikuwa yakionyesha ''kuna hali mbaya'' ya maambukizi na vifo nchini.
Kwa sasa imepita miezi 6 tokea mijadala mikali itokee nchini na nje ya nchi kuhusu maamuzi ya Rais Magufuli kuhusiana na korona. Kinachoshangaza kwa sasa hata matamko ya Ubalozi wa Marekani nchini hayatolewi tena na hata wale ambao walikuwa wanakubaliana nayo huku wakimshutumu Rais Magufuli wamebadilisha mwelekeo kimya kimya baada ya kushindwa kupambana na ukweli halisi.
Je, Matamko ya Ubalozi wa Marekani yalikuwa yana malengo gani?
Kama matamko hayo yalikuwa yana malengo, Je, malengo yake yametimia ndio maana hayatolewi tena?
Je, waliokuwa wanakubaliana na matamko ya Ubalozi wa Marekani wamepotelea wapi?
Nadhani Ubalozi wa Marekani umegundua kuwa matamko hayo yalikuwa hayaisaidii Marekani kwa sababu walichokuwa wanakisema kilikuwa hakionekani kwenye uhalisia lakini kikubwa zaidi, balozi zingine kama za umoja wa Ulaya zilikuwa kimya.
Matamko ya mara kwa mara ya Ubalozi wa Marekani yalimuibua mwandishi kutoka Uholanzi wa kampuni ya habari, VOICE OF AMERICA aitwaye Ruud Elmendorp kufanya uchunguzi wa kina nchini ili kujua ukweli. Alitembelea mpaka makaburi mbali mbali nchini mara kwa mara hasa yaliyopo Dar es Salaam kuona kama kuna shughuli nyingi za mazishi lakini aligundua hakuna shughuli hizo.
Ukitaka kusoma habari na kuangalia video yake ya Uchunguzi unaweza kugonga LINK hii >>>COVID-19 Diaries: Can Tanzania Really Be Coronavirus-Free?
Kuna msema usemao, ''mficha maradhi kifo humuumbua''. Hii ina maana kuwa kama serikali ya Tanzania ilikuwa inaficha maradhi yatokanayo na COVID-19 basi vifo vya watu wengi vingeiumbua serikali.
Baada ya maambukizi ya COVID-19 kuanza kusambaa kwa kasi katika nchi za Afrika, nchi nyigi za Afrika zilijikuta zikifuata mfumo uliokuwa umependekezwa na WHO katika kukabiliana na janga hili lakini Serikali ya Tanzania iliamua kufuata mfumo tofauti ambao ulizishangaza nchi nyingi duniani lakini pia umesababisha kuzolota zaidi kwa mahusiano ya serikali ya Tanzania na serikali ya Kenya.
Maamuzi ya serikali sio kwamba yalizua mjadala mkubwa na mkali kwa jumuiya za kimataifa peke yake bali pia hata hapa nchini. Jukwaa la Jamiiforums halikubaki nyuma katika mjadala huo ambapo thread hii;
GONGA LINK>>>Janga la COVID-19: Naipongeza Serikali kwa kukataa kuiga baadhi ya mbinu za ’Nchi za Magharibi’ , iliyofunguliwa mwezi wa tatu ilichochea mjadala mkubwa na mkali kuhusu maamuzi ya serikali.
Mwana Jamiiforums Nyani Ngabu alikuwa ni mmoja wa Watanzania wa mwanzo kukubaliana na mtazamo wa Rais Magufuli katika mapambano ya Korona. Mwezi wa tatu alileta mada yenye kichwa cha habari, ''Kirusi kinachotisha kuliko Corona ni uoga/hofu. Baadhi ya wanajamii walipingana naye sana kuhusu mtazamo wake wengine wakimshambulia yeye badala ya hoja yake.
Mada yake hiyo inapatikana hapa, GONGA LINK>>>Kirusi kinachotisha kuliko Corona ni uoga/ hofu
Mwanajamiiforums mwingine Mzee Mwanakijiji alileta pia mada mwezi wa tatu kuhusu kile ambacho alikuwa anakiita maamuzi ya Rais Magufuli kuhusu Corona ni bahati na nasibu lakini akamalizia kwa kuuliza ITALIPA?
Ukitaka kusoma thread hiyo GONGA LINK>>>HOJA NDANI YA HOJA: Rais Magufuli na bahati nasibu ya korona - ITALIPA?
Mijadala hii ilikuwa inakolezwa na matamko yaliyokuwa yanatolewa mara kwa mara na Ubalozi wa Marekani nchini Tanzania ambayo yalikuwa yakionyesha ''kuna hali mbaya'' ya maambukizi na vifo nchini.
Kwa sasa imepita miezi 6 tokea mijadala mikali itokee nchini na nje ya nchi kuhusu maamuzi ya Rais Magufuli kuhusiana na korona. Kinachoshangaza kwa sasa hata matamko ya Ubalozi wa Marekani nchini hayatolewi tena na hata wale ambao walikuwa wanakubaliana nayo huku wakimshutumu Rais Magufuli wamebadilisha mwelekeo kimya kimya baada ya kushindwa kupambana na ukweli halisi.
Je, Matamko ya Ubalozi wa Marekani yalikuwa yana malengo gani?
Kama matamko hayo yalikuwa yana malengo, Je, malengo yake yametimia ndio maana hayatolewi tena?
Je, waliokuwa wanakubaliana na matamko ya Ubalozi wa Marekani wamepotelea wapi?