Yajue usiyoyafahamu kuhusu Vita ya Kagera

Ubavu

JF-Expert Member
Jun 19, 2012
2,791
3,236
Wakuu hapa nitawaletea matukio yote muhimu wakati wa vita hii ya Kagera. Sio kama mimi ndiye niliyeandika la hasha! Ninachokifanya mie ni kuwaletea hapa kutoka Gazeti la Mwananchi. Kaa nami upate uhondo huu.

Vita kati ya Tanzania na Uganda, au Vita ya Kagera ilidumu kwa miezi sita kuanzia Novemba 1978 hadi Aprili 1979. Vita hiyo ndiyo iliyouangusha utawala wa Idi Amin Dada uliodumu kwa muda wa miaka minane.

Idd Amin aliingia madarakani Jumatatu ya Januari 25, 1971 alipoiangusha serikali ya Dk Milton Obote na aliondoka Jumatano ya Aprili 11, 1979 wakati majeshi ya Tanzania na ya Uganda yaliposhirikiana kumuondoa.

Mgogoro wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Uganda ulianza Jumatatu ya Januari 25, 1971 baada ya Amin kuipindua Serikali ya Dk Obote. Muda mfupi baada ya hapo, Rais wa Tanzania alimpa Dk Obote hifadhi ya kisiasa. Akiwa Tanzania Dk Obote alianza mipango ya kurejea Uganda akitumia ardhi ya Tanzania.

Mambo mengi ambayo yangeweza kusababisha Vita ya Kagera yalikuwa yametendeka tangu Januari 1971 hadi Oktoba 1978, lakini kwa kipindi chote hicho hakuna vita iliyozuka.

Vita hiyo ilianza rasmi siku ileile ya maadhimisho ya Uhuru wa Uganda, yaani Jumatatu ya Oktoba 9, 1978 baada ya mwanajeshi mmoja wa Uganda kuvuka mpaka na kuingia Tanzania kupata kinywaji na kukutana na mpenzi wake ambaye alikuwa raia wa Tanzania.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Monitor la Uganda la Jumanne ya Oktoba 9, 2017, wakati mwanajeshi huyo akiwa mpakani upande wa Tanzania kwa starehe zake, alijikuta akipambana na wanausalama wa Tanzania.

Mwanajeshi huyo alikamatwa na kuwekwa rumande. Mapema asubuhi ya siku iliyofuata, aliachiwa aondoke. Kwa kudhani amedhalilishwa na wanausalama wa Tanzania, alikimbilia kambini kwake upande wa Uganda, akachukua bunduki na kurejea upande wa Tanzania kulipiza kisasi.

Alipofika umbali fulani kutoka kituo alichokuwa ameshikiliwa, alifyatua risasi kwa mbali. Askari wa zamu wa kituo hicho walilazimika kukimbia. Hakuna hata mmoja aliyejeruhiwa.

Alipojisikia vizuri kwa kitendo hicho, aliamua kurejea kambini kwake upande wa Uganda na kumdanganya kamanda wa kikosi chake aliyejulikana kwa jina la Luteni Byansi kwamba alitekwa na askari wa Tanzania, lakini akapambana nao.

Bila kutafakari sana, Luteni Byansi alimpigia simu Kamanda wa Kikosi cha Malire (MMRR) kilichoko Lubiri mjini Kampala, Kanali Juma Ali Oka (alikuwa maarufu kama Juma Butabika).

Bila kuwajulisha maofisa wa ngazi za juu wa Jeshi la Uganda (UPDF), Kanali Butabika aliviamuru vikosi vya jeshi vilivyokuwa Ziwa Victoria kwenda kuongeza nguvu kwenye kikosi cha Luteni Byansi kuishambulia Tanzania.

“Nilikuwa kamanda wa kwanza wa vifaru kuingia Tanzania. Tuliamriwa kushambulia. Tulikaa Tanzania kwa wiki mbili kabla ya kuamriwa kuondoka na kurejea Uganda,” Luteni Muzamir Amule wa UPDF alimwambia mwandishi Faustine Mugabe wa Daily Monitor katika mahojiano aliyofanyiwa mwaka 2015 nchini Uganda.

