Yah: Matumizi ya Nembo ya Taifa Halisi (coat of arms) katika hotuba za Rais

Umkonto

JF-Expert Member
Dec 27, 2018
2,099
3,610
Wajuzi hii imekaaje? Kwa sasa Nembo ya Taifa (Coat of Arms), ni kama vile imebadilishwa hasa rangi na kupoteza uhalisia wake.

Ukifuatilia hotuba za rais Samia, nembo hii inakuwa ina rangi kama ya damu ya mzee, au ya mbao hivi, tofauti na uhalisia wake.

Hivyo, waandaji wa hafla za rais jitahidini muwe mnaweka Nembo yenye rangi halisi ya Taifa (Coat of Arms), mbele ya rais kama mtaona inafaa, ili kuendeleza historia ya nchi.

Hapo chini nitabainisha nembo halisi na hii nembo ambayo imechakachuliwa ila inatumika kwenye hotuba za rais kwa sasa.

Kwa wasiofahamu, nembo ya taifa (Coat of Arms), ni nembo rasmi ya serikali. Hii hutumika kama muhuri rasmi wa serikali ya Tanzania.

Nembo hii imebeba ujumbe mbalimbali ndani yake, hivyo kuibadilisha hata rangi tu, basi hupoteza uhalisia wake. Kwa mfano, nembo halisi ya taifa ina mimea miwili ya pamba na karafuu, swali, je hayo mazao yataonekana vipi ikiwa rangi ni damu ya mzee badala ya kijani?

Kwa ufupi, nembo ya taifa halisi imebeba vitu 12 vyenye maana zake, ambavyo vinatakiwa viwe katika rangi halisi kama ifuatavyo, kwa kifupi lakini:-

1. Watu wawili-mwanaume na mwanamke.
-Humaanisha, nchi itajengwa kwa ushirikiano wa wanaume na wanawake.

2. Ngao na Mkuki (Shield and Spear)
-Huwakilisha silaha zilizotumiwa na Watanzania wakati wa kupinga ukoloni.

3. Ufito wa rangi ya dhahabu (Golden band) sehemu ya juu ya ngao.
-Huwakilisha utajiri wa madini yanayopatikana nchini.

4. Moto unaowaka katika mwenge wa uhuru.
-Huwakilisha uhuru na nuru.

5. Bendera ya taifa.
-Huwakilisha Tanzania ni nchi huru.

6. Ufuto mwekundu katika ngao (Red band on the shield).
-Huwakilisha udongo wa rutuba unaopatikana nchini.

7. Shoka na Jembe (Axe and Hoe).
-Huwakilisha vifaa vilivyokuwa vinatumiwa kuiendeleza nchi.

8. Mawimbi ya bahari (Sea waves).
-Huwakilisha vyanzo vya maji vinavyopatikana Tanzania.

9. Kilele cha mlima Kilimanjaro.
-Huwakilisha mlima mrefu Afrika unaopatikana Tanzania.

10. Mazao-Pamba na Karafuu.
-Huwakilisha mazao ya biashara yanayolimwa Tanzania.

11. Maneno "Uhuru na Umoja".
-Huu ni moto/motto (kionjo) wa nchi yetu.

12. Pembe mbili za ndovu.
-Huwakilisha urithi wa nchi yetu katika nyanja ya wanyama.





images-1.jpg
download.jpg
 
Mbona walianza kuibadilisha toka awamu ya 5 au hukuwepo Tanzania?
 
Mke wangu huyo hapo kwenye nembo ya taifa alikuwa pisi kali sana enzi za uhai wake sio hawa wanawake wa miaka hii.
 
Sikuwepo Tanzania. Ila ukosoaji huu hauhusiani na mama kuupinga mwingi.

Binafsi nawashauri waandaa mikutano waliangalie hili la nembo halisi. Ni muhuri wa serikali huo!

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
Jinsi ulivyoiona hiyo nembo huko ulikokua ndivyo unavyoiona hapo ulipo,acha mbwembwe za "sikuepo Tanzania"kwani ulishawah kuiona podium ya rais zero distance ww??
 
