Yajue masharti ya kufuga njiwa: Hawapendi Umbea na Ulevi

Hahaha ulijuaje mkuu? Mimi kaka yangu alikua anafungua kale kadirisha wanachopitia na anchotumia kuwapa chakula bas mara mnaona njiwa mgeni juu ya paa mara kaingia akishaingia anafunga hicho kidirisha anafungua mlango mkubwa anamnyonyoa mabawa anakua tayar kishamteka nilikua nainjoi sana the way wanafuga ilifikia point akiwafungulia wanamrukia mkononi hivi anawaita ana mluzi anapiga hata kama wako mbali watakuja na hadleo wanafuga walinifundisha pia jinsi ya kumjua jike na dume na njiwa ni waoga sana
umenikumbusha mbali...mateka. Alaf kuna mafundi wa kuteka. Ni kukaa karib na kaka zako ama?kwenye jamii yetu nayoishi haya ya njiwa ni michezo ya vijana wa kiume
 
Mengi uliyoandika ni uongo,nimefunga njiwa kwa zaidi ya miaka mitano(ni miaka 16 leo lakini kumbukumbu zao ninazo,baada ya kwenda shule mbali nje na nyumbani wakaisha maana walikoswa msimamizi.
 
14. Njiwa ukitaka kuwashika kwajili yakuuza , kuchinja, unatakiwa uwashike usiku sababu usiku huwa hawaoni...ukimshika mmoja mchana wanaobaki wakiona huondoka wote
 
Porojo tupu. Mie nafuga njiwa tena wengi sana, hawa wa kawaida, wana rangi na patterns mbali mbali na wengine ni weupe kabisa. Nilianza na wanne tu baada ya mwaka wakawa zaidi ya 30, sasa hivi wanazidi 300, siwezi kuwahesabu.

Wanaishi juu ya banda kubwa la kuku, walivyo kuwa wanazidi nikawawekea dari za mbao za marine ambazo nimeziongezea coat ya waterproof hardner.

Kitoweo kitamu sana. Siku nikitamani huwa nachinja 20 mpaka 30, Na nimegawa wengi sana na nimeuza wengi sana.

Wao mradi chakula kwa wingi (Mtama, choroko, kundi) na maji safi ya kutosha kwenye mabeseni, wanapenda sana kuoga kwenye maji.

Hakikisha wanapoishi hakuna access ya paka, panya na nyoka.

Mengine yote ni myths.
asante kwa darsa. nachokupendea bibi si mchoyo wa ilimu adhimu kama hizi.
 
Kama kuna tukio nyumbani kwako au kwa jirani wa karibu, mfano harusi, msiba au sherehe yoyote wajulishe, wakistukia tu watu nyomi, mziki huo au vilio wanasepa wote. Kuna bibi mmoja aliwafuga wengi na kuwapa taarifa kama kuna tukio nyumbani kwake au kwa majirani, sasa alifiwa na mwanae wa Dar kutokana na uchungu akasahau kuwaambia, siku ya msiba hawakutoka ila siku ya pili alikuta banda tupu. Afu sijui huwa wanaenda wapi maana hupotea tu.
unawapaje taarifa
 
Kuna ya ukweli na ya uwongo mengi pia umejaza. Mimi njiwa nimefuga.
Ukiachana tofauti ya bei ya njiwa huanzia elfu 10 pair moja ya njiwa Wa kawaida, elfu 60 kwa wale weupe, na wengine wapo wanauzwa hadi laki 8 kwa pair moja!

(Kazi moja ya njiwa ni urembo,burudani,kitowewo na baraka)

Kabla ya kufuga njiwa hao ni vyema sasa kutambua masharti yao;
  1. Kwanza kabisa njiwa ukiwanunua kutoka kwa mtu, sharti wawe wawili pair (dume na jike)
  2. Kama muuzaji aliwafuga kwa banda la juu, hakikisha unakowapeleka uwaandalia banda la juu, ukiwaweka banda la chini wanaondoka
  3. Kama banda lako la chini, tafta muuzaji mwenye banda chini ndipo ununue vinginevyo unashauliwa uwanyonyoe manyoya na kuwafungia siku 40 kabla ya kuwafungulia.
  4. Njiwa wakiwa mbele yako usipende kuwajadili, hawapendi masimango wataondoka!
  5. Ukifuga njiwa nao hufatilia nyendo zako, ukiwa mlevi hawakai wanaondoka kwasababu wanaamini mlevi anaweza sahau kuwafungulia bandani siku moja
  6. Njiwa wana nguvu kiimani, hawapendi mfugaji awe mmbeya kugombana na majilani, kwasababu wakati Wa ugomvi njiwa hukaa juu ya paa wakisikiliza halafu huondoka na hawarudi tena
  7. Njiwa hawapendi kuona Umechinja njiwa mwenzao mbele yao, wakiona wanahama wote kwasababu wanahisi utawachinja.
  8. Njiwa hawapendi Makelele ya kushtukiza kama honi Kali, kuwarushia jiwe na miziki mikubwa, ukifanya hivyo wanahama
  9. Njiwa akifa mmoja, huomboleza, unashauliwa umtaftie mwenza haraka kwa njiwa anaebaki la sivyo wanaondoka
  10. Hakikisha njiwa huwachanganyi na kuku mwenye vifaranga, wakipararuliwa huondoka mazima.
  11. Njiwa wanaofugwa banda la uani/nyuma/jikoni huzaliana haraka zaidi kwasababu ya mazingira tulivu
  12. Hakikisha pakashume hawazoei kufika nyumbani kwako! njiwa hawapatani na paka pori la sivyo wanahama wote!
  13. Inasemekana njiwa ni Wa pili kwa wivu baada ya nyegele! Hakikisha unafuga wawiliwawili.
Hayo ni machache tu kati ya masharti ya njiwa!!!
View attachment 1101970
 