Kwa maoni yake, Kanali Butabika aliingiza Uganda vita isiyo na ulazima wowote.

“Unawapelekaje vitani wanajeshi kutoka Malire (Kampala) hadi Mutukula (Tanzania) bila kumtaarifu Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama au hata kamanda yeyote wa juu wa jeshi?” anahoji Luteni Amule katika habari hiyo.

Ijumaa ya Oktoba 27, 1978, mara baada ya uamuzi wa Kanali Juma Butabika, zilitumwa ndege tatu za kivita aina ya ‘MiG-21’ (Mikoyan-Gurevich) za Kirusi. Marubani bora zaidi wa ndege hizo nchini Uganda, Luteni David Omita, Luteni Atiku na Luteni Abusala walichaguliwa kwa kazi hiyo maalumu.

Kumbukumbu nyingine zinaonyesha kulikuwa na rubani mwingine aliyeitwa Walugembe. Mwaka mmoja kabla, marubani hao watatu—Luteni Omita, Luteni Atiku na Luteni Abusala—walikuwa wamerejea kutoka mafunzoni nchini Urusi.

Uganda ilinunua ndege 20 za aina hiyo mwaka 1977 kuziba pengo la zile aina ya MiG-15 zilizoharibiwa Jumapili ya Julai 4, 1976, wakati makomandoo wa Israel walipoivamia Uganda katika shambulio linalojulikana kama Operation Entebbe.

Ndege hizo zilipaa kutoka Entebbe kwenda kuishambulia Tanzania. Ndani ya muda mfupi zikawa zimeshambulia na kurejea Uganda.

Zilipogeuka, ndege ya Luteni Omita ilipigwa kombora na wanajeshi wa Tanzania. Kombora hilo liliharibu bawa lake la kushoto na ikashika moto. Lakini kati ya sekundi chache kabla ya kushika moto, Luteni Omita alifanikiwa kuruka kwa parachuti.

Hadi wanajeshi wa Tanzania wanafika yalipokuwa mabaki ya ndege hiyo, rubani huyo alikuwa ameshatoweka.

Nchini Uganda, wanajeshi wenzake wakiamini kuwa Luteni Omita ameuawa na majeshi ya Tanzania, walimwona akirejea kambini kwa mguu. Baadaye alipelekwa Entebbe kukutana na Idi Amin ambaye alimpongeza kwa ujasiri wake.

Jumapili ya Oktoba 29, 1978, kwa mujibu wa matangazo ya kituo cha redio cha Voice of Uganda ya Oktoba 30, 1978, Idi Amin aliwapandisha vyeo Omita, Atiku, Abusala na Walugembe kuwa makanali na kuwafanyia tafrija.

Tafrija ya kuwapandisha vyeo ilifanyika mjini Entebbe kwenye Uwanja wa Ndege wa Jeshi.

Wakati Idi Amin akiwa katika sherehe hiyo, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lilifanya shambulio lake la kwanza kabisa eneo la Kikagati ndani ya Uganda na kuingia kilometa kadhaa bila ya upinzani wowote.

Itaendelea kesho
Source Mwananchi la leo 10 Dec 2018
 
Itaendelea kesho

Okay well, itaendelea kesho, lakini itakapoendelea kesho ulete narative sahihi kuhusu muamuzi wa Uganda aliyewaleta vitani.

Kusema Kanali Juma wa kikosi cha Malire ndio aliamua Uganda ije vitani Tanzania bila kupata sahihi, dokezo, baraka wala hata kujulishwa dikteta Iddi Amini Dada is simply ridiculous.

Nduli Amini hawezi kusafishwa kwa kumlaumu Kanali Juma wa Uganda kwamba ndie aliyeamua vita kwa sababu Amini alikuwa ameshaeleza mapema sana kwamba anakwenda kuishambulia Tanzania siku za usoni.

Kwanza Iddi Amini mwenyewe alionyesha mwili wa kamanda wa polisi wa Tanzania, RPC Pope wa Ziwa Magharibi, aliyeuawa na Waganda kabla ya mwaka 1978. Vita iliamuliwa na Amini.
 
