Yajue mambo manne yanayomaliza sana hela katika haya maisha

hata mimi

JF-Expert Member
Oct 17, 2017
1,352
1,428
Habari...

Kumradhi, ninaandika kwa kifupi sana

Kuna mambo mengi yanayomaliza pesa katika maisha haya ila manne kati yao ni kiboko. Mbaya zaidi ni kwamba mtu hawezi kuyakwepa

1.Ujenzi
Achilia mbali nyumba, Kitasa cha mlango tu elfu sabini! Fikiria kuhusu mlango wenyewe

2.Maradhi
Nadhani wenyewe mashahidi operesheni kwa jk institute ni milioni zake na hela, halafu wanakuwekea na neno tu!

3.Elimu
Waulizeni wanaosomesha; ada ya chuo cha urubani tu ni pension ya mzee halafu mnakuja kushangaa kwanini unesi au ualimu unakuwa na wahitimu wengi (umekuwa kimbilio la wengi) licha ya kuonekana kama sekta dhalili

4.Kesi
Dhamana tu milioni tano, kesi haijaanza kuunguruma hapo. Japo napo panategemea aina ya kesi na kesi/mahakama ila ilimradi tu imeitwa kesi basi ni kisa hasa

Tumwombe MwenyeziMungu huku tukiendelea kujipinda ili tuepukane na madhara ya mambo hayo (mfano kesi na maradhi) na tufaidi mazuri yake (mfano elimu na ujenzi)
 
vinavyomaliza pesa hapo ni viwili tu.

maradhi na kesi.

ujenzi na elimu haviji kama ajali.unajua kabisa ni jukumu linalokuhusu,ndio maana huwezi kudata sababu yake,labda kama umeparamia ukuta mrefu usio size yako.
 
Kuna gharama zinakwepeka kwa kuishi maisha yanayofanana na wewe,mfano ujenzi: umetoa mfano wa kitasa cha sh 70,0000. lakini kuna kitasa cha sh 30,000.kinaweza kudumu hata miaka10 .
hii ni sawa kabisa na kufunga nyumba na kufuli ya elfu 6,ndani kuna tv ya laki 8.

kitasa cha elfu 30 ni kizuri ila labda milango ya ndani huko,nje pale gate kuu lazima ukaze matako,no way.
 
Pesa inamalizika kwenye matumizi yanayojirudia kila siku, hayo uliyoyaandika yanatumika kimazoea tu ili kufarijiana.

1Chakula
2Umeme/Nishati
3Maji
4Mafuta/Usafiri/Nauli
5Kuhonga
6 Vilevi/Pombe/Unga/Casino.
7Mavazi/Malazi
8Watoto
9Wakwe
10Wazazi/Ndugu/ Wategemezi.
 
Pesa inamalizika kwenye matumizi yanayojirudia kila siku, hayo uliyoyaandika yanatumika kimazoea tu ili kufarijiana.

1Chakula
2Umeme/Nishati
3Maji
4Mafuta/Usafiri/Nauli
5Kuhonga
6 Vilevi/Pombe/Unga/Casino.
7Mavazi/Malazi
8Watoto
9Wakwe
10Wazazi/Ndugu/ Wategemezi.
Ujue mambo ya kila siku yanakula hela sawa ila ile ni papo kwa hapo you spend as you earn ila izo ngoma hapo juu ni hela ya mkupuo ambayo huwa ndo inaonekana zaidi (pengo lake)
 
vinavyomaliza pesa hapo ni viwili tu.

maradhi na kesi.

ujenzi na elimu haviji kama ajali.unajua kabisa ni jukumu linalokuhusu,ndio maana huwezi kudata sababu yake,labda kama umeparamia ukuta mrefu usio size yako.
Hata kama haviji kama ajali ila unavifanya huku unavisifu bosi (kwamba vinakufilisi)
 
Habari...

Kumradhi, ninaandika kwa kifupi sana

Kuna mambo mengi yanayomaliza pesa katika maisha haya ila manne kati yao ni kiboko. Mbaya zaidi ni kwamba mtu hawezi kuyakwepa

1.Ujenzi
Achilia mbali nyumba, Kitasa cha mlango tu elfu sabini! Fikiria kuhusu mlango wenyewe

2.Maradhi
Nadhani wenyewe mashahidi operesheni kwa jk institute ni milioni zake na hela, halafu wanakuwekea na neno tu!

3.Elimu
Waulizeni wanaosomesha; ada ya chuo cha urubani tu ni pension ya mzee halafu mnakuja kushangaa kwanini unesi au ualimu unakuwa na wahitimu wengi (umekuwa kimbilio la wengi) licha ya kuonekana kama sekta dhalili

4.Kesi
Dhamana tu milioni tano, kesi haijaanza kuunguruma hapo. Japo napo panategemea aina ya kesi na kesi/mahakama ila ilimradi tu imeitwa kesi basi ni kisa hasa

Tumwombe MwenyeziMungu huku tukiendelea kujipinda ili tuepukane na madhara ya mambo hayo (mfano kesi na maradhi) na tufaidi mazuri yake (mfano elimu na ujenzi)
5. Mapenzi
 
21 Reactions
Reply
Back
Top Bottom