richaabra
JF-Expert Member
- Jul 12, 2016
- 1,454
- 3,469
2. Hayaruhusiwi maongezi ya kawaida, baina ya mwanaume na mwanamke ambaye huna mahusiano naye, maongezi yanayoruhusiwa ni ya kikazi au kimasomo tu.
3. North Korea kuna sheria maalum za jinsi ya unyoaji na kuna hair style sita tu ambazo mwanaume au wanawake wanatakiwa waweke nywele zao, vinginevyo ni makosa.
4. Ni kinyume na sheria kutumia mtandao wa internet bila sababu ya msingi, wanaoruhusiwa ni wale walioruhusiwa na serikali kwa kazi muhimu tu.
5. North Korea ni kinyume cha sheria kuangalia filamu za ponografi, au kuangalia filamu za Korea ya Kusini na zile za nchi za Mangaribi, wanaobainika hupewa adhabu ya kupigwa risasi hadharani hadi kufa.
6. Haruhusiwi mtu yeyote kusikiliza nyimbo tofauti na za taifa, miziki au nyimbo zilizoruhusiwa ni nyimbo za taifa tu.
7. Ni kinyume na sheria kwa mtu yeyote kusafiri nje ya nchi bila sababu maalum, wanaofanya hivyo huonekana kuwa ni wasaliti, na wanaobainika adhabu yao huwa ni kifo.
Mhhh! Wakuu kwa wale tunaosema Tanzania tuna udikteta flani mhhhh ni kweli, lakini kuna madikteta duniani asee!