Sehemu ya Pili

Jana tuliona jinsi luteni wa Jeshi la Uganda alivyosababisha Uganda iishambulie Tanzania baada ya kuingia katika mzozo na wanausalama wa Tanzania wakati alipovuka mpaka kuja nchini kunywa pombe. Askari huyo alikamatwa na baadaye kuachiwa, lakini alidanganywa kuwa alitekwa na akapambana nao. Sasa endelea...

Mbali na nchi jirani kama Malawi, Kenya, Zaire (Congo DRC) na Msumbiji, eneo moja lililokuwa katika hatari kubwa ya kushambuliwa na maadui wa nje ni mpaka wa Uganda na Tanzania, lakini haukulindwa vya kutosha.

Chokochoko kati ya Tanzania na Uganda zilianza mwaka 1971. Mwaka uliofuata kukawa na makubaliano yaliyojulikana kama ‘Mazungumzo ya Mogadishu’ yaliyofanyika nchini Somalia Alhamisi ya Oktoba 5, 1972.

Mazungumzo hayo yalikuwa ni usuluhishi wa mgogoro kati ya Tanzania na Uganda. Kwa maana hiyo, Somalia iliepusha vita kati ya Tanzania na Uganda kwa miaka sita tangu 1972 hadi hali ilipovurugika mwaka 1978.

Walioshiriki katika mazungumzo hayo ni mawaziri wa mambo ya nje, ambao ni John Samuel Malecela (Tanzania), Joshua Wanume Kibedi (Uganda) na Umar Arteh Ghalib au Omer Carte Qalib (Somalia). Mwingine ni katibu mkuu wa Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU), Nzo Ekangaki.

Mazungumzo ya Mogadishu yalifikia makubaliano kwamba majeshi ya Tanzania yakae kilomita 16 au zaidi kutoka mpaka wa Uganda. Lakini hata nje kabisa ya umbali huo, Jeshi la Tanzania halikuwako. Hilo linadokeza kwamba Tanzania haikufikiria kuwa Idi Amin angeishambulia Tanzania.

Kikosi kilichokuwa na jukumu la kuulinda mpaka wa Uganda ni Brigedi ya 202 ya Tabora chini ya Brigedia Yusuf Himid, ambaye alikuwa akisimamia Kanda ya Magharibi.

Mpakani palikuwa na batalioni ya tatu, yaani kikosi cha askari ambacho kina kombania kadhaa na ambacho ni sehemu ya brigedi au rejimenti. Hiki kilikuwa chini ya Luteni Kanali Morris Singano, ambaye miezi miwili kabla alihamishwa kutoka Mbeya kwenda Kanda ya Ziwa.

Mara baada ya zile ndege tatu za kivita za Uganda zilizoishambulia Tanzania zikiendeshwa na maluteni David Omita, Atiku na Abusala, Singano alituma taarifa hizo Brigedi ya Tabora, lakini Brigedi ilifikiria anachofanya Idi Amin ni kilekile alichokuwa akikifanya kwa zaidi ya miaka sita, kumbe hali ilikuwa tofauti.

Alhamisi ya Oktoba 20, 1978, baada ya mji wa Bukoba kushambuliwa, Mkuu wa Mkoa wa Kagera wakati huo ukiitwa Ziwa Magharibi, Mohamed Nassoro Kissoky, aliitisha mkutano wa viongozi wa CCM na Serikali na kuwaambia kwamba kinachoendelea mpakani ni hali ya kutoelewana tu na kwa sababu hiyo hakuna haja ya kuwa na hofu.

Kissoky aliwasihi viongozi hao wawaambie wananchi kuwa, “sisi ni marafiki wa Uganda na Idi Amin alikuwa mpakani akishikana mikono na watu wetu”.

Lakini wananchi wengi hawakuridhishwa na maneno ya Kissoky kwa sababu ndege za Amin zilikuwa zikionekana mara kwa mara na bado kulikuwa na wasiwasi wa mashambulizi mengine.

