Mikono yenye Sugu
Senior Member
- Jul 1, 2020
- 133
- 215
Kitendo cha Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Tarime kutumia lugha isiyo ya staha jukwaani kwa kumuita mgombea wa CHADEMA "mwanamke malaya" ni cha kidhalilishaji na hakipaswi kunyamaziwa pasipo kukemea.
Tupo katika mchakato wa kampeni kwa ajili ya uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu na Tume imekuwa ikisisitiza kila mara wagombea wa vyama vyote kufanya kampeni za kistaarabu pasipo kutumia maneno ya uchochezi na uvunjifu wa amani. Alichokifanya Mwenyekiti huyo ni udhalilishaji dhidi ya mama zetu akiwemo mama yake, dada zake na shangazi zake.
Ni matumaini yangu kuwa CCM, hususan watendaji waandamizi wakiongozwa na Katibu Mkuu Mwl Bashiru, watajitokeza hadharani kukemea kauli hiyo sambamba na kuomba radhi umma wa wanawake wa taifa hili na wapenda amani wote kwa kitendo kilichofanywa na mwenyekiti huyo mwenye nakisi ya maadili.
Nakipenda chama changu, lakini kamwe sitakuwa tayari mapenzi hayo kunifanya nisione yasiyofaa na kuyakemea.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.
Tupo katika mchakato wa kampeni kwa ajili ya uchaguzi mkuu Oktoba mwaka huu na Tume imekuwa ikisisitiza kila mara wagombea wa vyama vyote kufanya kampeni za kistaarabu pasipo kutumia maneno ya uchochezi na uvunjifu wa amani. Alichokifanya Mwenyekiti huyo ni udhalilishaji dhidi ya mama zetu akiwemo mama yake, dada zake na shangazi zake.
Ni matumaini yangu kuwa CCM, hususan watendaji waandamizi wakiongozwa na Katibu Mkuu Mwl Bashiru, watajitokeza hadharani kukemea kauli hiyo sambamba na kuomba radhi umma wa wanawake wa taifa hili na wapenda amani wote kwa kitendo kilichofanywa na mwenyekiti huyo mwenye nakisi ya maadili.
Nakipenda chama changu, lakini kamwe sitakuwa tayari mapenzi hayo kunifanya nisione yasiyofaa na kuyakemea.
MUNGU IBARIKI TANZANIA.