Ya Yanga Afrika na maandalizi Uturuki

Mphamvu

JF-Expert Member
Jan 28, 2011
10,702
3,288
Ni wazo zuri kubadili upepo wakati huu wa maandalizi ya nusu ijayo ya msimu wa ligi.
Lakini nina tatizo kidogo na safari hii... Na kudeclare interest, niko in favor of Simba kwenye derby ya Kariakoo.
Nadhani tumeiga Ulaya ambako huwa wanaenda pre-season nje ya bara lao bila kujua mantiki ya safari zao. Wale huwa wanaenda kufanya utalii pamoja na kuimarisha base zao za biashara, Madrid wanae Ronaldo Maguvu ambae kutua kwake Japan au Korea kutapandisha mauzo ya jezi zao na bidhaa zingine za timu, Manchester United wanao kina Rooney, RvP na wengineo kwa matumizi hayo hayo. Kwao, licha ya kuingia gharama kubwa lakini kuna kitu wanapata in return.
Endapo Yanga wangekuwa wanaenda kwenye game za kimataifa msimu ujao ingeweza kuleta maana kwani wangejenga mazingira ya kucheza na timu za nchi tofauti hasa za Uarabuni ambazo huwa tunapata nazo shida kwenye michuano ya CAF.
Kingine ni pesa, tunajiingiza kwenye matumizi ya sifa yasiyo na msingi ili tu kumkoga mtani. Mpunga wa kusafirisha timu kwenda huko ungeweza kutumika kwenda Mombasa au pengine kwenye unafuu na chenji ikabaki ya kufanyia upembuzi yakinifu wa estadio letu. Pengine Yanga wanafuata training facilitez nzuri, lakini training uwanja mzuri halafu mechi Sokoine na Kaitaba? Wote ni mashuhuda wa jinsi pre-season training yao ya Mwananyamala ilivyowawezesha kukabiliana kwa uzuri na viwanja vya mikoani na kuvuna pointi Mkwakwani, Amri Abeid na Sokoine...
Ni vizuri kwenda nje, lakini ni Good for Nothing.
Inapendeza sana kuwaringishia washabiki wa Simba safari ya Turkey, lakini kwa malengo ya muda mrefu hamna kitu hapo, ni siasa za mpira.
Yanga Imara.
DAIMA MBELE, NYUMA MWIKO!
 
mkuu Mphamvu,kumbuka pia upande wa pili wa safari kama hizo kwa timu zetu!je ni kweli zinakuwa ni kwa manufaa ya timu au mdhamini au kundi la watu fulani wanaotaka kufanikisha malengo yao ya kibiashara?nadhani bado unayo kumbukumbu ya timu ya ngumi iliyoenda kama sikosei shelisheli au visiwa vinavyo karibiana na huko,walikamatwa na madawa!!je madawa yale yalikuwa ni ya nani?je tuna uhakika timu zetu zinapokwenda huko hazitabeba na vitu vingine wakati zikienda au wakati wa kurudi!!huenda hicho ndo kinawapeleka Yanga huko!!all in all kama safari haina ujanja ujanja wanaoufahamu wachache ngoja vijana waongeze CV za safari!!!
ni mtazamo tu jamanai!!
 
mkuu Mphamvu,kumbuka pia upande wa pili wa safari kama hizo kwa timu zetu!je ni kweli zinakuwa ni kwa manufaa ya timu au mdhamini au kundi la watu fulani wanaotaka kufanikisha malengo yao ya kibiashara?nadhani bado unayo kumbukumbu ya timu ya ngumu iliyoenda kama sikosei shelisheli au visiwa vinavyo karibiana na huko,walikamatwa na madawa!!je madawa yale yalikuwa ni ya nani?je tuna uhakika timu zetu zinapokwenda huko hazitabeba na vitu vingine wakati zikienda au wakati wa kurudi!!huenda hicho ndo kinawapeleka Yanga huko!!all in all kama safari haina ujanja ujanja wanaoufahamu wachache ngoja vijana waongeze CV za safari!!!
ni mtazamo tu jamanai!!

acha uzandiki na wivu wewe lafa utakufa na kijiba yanga viongozi wake wote ni mamilionea wenye pesa na makampuni yao wamewekeza kuanzia alhaji bin kleib davies mosha tafuteni njia za kufanya ua mumsahuri huyu mzee wa bastola atafute pesa sio kula hela la rambirambi ya marehemu mafisango leo miezi minne wafanyakazi wa tabora fm hawajalipwa mshahara na sikukuu inakuja mnakalia majungu tu dawa Za kulevya azim dewji ndio aliwabebesha simba kwenda ufaransa 1993 kama unabisha muulize george lucas au fikiri magoso watakuambia
 
Last edited by a moderator:
acha uzandiki na wivu wewe lafa utakufa na kijiba yanga viongozi wake wote ni mamilionea wenye pesa na makampuni yao wamewekeza kuanzia alhaji bin kleib davies mosha tafuteni njia za kufanya ua mumsahuri huyu mzee wa bastola atafute pesa sio kula hela la rambirambi ya marehemu mafisango leo miezi minne wafanyakazi wa tabora fm hawajalipwa mshahara na sikukuu inakuja mnakalia majungu tu dawa Za kulevya azim dewji ndio aliwabebesha simba kwenda ufaransa 1993 kama unabisha muulize george lucas au fikiri magoso watakuambia

Sijapenda hii coment, iko chini ya viwango vya GreatThinker...
 
mkuu Mphamvu,kumbuka pia upande wa pili wa safari kama hizo kwa timu zetu!je ni kweli zinakuwa ni kwa manufaa ya timu au mdhamini au kundi la watu fulani wanaotaka kufanikisha malengo yao ya kibiashara?nadhani bado unayo kumbukumbu ya timu ya ngumu iliyoenda kama sikosei shelisheli au visiwa vinavyo karibiana na huko,walikamatwa na madawa!!je madawa yale yalikuwa ni ya nani?je tuna uhakika timu zetu zinapokwenda huko hazitabeba na vitu vingine wakati zikienda au wakati wa kurudi!!huenda hicho ndo kinawapeleka Yanga huko!!all in all kama safari haina ujanja ujanja wanaoufahamu wachache ngoja vijana waongeze CV za safari!!!
ni mtazamo tu jamanai!!

Kukosekana kwa mantiki ya safari hizi kunaibuwa wasiwasi wa kutokea kwa vitu kama hivi.
Yanga imepata uongozi mpya ambao nadhani umedhamiria kuleta mabadiliko, lakini si kwa kuunda safari kama hizi.
Safari ile inaweza kugharimu Mil. 100 hivi, pesa ambazo wangeweza kupata eneo kwa ajili ya kujenga training centre ya timu na pengine academy.
 
Last edited by a moderator:
mkuu Mphamvu,kumbuka pia upande wa pili wa safari kama hizo kwa timu zetu!je ni kweli zinakuwa ni kwa manufaa ya timu au mdhamini au kundi la watu fulani wanaotaka kufanikisha malengo yao ya kibiashara?nadhani bado unayo kumbukumbu ya timu ya ngumi iliyoenda kama sikosei shelisheli au visiwa vinavyo karibiana na huko,walikamatwa na madawa!!je madawa yale yalikuwa ni ya nani?je tuna uhakika timu zetu zinapokwenda huko hazitabeba na vitu vingine wakati zikienda au wakati wa kurudi!!huenda hicho ndo kinawapeleka Yanga huko!!all in all kama safari haina ujanja ujanja wanaoufahamu wachache ngoja vijana waongeze CV za safari!!!
ni mtazamo tu jamanai!!
haya wazee mbona hamfurahi hii trip ya yanga ,haya basi tunaenda kupeleka na kuleta mzigo fanyeni mnalotaka yanga itapaa.
 
Mbona wenyewe walishasema wanaenda kufanya nini, na wewe unawawekea sababu zako. Wamekwambia uko kuna training facilities bora zaidi kuliko bongo. Pia motisha ni muhimu sana kwa wachezaji wetu, Man U wanasababu zao na Yanga wanazo za kwao ambazo ni za maana kwao. Kumlingishia Simba wapi na wapi, mbona hamuishi nongwa wakati wenyewe wanarekebisha mambo yao na wanachama acheni yanga waboreshe soka lao.
 
Mbona wenyewe walishasema wanaenda kufanya nini, na wewe unawawekea sababu zako. Wamekwambia uko kuna training facilities bora zaidi kuliko bongo. Pia motisha ni muhimu sana kwa wachezaji wetu, Man U wanasababu zao na Yanga wanazo za kwao ambazo ni za maana kwao. Kumlingishia Simba wapi na wapi, mbona hamuishi nongwa wakati wenyewe wanarekebisha mambo yao na wanachama acheni yanga waboreshe soka lao.

Wewe nani hata utuzuie kuwajadili Yanga?
Haya ni maono yangu juu ya safari yao, na sio kwa Yanga tu, hata timu nyingine itakayofanya safari kama hiyo.
Training facilities zinatakiwa ziwe long termed, huwezi kutrain na kulala pazuri mwezi mmoja halafu ukarudi kutrain Kaunda na kulala vile vitanda vya futi 2.5 kwenye jengo la njano, ni ujinga huo.
Next time jaribu kuangalia kila wazo kwa mtazamo neutral...
 
Mi hapa naona kama uongozi wa Yanga umekurupuka tu ili mradi wafurahishe jamii na wapate la kusema kwa watani wao Simba...mi nafikiri yanga wangeanza kutembelea timu kubwa za Afrika kwanza na wajifunze kutoka huko waone wenzao wamefanya nini kuwa hapo walipo Mfano.TP mazembe,Esperance au timu nyingine kubwa tu za Afrika na hi ingesaidia sababu hata miundo mbinu ya kiafrika inafanana sana..mi nafikiri hi ingewasaidia sana yanga kuliko kwenda Uturuki.
 
Hawaendi ziara ya mafunzo. Ni pamoja na wachezaji kuabadili mazingira ili wawe sawa kisaikolojia.
 
Kukosekana kwa mantiki ya safari hizi kunaibuwa wasiwasi wa kutokea kwa vitu kama hivi.
Yanga imepata uongozi mpya ambao nadhani umedhamiria kuleta mabadiliko, lakini si kwa kuunda safari kama hizi.
Safari ile inaweza kugharimu Mil. 100 hivi, pesa ambazo wangeweza kupata eneo kwa ajili ya kujenga training centre ya timu na pengine academy.

Baadaye tutajadili gharama za usajili, kwamba ni kwanini wasingechukua fremu Kariakoo wakakuza mtaji. Halafu tutafika kwenye pesa za kuweka kambi, kwamba kwa nini wachezaji wasitokee majumbani mwao ili Yanga wapate pesa za kununulia mashamba ya mananasi Kiwangwa waongeze pato. Jamani eeh, timu ipo na ligi inaendelea. Mipango ya maendeleo ya klabu haipaswi kuzuia ufanisi wa timu katika ligi. Safari kama hii zina maana kubwa hata kwa saikolojia ya wachezaji. Simba ni lini watakwenda Zanzibar?????
 
waacheni jameni yeboyebo wakatalii .safari moja huanzisha nyingine na yanga ni timu kubwa east africa na wakirudi wanalamba 5+1 bila
 
Back
Top Bottom