Kwa muda wote huu, ukiacha kauli ya Kissoky, hakuna ofisa mwingine yeyote wa CCM wala Serikali ambaye alikuwa ametoa kauli yoyote hadharani kuhusu kinachoendelea kati ya Tanzania na Uganda.

Jumapili ya Oktoba 22,1978 kundi la wanajeshi wa Uganda lilivuka mpaka kuingia Tanzania kunywa pombe. Waliendelea kunywa hadi askari wa Tanzania walipoingia eneo hilo. Huku wakiwa wameanza kulewa, walianza kufyatua risasi ovyo. Askari wa Tanzania nao wakajibu mapigo. Katika mapambano hayo mwanajeshi mmoja wa Uganda aliuawa.

Siku tatu baadaye, asubuhi ya Jumatano ya Oktoba 25, ikaripotiwa kuwa Mutukula ilikuwa ikishambuliwa vikali. Ingawa Kanali Singano alikuwa na wanajeshi wachache na alielekea kuzidiwa, alifanikiwa kunasa mawimbi ya redio iliyokuwa ikitumiwa na Jeshi la Uganda kutokea Kampala.

Kwa mujibu wa kitabu War in Uganda: The Legacy of Idi Amin, mawasiliano ya redio yalifanywa na Luteni Kanali Marajani. Lakini Uganda hawakuweza kuyanasa.

Asubuhi ya Ijumaa ya Oktoba 27, ndipo ndege tatu za kivita za Uganda aina ya MiG-21 ziliposhambulia mji wa Bukoba. Kombora moja kutoka katika ndege hizo lilianguka mita chache kutoka ilipo Hospitali ya Bukoba. Mojawapo ya ndege hizo ilitunguliwa.

Kwa wakati wote huu, vyombo vya habari vya Tanzania havikutangaza chochote kuhusu matukio hayo. Habari za matukio hayo zilisambazwa na wale waliokuwa wakikimbia vita.

Ingawa madhara hayakuwa makubwa, shambulio la Bukoba lilifanya raia kutaharuki na wengi kuukimbia mji. Hadi jioni ya siku hiyo, barabara zote za kutoka Bukoba zikawa zimefurika watu.

Jumatatu, asubuhi ya Oktoba 30 maelfu ya wanajeshi wa Uganda waliingia tena Tanzania kupitia maeneo manne—Kukunga, Masanya, Mutukula na Minziro. Raia wa Tanzania waliojaribu kupambana na majeshi hayo waliuawa.

Mamia ya wananchi wa Tanzania, hususan wanawake, walichukuliwa mateka na kupelekwa Uganda kwenye kambi ya Kalisizo. Kwa mujibu wa kitabu Great Britain’s Policy on the Uganda-Tanzania War (1978-9) cha Elisabeth Stennes Skaar, baada ya kuteka eneo lenye ukubwa wa kilomita 1,800 za mraba, wanajeshi wa Uganda walianza kupora, kubaka na kuua.

Kwa mujibu wa kijitabu cha Daniel Acheson-Brown cha The Tanzanian Invasion of Uganda: A Just War? kwa siku hiyo moja tu zaidi ya Watanzania 1,500 waliuawa. Wanajeshi wa Uganda walipora kila walichoweza kupora, yakiwamo magari. Na magari ambayo yalikuwa mabovu, yaling’olewa vipuri. Uporaji huo ulihusisha hata masufuria na vijiko jikoni.

Kiwanda cha Sukari cha Kagera kiliathirika zaidi na uporaji huo pamoja na ranchi ya Mishenyi. Mifugo iliyoporwa Kagera ikapelekwa Mbarara, Uganda ambako iligawiwa kwa askari na ndugu na marafiki wao.

Baadaye siku hiyo, Redio Uganda ikatangaza kulikomboa eneo la Kagera na kusema sasa mpaka halali wa Tanzania na Uganda ni Mto Kagera. Idi Amin mwenyewe alizuru eneo hilo na kupiga picha na silaha zilizoachwa na wanajeshi wa Tanzania waliokimbia.

