Yalaiti - Malika

Baba_Enock

JF-Expert Member
Aug 21, 2008
7,076
2,443
Kwa wale waliokuwepo enzi hizo hiki kitu kilivutia sana!
=================================================
Yalaiti napenda pasi kifani
tafauti sikutilii moyoni
sikuachi leo na kesho peponi
Ha ha ha I LOVE YOU

Ni la dhati kwa hakika pendo langu
sikufiti kwani ndicho kilimwengu
sikuwati mpaka mbele za mungu

Toa shaka na wasiwasi moyoni
kukwepuka hilo haliwezekani
takushika leo na kesho peponi

Lanishinda kuwa nawe mbali mbali
wangu nyonda amini naukubali
nakupenda wala sioni badali

Japo watu mno watatulaumu
sio kitu wala singiwe na hamu
pendo letu tulidumishe lidumu

Duniani naomba kwa mwenyeezi
maisha yadumu yetu mapenzi
na peponi tuwe sote laazizi

=================================================
Enjoy your Weekend
 
Kwa wale waliokuwepo enzi hizo hiki kitu kilivutia sana!
=================================================
Yalaiti napenda pasi kifani
tafauti sikutilii moyoni
sikuachi leo na kesho peponi
Ha ha ha I LOVE YOU

Ni la dhati kwa hakika pendo langu
sikufiti kwani ndicho kilimwengu
sikuwati mpaka mbele za mungu

Toa shaka na wasiwasi moyoni
kukwepuka hilo haliwezekani
takushika leo na kesho peponi

Lanishinda kuwa nawe mbali mbali
wangu nyonda amini naukubali
nakupenda wala sioni badali

Japo watu mno watatulaumu
sio kitu wala singiwe na hamu
pendo letu tulidumishe lidumu

Duniani naomba kwa mwenyeezi
maisha yadumu yetu mapenzi
na peponi tuwe sote laazizi

=================================================
Enjoy your Weekend


Swadakta
 
enzi hizo muziki wa taarab ulikuwa na heshima zake, sio siku hizi taarab ikianza kupigwa ukiwa jirani na watoto unazima redio
heheheheeeeeeeeeeee ni kweli kaka si afadhali watoto sema ukiwa na mama mkwe ni aibu na hizo nyonga /miuno yani ni aibu tupu,mimi naangalia Tv na kusikiliza radio chumbaniiiiiii kwa kuogopa hizo aibu za akina Mzee Yusuph,huyu mpemba katuletea balaa kwenye taarabu
 
Hivi huu wimbo nani aliyeutunga? Nimeusikia kwa Bi. Kidude ila kuna wanaosema na yeye amekopi kwa hayati Siti binti Saad.
 
Ila ni bikiduke aliyeuboresha

Alianza Hivi takadiriiii siwezi kuiepukaaa
Tasubiriiii litaklonifikaaaaa
 
Bi kidude anaimba
Wewe papa nakutuma kwa mkizi
Maneno kamwambie waziwazi
Kunikopa wala kunipa hawezi.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom