Yajue masharti ya kufuga njiwa: Hawapendi Umbea na Ulevi

Njiwa nimefuga sana na aina ya Njiwa mimaowapenda

1 White

2 Manga

3 Fungo

4 Adidas

5 Tizeti

6 Chotara
 
Ukiachana tofauti ya bei ya njiwa huanzia elfu 10 pair moja ya njiwa Wa kawaida, elfu 60 kwa wale weupe, na wengine wapo wanauzwa hadi laki 8 kwa pair moja!

(Kazi moja ya njiwa ni urembo,burudani,kitowewo na baraka)

Kabla ya kufuga njiwa hao ni vyema sasa kutambua masharti yao;
  1. Kwanza kabisa njiwa ukiwanunua kutoka kwa mtu, sharti wawe wawili pair (dume na jike)
  2. Kama muuzaji aliwafuga kwa banda la juu, hakikisha unakowapeleka uwaandalia banda la juu, ukiwaweka banda la chini wanaondoka
  3. Kama banda lako la chini, tafta muuzaji mwenye banda chini ndipo ununue vinginevyo unashauliwa uwanyonyoe manyoya na kuwafungia siku 40 kabla ya kuwafungulia.
  4. Njiwa wakiwa mbele yako usipende kuwajadili, hawapendi masimango wataondoka!
  5. Ukifuga njiwa nao hufatilia nyendo zako, ukiwa mlevi hawakai wanaondoka kwasababu wanaamini mlevi anaweza sahau kuwafungulia bandani siku moja
  6. Njiwa wana nguvu kiimani, hawapendi mfugaji awe mmbeya kugombana na majilani, kwasababu wakati Wa ugomvi njiwa hukaa juu ya paa wakisikiliza halafu huondoka na hawarudi tena
  7. Njiwa hawapendi kuona Umechinja njiwa mwenzao mbele yao, wakiona wanahama wote kwasababu wanahisi utawachinja.
  8. Njiwa hawapendi Makelele ya kushtukiza kama honi Kali, kuwarushia jiwe na miziki mikubwa, ukifanya hivyo wanahama
  9. Njiwa akifa mmoja, huomboleza, unashauliwa umtaftie mwenza haraka kwa njiwa anaebaki la sivyo wanaondoka
  10. Hakikisha njiwa huwachanganyi na kuku mwenye vifaranga, wakipararuliwa huondoka mazima.
  11. Njiwa wanaofugwa banda la uani/nyuma/jikoni huzaliana haraka zaidi kwasababu ya mazingira tulivu
  12. Hakikisha pakashume hawazoei kufika nyumbani kwako! njiwa hawapatani na paka pori la sivyo wanahama wote!
  13. Inasemekana njiwa ni Wa pili kwa wivu baada ya nyegele! Hakikisha unafuga wawiliwawili.
Hayo ni machache tu kati ya masharti ya njiwa!!!
View attachment 1101970
Naomba kufahamu njiwa wanafaa kabisa kula kama kitoweo au wanafugwa kama mapambo tu?
 
Zinakusaidia nn njiwa kufuga mkuu??🤔🤔.au mie siko sawa...!ndo nyie mnaofuga mende ati wana soko😅..mbona kuna mambo mengi ya kifanya jaman😅😅
FaizaFoxy kanihamasisha kufuga, manake kasema nyama yao tamu balaa!!! Yaani tayari nishaanza kujenga picha kichwani jinsi nitakavyokuwa nakula njiwa za kuchoma kila Jmosi na Jpili!
 
Ukiachana tofauti ya bei ya njiwa huanzia elfu 10 pair moja ya njiwa Wa kawaida, elfu 60 kwa wale weupe, na wengine wapo wanauzwa hadi laki 8 kwa pair moja!

(Kazi moja ya njiwa ni urembo,burudani,kitowewo na baraka)

Kabla ya kufuga njiwa hao ni vyema sasa kutambua masharti yao;
  1. Kwanza kabisa njiwa ukiwanunua kutoka kwa mtu, sharti wawe wawili pair (dume na jike)
  2. Kama muuzaji aliwafuga kwa banda la juu, hakikisha unakowapeleka uwaandalia banda la juu, ukiwaweka banda la chini wanaondoka
  3. Kama banda lako la chini, tafta muuzaji mwenye banda chini ndipo ununue vinginevyo unashauliwa uwanyonyoe manyoya na kuwafungia siku 40 kabla ya kuwafungulia.
  4. Njiwa wakiwa mbele yako usipende kuwajadili, hawapendi masimango wataondoka!
  5. Ukifuga njiwa nao hufatilia nyendo zako, ukiwa mlevi hawakai wanaondoka kwasababu wanaamini mlevi anaweza sahau kuwafungulia bandani siku moja
  6. Njiwa wana nguvu kiimani, hawapendi mfugaji awe mmbeya kugombana na majilani, kwasababu wakati Wa ugomvi njiwa hukaa juu ya paa wakisikiliza halafu huondoka na hawarudi tena
  7. Njiwa hawapendi kuona Umechinja njiwa mwenzao mbele yao, wakiona wanahama wote kwasababu wanahisi utawachinja.
  8. Njiwa hawapendi Makelele ya kushtukiza kama honi Kali, kuwarushia jiwe na miziki mikubwa, ukifanya hivyo wanahama
  9. Njiwa akifa mmoja, huomboleza, unashauliwa umtaftie mwenza haraka kwa njiwa anaebaki la sivyo wanaondoka
  10. Hakikisha njiwa huwachanganyi na kuku mwenye vifaranga, wakipararuliwa huondoka mazima.
  11. Njiwa wanaofugwa banda la uani/nyuma/jikoni huzaliana haraka zaidi kwasababu ya mazingira tulivu
  12. Hakikisha pakashume hawazoei kufika nyumbani kwako! njiwa hawapatani na paka pori la sivyo wanahama wote!
  13. Inasemekana njiwa ni Wa pili kwa wivu baada ya nyegele! Hakikisha unafuga wawiliwawili.
Hayo ni machache tu kati ya masharti ya njiwa!!!
View attachment 1101970
Chai imezidi sana

Nimefuga njiwa kwa miaka Chief

Ila si kwa masharti haya
 
Mi naombeni njia za kuwatimua tuu,wamehamia kwangu na wamezaliana mnoo,kila siku wanadondosha ceilling board za kuzunguka nyumba,nawatwanga manati ila ndio kama nimewaongezea kasi ya kuzaliana...
plus kuchafua kuta kwa kinyesi kama popo
 
Nyongeza:
Hawapendi kusikia sauti za mahaba/za kubanjuana toka kwa binadamu.
Inashauriwa kuweka banda lao mbali na vyumba vya watu wazima ambao daily wanagegedana tena kavukavu.
Usipofanya hivyo njiwa watatomb@n@ sana na kushindwa kupata muda wa kula na hatimaye kufa wote kwa njaa!!
Eh!
 
28 Reactions
Reply
Back
Top Bottom