Habari za kutekwa kwa Kagera zikamfikia Mwalimu Julius Nyerere. Jumatatu ya Oktoba 30, 1978 Mwalimu Nyerere aliwaita makamanda wa JWTZ nyumbani kwake. Miongoni mwao alikuwa Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama, Luteni Jenerali Abdallah Twalipo.

Mkutano huo kati ya Mwalimu Nyerere na makamanda wa jeshi ulimalizika saa nne asubuhi, Mwalimu aliamuru kazi ianze mara moja. Siku iliyofuata, Jumanne ya Oktoba 31, katika taarifa ya habari ya saa 1:00 asubuhi, Redio Tanzania Dar es Salaam ilitangaza kwa mara ya kwanza matukio ya kivita katika mpaka wa Tanzania na Uganda.

Itaendelea kesho

Source: Mwananchi la leo.
IMG_20181211_080548.jpeg
vitapic.jpeg
 
Wakuu hapa nitawaletea matukio yote muhimu wakati wa vita hii ya Kagera. Sio kama mimi ndiye niliyeandika la hasha! Ninachokifanya mie ni kuwaletea hapa kutoka Gazeti la Mwananchi. Kaa nami upate uhondo huu.

Vita kati ya Tanzania na Uganda, au Vita ya Kagera ilidumu kwa miezi sita kuanzia Novemba 1978 hadi Aprili 1979. Vita hiyo ndiyo iliyouangusha utawala wa Idi Amin Dada uliodumu kwa muda wa miaka minane.

Idd Amin aliingia madarakani Jumatatu ya Januari 25, 1971 alipoiangusha serikali ya Dk Milton Obote na aliondoka Jumatano ya Aprili 11, 1979 wakati majeshi ya Tanzania na ya Uganda yaliposhirikiana kumuondoa.

Mgogoro wa kidiplomasia kati ya Tanzania na Uganda ulianza Jumatatu ya Januari 25, 1971 baada ya Amin kuipindua Serikali ya Dk Obote. Muda mfupi baada ya hapo, Rais wa Tanzania alimpa Dk Obote hifadhi ya kisiasa. Akiwa Tanzania Dk Obote alianza mipango ya kurejea Uganda akitumia ardhi ya Tanzania.

Mambo mengi ambayo yangeweza kusababisha Vita ya Kagera yalikuwa yametendeka tangu Januari 1971 hadi Oktoba 1978, lakini kwa kipindi chote hicho hakuna vita iliyozuka.

Vita hiyo ilianza rasmi siku ileile ya maadhimisho ya Uhuru wa Uganda, yaani Jumatatu ya Oktoba 9, 1978 baada ya mwanajeshi mmoja wa Uganda kuvuka mpaka na kuingia Tanzania kupata kinywaji na kukutana na mpenzi wake ambaye alikuwa raia wa Tanzania.

Kwa mujibu wa gazeti la Daily Monitor la Uganda la Jumanne ya Oktoba 9, 2017, wakati mwanajeshi huyo akiwa mpakani upande wa Tanzania kwa starehe zake, alijikuta akipambana na wanausalama wa Tanzania.

Mwanajeshi huyo alikamatwa na kuwekwa rumande. Mapema asubuhi ya siku iliyofuata, aliachiwa aondoke. Kwa kudhani amedhalilishwa na wanausalama wa Tanzania, alikimbilia kambini kwake upande wa Uganda, akachukua bunduki na kurejea upande wa Tanzania kulipiza kisasi.

Alipofika umbali fulani kutoka kituo alichokuwa ameshikiliwa, alifyatua risasi kwa mbali. Askari wa zamu wa kituo hicho walilazimika kukimbia. Hakuna hata mmoja aliyejeruhiwa.

Alipojisikia vizuri kwa kitendo hicho, aliamua kurejea kambini kwake upande wa Uganda na kumdanganya kamanda wa kikosi chake aliyejulikana kwa jina la Luteni Byansi kwamba alitekwa na askari wa Tanzania, lakini akapambana nao.

Bila kutafakari sana, Luteni Byansi alimpigia simu Kamanda wa Kikosi cha Malire (MMRR) kilichoko Lubiri mjini Kampala, Kanali Juma Ali Oka (alikuwa maarufu kama Juma Butabika).