Hili lilishazungumziwa hapa miaka kadhaa nyuma,kuna uzi wake.

Kumbe lilishazungumziwa! Sasa wandaaji waanze kutumia nembo halisi kwani vitu vilivyomo vina maana yake

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Wajuzi hii imekaaje? Kwa sasa Nembo ya Taifa (Coat of Arms), ni kama vile imebadilishwa hasa rangi na kupoteza uhalisia wake.

Ukifuatilia hotuba za rais Samia, nembo hii inakuwa ina rangi kama ya damu ya mzee, au ya mbao hivi, tofauti na uhalisia wake.

Hivyo, waandaji wa hafla za rais jitahidini muwe mnaweka Nembo yenye rangi halisi ya Taifa (Coat of Arms), mbele ya rais kama mtaona inafaa, ili kuendeleza historia ya nchi.

Hapo chini nitabainisha nembo halisi na hii nembo ambayo imechakachuliwa ila inatumika kwenye hotuba za rais kwa sasa.

Kwa wasiofahamu, nembo ya taifa (Coat of Arms), ni nembo rasmi ya serikali. Hii hutumika kama muhuri rasmi wa serikali ya Tanzania.

Nembo hii imebeba ujumbe mbalimbali ndani yake, hivyo kuibadilisha hata rangi tu, basi hupoteza uhalisia wake. Kwa mfano, nembo halisi ya taifa ina mimea miwili ya pamba na karafuu, swali, je hayo mazao yataonekana vipi ikiwa rangi ni damu ya mzee badala ya kijani?

Kwa ufupi, nembo ya taifa halisi imebeba vitu 12 vyenye maana zake, ambavyo vinatakiwa viwe katika rangi halisi kama ifuatavyo, kwa kifupi lakini:-

1. Watu wawili-mwanaume na mwanamke.
-Humaanisha, nchi itajengwa kwa ushirikiano wa wanaume na wanawake.

2. Ngao na Mkuki (Shield and Spear)
-Huwakilisha silaha zilizotumiwa na Watanzania wakati wa kupinga ukoloni.

3. Ufito wa rangi ya dhahabu (Golden band) sehemu ya juu ya ngao.
-Huwakilisha utajiri wa madini yanayopatikana nchini.

4. Moto unaowaka katika mwenge wa uhuru.
-Huwakilisha uhuru na nuru.

5. Bendera ya taifa.
-Huwakilisha Tanzania ni nchi huru.

6. Ufuto mwekundu katika ngao (Red band on the shield).
-Huwakilisha udongo wa rutuba unaopatikana nchini.

7. Shoka na Jembe (Axe and Hoe).
-Huwakilisha vifaa vilivyokuwa vinatumiwa kuiendeleza nchi.

8. Mawimbi ya bahari (Sea waves).
-Huwakilisha vyanzo vya maji vinavyopatikana Tanzania.

9. Kilele cha mlima Kilimanjaro.
-Huwakilisha mlima mrefu Afrika unaopatikana Tanzania.

10. Mazao-Pamba na Karafuu.
-Huwakilisha mazao ya biashara yanayolimwa Tanzania.

11. Maneno "Uhuru na Umoja".
-Huu ni moto/motto (kionjo) wa nchi yetu.

12. Pembe mbili za ndovu.
-Huwakilisha urithi wa nchi yetu katika nyanja ya wanyama.





View attachment 2232052View attachment 2232053
Mbali na hilo, TBC1 nao pia wameubadilisha mlio wa ngoma za Mzee Morris wakatoa ule original ambao ulikuwa unatumika kabla ya taarifa ya habari kipindi cha Mwalimu na hata wakati wa Mwinyi. Wameweka mlio wa ngoma zingine tu ambazo mapigo yake yanaendana kama ya zile za Mzee Morris, hadi inati huzuni. TBC wanao mlio original wa ngoma hizo kwenye archive yao, kwa nini wameamua kutumia mlio mwingine? Ni ule wanaoutumia kwenye taarifa y habari ya saa 7 mchana kila siku. Inasikitisha sana
 
Back
Top Bottom