Ya Kujifunza kwa tukio la Ajali ya watoto Arusha

Baba Wawili 2012

JF-Expert Member
Mar 21, 2012
413
335
Habari wana jamvi.

Nimeguswa sana na kuhuzunika kwa watoto wetu kupoteza maisha kama mshumaa katika upepo.
Poleni wafiwa poleni sani.

Kama mzazi na huwa silalagi ninapokuwa napata taarifa kuwa mwanangu eti wameenda tour za kishule huwa naomba simu ya dereva nanapiga simu kumuasa dereva kuhusu mwendo siku moja kabla ya safari....

Lakin yote na yote kuna haya ambayo yanawezekana kabisa serikali na wamiliki wa shule hasa binafsi kuyafanyia kazi haraka sana:
  • Kama nchi hatuna program maalum kwa ajili ya drivers wa schools bus, au drivers wa makundi maalum. Mf nchi za wenzetu dereva wa gari za shule leseni sio kigezo pekee cha kuwa school driver, anatakiwa kuwa km part ya mwalimu, gurdian, mzazi, uendeshaji, lugha, msaada kwa watoto, .......katika hili mara nyingi wamiliki wa shule wanajiri bora dereva hasa huchukua relatives nyumban, kumpa gari, cheap people, wazee......Tunalipa ada nying sana.. kuna haja serikali kupitia wizara husika, elimu, usafirishaji kuweka miongozo katika hili..N.I.T kuna koz za madereva VIP watu hulipa zaid ya laki 4 kwa miez 3, kwangu mimi VIP ni watoto wetu katika shule tulizowakabidhi wawalee kwa niaba yetu...kuwe na koz maalum kwa ajili madereva wanaondesha gari za wanafunzi......na wazazi na watoto wawe na uwezo wa kuwafanyia evaluation na feedback kupokelewa.
  • Wizara ya elimu na usafirishaji kupitia sumatra, wizara ya mambo ya ndani kupitia trafic, kuweka muongozo kwa wamiliki wa shule kununua gari/school bus zilizo kuwa ni nzima sio third part. kwa uzoef wangu wamiliki wa shule hununua daladala zilizokwisha choka na kupaka rangi za njano na kuonekana mpya.....na hata usalaama barabarani huwa wakiona school bus awakagui....wanaipisha tu....hapa kuwe na utaratibu wa kuwabana wamiliki kununua gari zilizo nzima....na linawezekana....ni miongozo tu ya serikali atakae shindwa abadilishe business,,,,lazima tuwe na taifa lenye kuwa na welfare ya juu kwa watoto wetu. Katika hili hata suala la insurance la magari haya ziwe comprehensive sio third part.
  • sitaki kulaumu kuhusu yaliotokea kabla ya ajali but ni muhimu kutafakari mvua kubwa ilinyesha kabla ya safari..... na mvua ni dalili za hatar kwa usafiir....yaani apakuwa na busara ata kuarisha safari.....hii ni kukkosa muongozo kutoka serikalini
  • Nategemea matamako yenye kutoa miongozo kutoka wizara husika na watoto, elimu, usafirishaji na usalama barabarani kuhusu nini wamiliki wa shule wanapaswa kuchukua taahadhari kwa hali km hii isitokee.....
 
  • Thanks
Reactions: MTK
Back
Top Bottom