Bila kuwajulisha maofisa wa ngazi za juu wa Jeshi la Uganda (UPDF), Kanali Butabika aliviamuru vikosi vya jeshi vilivyokuwa Ziwa Victoria kwenda kuongeza nguvu kwenye kikosi cha Luteni Byansi kuishambulia Tanzania.

“Nilikuwa kamanda wa kwanza wa vifaru kuingia Tanzania. Tuliamriwa kushambulia. Tulikaa Tanzania kwa wiki mbili kabla ya kuamriwa kuondoka na kurejea Uganda,” Luteni Muzamir Amule wa UPDF alimwambia mwandishi Faustine Mugabe wa Daily Monitor katika mahojiano aliyofanyiwa mwaka 2015 nchini Uganda.

Kwa maoni yake, Kanali Butabika aliingiza Uganda vita isiyo na ulazima wowote.

“Unawapelekaje vitani wanajeshi kutoka Malire (Kampala) hadi Mutukula (Tanzania) bila kumtaarifu Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama au hata kamanda yeyote wa juu wa jeshi?” anahoji Luteni Amule katika habari hiyo.

Ijumaa ya Oktoba 27, 1978, mara baada ya uamuzi wa Kanali Juma Butabika, zilitumwa ndege tatu za kivita aina ya ‘MiG-21’ (Mikoyan-Gurevich) za Kirusi. Marubani bora zaidi wa ndege hizo nchini Uganda, Luteni David Omita, Luteni Atiku na Luteni Abusala walichaguliwa kwa kazi hiyo maalumu.

Kumbukumbu nyingine zinaonyesha kulikuwa na rubani mwingine aliyeitwa Walugembe. Mwaka mmoja kabla, marubani hao watatu—Luteni Omita, Luteni Atiku na Luteni Abusala—walikuwa wamerejea kutoka mafunzoni nchini Urusi.

Uganda ilinunua ndege 20 za aina hiyo mwaka 1977 kuziba pengo la zile aina ya MiG-15 zilizoharibiwa Jumapili ya Julai 4, 1976, wakati makomandoo wa Israel walipoivamia Uganda katika shambulio linalojulikana kama Operation Entebbe.

Ndege hizo zilipaa kutoka Entebbe kwenda kuishambulia Tanzania. Ndani ya muda mfupi zikawa zimeshambulia na kurejea Uganda.

Zilipogeuka, ndege ya Luteni Omita ilipigwa kombora na wanajeshi wa Tanzania. Kombora hilo liliharibu bawa lake la kushoto na ikashika moto. Lakini kati ya sekundi chache kabla ya kushika moto, Luteni Omita alifanikiwa kuruka kwa parachuti.

Hadi wanajeshi wa Tanzania wanafika yalipokuwa mabaki ya ndege hiyo, rubani huyo alikuwa ameshatoweka.

Nchini Uganda, wanajeshi wenzake wakiamini kuwa Luteni Omita ameuawa na majeshi ya Tanzania, walimwona akirejea kambini kwa mguu. Baadaye alipelekwa Entebbe kukutana na Idi Amin ambaye alimpongeza kwa ujasiri wake.

Jumapili ya Oktoba 29, 1978, kwa mujibu wa matangazo ya kituo cha redio cha Voice of Uganda ya Oktoba 30, 1978, Idi Amin aliwapandisha vyeo Omita, Atiku, Abusala na Walugembe kuwa makanali na kuwafanyia tafrija.

Tafrija ya kuwapandisha vyeo ilifanyika mjini Entebbe kwenye Uwanja wa Ndege wa Jeshi.

Wakati Idi Amin akiwa katika sherehe hiyo, Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lilifanya shambulio lake la kwanza kabisa eneo la Kikagati ndani ya Uganda na kuingia kilometa kadhaa bila ya upinzani wowote.

Itaendelea kesho
Source Mwananchi la leo 10 Dec 2018
Dah
Kama history ingekuwa ina fundishwa kiundan Kama hivi madogo wasinge feli shulen
 
Back
Top Bottom