Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Njia pekee ya kutoa matangazo rasmi kwamba mikoa ya Tanzania haina tena watu walioathirika na virusi vya Covid-19 ni kama tumeenda kuwauliza waganga wa kienyeji na wao ndio wakatupa huo uhakika.
Haingii akilini katika karne hii ya 21 kwamba tunajua kwamba mtu anaweza kuwa na virusi vya Covid-19 na asionyeshe dalili zozote za kuumwa, halafu tunasema hakuna wagonjwa wa Covid-19 Tanzania. Imani iliyoonyeshwa katika kuomba Covid-19 iishe isiwe msukumo wa kutangaza rasmi kwamba sasa hatuna tena Covid-19.
Je, tumefanya utafiti gani na kujihakikishia kwamba hatuna wagonjwa? Tumepima watu wangapi na katika maeneo yepi na kuona kwamba karibu 100% ya tuliowapima hawana virusi vya Covid-19 na hivyo ni halali kwetu kutangaza kwamba mikoa na Tanzania kwa ujumla haina wagonjwa wa Covid-19?
NIlishasema humu JF, hebu Ummy Mwalimu ajaribu hapa Dar angalau aende sehemu kama soko la Kariakoo, Manzese, Temeke, Tandale halafu apime watu "randomly" angalau 50 kila siku. Akikuta katika hawa 50 aliowapima 40 hawana Corona virus basi nitamuunga mkono kutangaza kwamba Tanzania hatuna Covid-19.
Suala la Wakenya kupima madereva wa Tanzania na kukuta kwamba labda 40% ya wanaowapima wana Covid-19 tusilichukulie kisiasa na kuanza kuwatukana Wakenya. Tunapaswa tuone ni dalili kwamba kuna kitu hakiko sawa Tanzania. Tunapaswa kuwashukuru Wakenya kwa kutuonyesha hilo na kufuatilia suala la upimaji badala ya kuwalalamikia.
Ni wazi kwamba haya matangazo ya Ummy yanalenga kumfurahisha Magufuli, lakini hayana mshiko wowote wa kisayansi. Na ndio maana tunakata shauri kwamba ili kutoa tangazo kwamba hatuna tena Covid-19 basi lazima itakuwa imepigwa ramli.
Haingii akilini katika karne hii ya 21 kwamba tunajua kwamba mtu anaweza kuwa na virusi vya Covid-19 na asionyeshe dalili zozote za kuumwa, halafu tunasema hakuna wagonjwa wa Covid-19 Tanzania. Imani iliyoonyeshwa katika kuomba Covid-19 iishe isiwe msukumo wa kutangaza rasmi kwamba sasa hatuna tena Covid-19.
Je, tumefanya utafiti gani na kujihakikishia kwamba hatuna wagonjwa? Tumepima watu wangapi na katika maeneo yepi na kuona kwamba karibu 100% ya tuliowapima hawana virusi vya Covid-19 na hivyo ni halali kwetu kutangaza kwamba mikoa na Tanzania kwa ujumla haina wagonjwa wa Covid-19?
NIlishasema humu JF, hebu Ummy Mwalimu ajaribu hapa Dar angalau aende sehemu kama soko la Kariakoo, Manzese, Temeke, Tandale halafu apime watu "randomly" angalau 50 kila siku. Akikuta katika hawa 50 aliowapima 40 hawana Corona virus basi nitamuunga mkono kutangaza kwamba Tanzania hatuna Covid-19.
Suala la Wakenya kupima madereva wa Tanzania na kukuta kwamba labda 40% ya wanaowapima wana Covid-19 tusilichukulie kisiasa na kuanza kuwatukana Wakenya. Tunapaswa tuone ni dalili kwamba kuna kitu hakiko sawa Tanzania. Tunapaswa kuwashukuru Wakenya kwa kutuonyesha hilo na kufuatilia suala la upimaji badala ya kuwalalamikia.
Ni wazi kwamba haya matangazo ya Ummy yanalenga kumfurahisha Magufuli, lakini hayana mshiko wowote wa kisayansi. Na ndio maana tunakata shauri kwamba ili kutoa tangazo kwamba hatuna tena Covid-19 basi lazima itakuwa imepigwa ramli.