Watu wanaosadikika kuwa ni majambazi wamevamia ofisi ya Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT) Usharika wa King'ongo, Kimara Dar es Salaam na kupora vitu mbalimbali ikiwamo laptop na fedha Sh. 250,000.
Tukio hilo lilitokea saa 4:00 usiku wa kuamkia jana, baada ya majambazi kumjeruhi kwa rungu mlinzi wa kanisa hilo sehemu ya kichwani kisha kumfunga kamba mikononi na miguuni.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa msako wa kuwakamata waliohusika unaendelea.
Alisema majambazi wakiwa na silaha walivamia kanisa hilo na kupora baadhi ya vitu na kiasi hicho cha fedha.
Kiongozi wa usharika huo, mchungaji Joseph Kyaka, alisema alitapa taarifa za kuvamiwa kwa usharika huo saa tisa usiku kutoka kwa mmoja wa majirani na kanisa hilo.
Alisema alipofika kanisani alimkuta mlinzi akiwa amefungwa kamba sehemu za miguuni na mikononi huku akitokwa na damu sehemu za kichwani.
"Nilifika haraka kanisani na kumkuta mlinzi akiwa amefungwa kamba na mlango wa ofisi yangu na wa mhasibu ukiwa umevunjwa, laptop yangu imechukuliwa," alisema Mchungaji Kyaka.
Mlinzi wa Kanisa, Zakaria Mwangole, alisema walifika majambazi saba waliobeba silaha mbalimbali mmoja akiwa na bunduki, wakamvamia, wakamfunga kamba, wakamlaza chini na kuanza kubomoa milango ya ofisi ya mchungaji na mhasibu.
Shuhuda wa tukio hilo, Mlunge Macha, alisema alisikia kishindo eneo la kanisani, muda mfupi akasikia mlio wa risasi mbili zikipigwa hewani na kelele za mlinzi
Written by Wamtambwe // 05/02/2013 // Habari //
Tukio hilo lilitokea saa 4:00 usiku wa kuamkia jana, baada ya majambazi kumjeruhi kwa rungu mlinzi wa kanisa hilo sehemu ya kichwani kisha kumfunga kamba mikononi na miguuni.
Kamanda wa Polisi mkoa wa Kinondoni, Charles Kenyela, alithibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa msako wa kuwakamata waliohusika unaendelea.
Alisema majambazi wakiwa na silaha walivamia kanisa hilo na kupora baadhi ya vitu na kiasi hicho cha fedha.
Kiongozi wa usharika huo, mchungaji Joseph Kyaka, alisema alitapa taarifa za kuvamiwa kwa usharika huo saa tisa usiku kutoka kwa mmoja wa majirani na kanisa hilo.
Alisema alipofika kanisani alimkuta mlinzi akiwa amefungwa kamba sehemu za miguuni na mikononi huku akitokwa na damu sehemu za kichwani.
"Nilifika haraka kanisani na kumkuta mlinzi akiwa amefungwa kamba na mlango wa ofisi yangu na wa mhasibu ukiwa umevunjwa, laptop yangu imechukuliwa," alisema Mchungaji Kyaka.
Mlinzi wa Kanisa, Zakaria Mwangole, alisema walifika majambazi saba waliobeba silaha mbalimbali mmoja akiwa na bunduki, wakamvamia, wakamfunga kamba, wakamlaza chini na kuanza kubomoa milango ya ofisi ya mchungaji na mhasibu.
Shuhuda wa tukio hilo, Mlunge Macha, alisema alisikia kishindo eneo la kanisani, muda mfupi akasikia mlio wa risasi mbili zikipigwa hewani na kelele za mlinzi
Written by Wamtambwe // 05/02/2013 // Habari //