Jamani
Huu ukuaji wa bei ya viwanja na nyumba ni kawaida kweli? Yaani nyumba kama hii huko Masaki inauzwa kwa Dola Milioni 2 kweli na hii ilikuwa ni 2023. Huko Kariakoo nimeona kuna jengo linauzwa kwa Bilion 5
View attachment 3595375
Hizo bei ni kama za Palm Beach Florida au kwenye Prime areas za huko Marekani. ambapo miundombinu (barabara, maji, umeme, na usalama) iko katika kiwango cha juu zaidi duniani.
Kulingana na takwimu za
The Africanvestor (2026), bei za ardhi katika maeneo ya biashara zimekuwa zikipanda kwa wastani wa
10% hadi 15% kila mwaka
Mi nadhan muda wa kuanzishwa kwa chombo maalum cha udhibiti, tukiite LARA (Land and Rent Authority), ambacho kitafanya kazi kama LATRA inavyodhibiti usafiri, ili kuleta nidhamu kwenye soko la ardhi na pango nchini Tanzania.
Kazi za Bodi ya LARA (Land and Rent Authority)
Bodi hii itakuwa na majukumu yafuatayo:
- Kupanga bei : Kuweka ukomo wa bei ya chini na ya juu kwa kila eneo (Zoning price regulation) kulingana na huduma zilizopo.
- Udhibiti wa Kodi Kuhakikisha pango la nyumba linaendana na thamani ya jengo na kipato cha eneo hilo, kuzuia wapangaji kunyanyasika.
- Usajili wa Miamala: Kila mauzo ya ardhi lazima yapitie kwenye mfumo wa bodi ili kuzuia ukwepaji kodi na bei za "ujanja ujanja".
- Kusimamia Madalali: Kuhakikisha madalali wamesajiliwa na wanafuata maadili, badala ya kuwa chanzo cha kupandisha bei ili wapate kamisheni kubwa.
View attachment 3595377
5. Mifano ya Nchi Zenye Mifumo Hii
- Ujerumani (Germany): Wana mfumo unaitwa "Mietspiegel" (Rent Index). Serikali inapanga kiwango cha pango ambacho mmiliki haruhusiwi kuzidi kulingana na eneo na ubora wa nyumba.
- Singapore: Serikali inamiliki takriban 90% ya ardhi na inadhibiti bei ili kuhakikisha kila raia anaweza kumudu makazi kupitia bodi yao ya HDB (Housing & Development Board)
- Afrika Kusini: Wana bodi inaitwa Rental Housing Tribunal ambayo inashughulikia migogoro ya pango na kuzuia upandishaji wa kodi usio na tija.