Huyu hajafuga mama. Amesimuliwa tu uongo mwingi nae kauleta hapa.
Porojo tupu. Mie nafuga njiwa tena wengi sana, hawa wa kawaida, wana rangi na patterns mbali mbali na wengine ni weupe kabisa. Nilianza na wanne tu baada ya mwaka wakawa zaidi ya 30, sasa hivi wanazidi 300, siwezi kuwahesabu.

Wanaishi juu ya banda kubwa la kuku, walivyo kuwa wanazidi nikawawekea dari za mbao za marine ambazo nimeziongezea coat ya waterproof hardner.

Kitoweo kitamu sana. Siku nikitamani huwa nachinja 20 mpaka 30, Na nimegawa wengi sana na nimeuza wengi sana.

Wao mradi chakula kwa wingi (Mtama, choroko, kundi) na maji safi ya kutosha kwenye mabeseni, wanapenda sana kuoga kwenye maji.

Hakikisha wanapoishi hakuna access ya paka, panya na nyoka.

Mengine yote ni myths.
 
20190522_071836.jpg
 
Mi naombeni njia za kuwatimua tuu,wamehamia kwangu na wamezaliana mnoo,kila siku wanadondosha ceilling board za kuzunguka nyumba,nawatwanga manati ila ndio kama nimewaongezea kasi ya kuzaliana...

Upo wap Mkuu nije kuwachukua.
 
Mi naombeni njia za kuwatimua tuu,wamehamia kwangu na wamezaliana mnoo,kila siku wanadondosha ceilling board za kuzunguka nyumba,nawatwanga manati ila ndio kama nimewaongezea kasi ya kuzaliana...
kamata mmoja chinja mchana mbele yao watasepa
 
1:Kwanza kabisa Njiwa ukiwanunua kwa mtu,sharti wawe wawili pair (dume na jike).

2:Kama muuzaji aliwafuga kwa banda la juu,hakikisha unakowapeleka uwaandalie banda la juu,ukiwaweka banda la chini wanaondoka.

3:Kama banda lako la chini,tafuta muuzaji mwenye banda la chini ndipo ununue vinginevyo unashauliwa uwanyonyoe manyoya na kuwafungia siku 40 kabla ya kuwafungulia.

4:Njiwa wakiwa mbele yako usipende kuwajadili,hawapendi masimango wataondoka!.

5:Ukifuga Njiwa nao hufatilia nyendo zako,ukiwa mlevi hawakai wanaondoka.Vurugu na kelele hawapendi.

6:Njiwa wana nguvu kiimani,hawapendi mfugaji awe Mmbea,kugombana na majirani.Kwa sababu wakatika wa ugomvi Njiwa hukaa juu ya Paa wakisikiliza halafu huondoka na hawarudi tena.

7:Njiwa hawapendi kuona umechinja Njiwa mwenzao mbele yao,wakiona wanahama wote kwa sababu wanahisi utawachinja.

8:Njiwa hawapendi makelele ya kushtukiza kama honi kali,kuwarushia jiwe na miziki mikubwa.Ukifanya hayo wanahama.

9:Njiwa akifa mmoja,huomboleza.Unashauliwa umtafute mwenza haraka kwa Njiwa anaebaki la sivyo wanaondoka/kuondoka.

10:Hakikisha Njiwa huwachanganyi na kuku mwenye vifaranga,wakiparuliwa huondoka mazima.

11:Njiwa wanaofugwa banda la Uani/nyuma/
jikoni huzaliana haraka zaidi kwa sababu ya mazingira tulivu.

12:Hakikisha Pakashume hawazoei kufika nyumbani kwako!.Njiwa hawapatani na Paka pori la sivyo wanahama wote!

13:Inasemekana Njiwa ni wa pili kwa wivu baada ya Nyegere..



Nakumbuka mbali sana nimuonapo njiwa,aliimbwa wakati huo nafaidi muziki,aliimbwa wakati uleee katika igizo la kidedea,kina tabia na jengua.....

Ewe njiwa,ewe njiwa peleka salaaamu.....

Way too far,i waa able to hear.
 
Back
Top Bottom