Ya LISSU yafika hapa pia...

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Nov 25, 2010
6,135
17,802
Yale ya watu wasio na uwezo kuongoza Idara za Serikali yanaendelea. Sasa ni Law School of Tanzania. Ni kuhusu matokeo ya wanafunzi kuchakachuliwa. Leo unapewa matokeo haya,kesho yale. Jana,Law School walitoa matokeo ya supplementary kwa wale waliozifanya mwezi wa saba. Yupo rafiki yangu mmoja alikuwa anadaiwa masomo mawili: LS 103(kuhusu kuandaa Nyaraka) linalofundishwa na Prof. Ismail Hamudi Majamba na LS 107(kuhusu Uuzaji wa Ardhi) linalofundishwa na Dr.Ringo Tenga.

Alipoangalia matokeo yake leo,amekuta matokeo yake ya masomo hayo ni mazuri. 'Ameclear'.Lakini ana supplementary mpya. Sasa ni LS 106(kuhusu Sheria za kibiashara). Si habari njema kwake.Hii tena imetoka wapi? Law School ikiwa ni Taasisi ya Mafunzo ya Uwakili inaingia kwenye kashfa nzito.Kashfa ya kuchakachua matokeo ya wanafunzi.

Kwakuwa mimi si mnafiki, angalieni kwenye website ya Law School halafu ingiza nambari LST/2010/07/147 ujionee ninayosema. Huu ni ujinga na us...........mkubwa. Waacheni watu wawe Mawakili. Tuliopo hatutoshi. Acheni ubabaishaji.Wajinga sana nyinyi....chungeni sana
 
pengine hawakai kupitisha matokeo ya supplimentary, ndio maana matatizo kama haya yanatokea,
 
Back
Top Bottom