babykailama
JF-Expert Member
- Mar 5, 2012
- 251
- 243
Mimi ni mshabiki mzuri sana kazi nzuri za sanaa. Nilimkubali Marehemu Kanumba katika jitijada zake katika kuiendeleza Tasnia ya Filamu za kibongo. Kibinadamu, inasikitisha kwa taa ya kijana kama huyu kutoweka ghafla katika umri wa ujana wake.
Pamoja na hayo, zipo hisia, maneno na matendo yaliyoibuka wakati wa msiba hadi mazishi yake ambayo sikubaliani nayo. Hapa nimeamua kuwashirikisha maana konzo ya maji haifumbatiki kiganjani, itapenya tu! Pamoja na kwamba alikuwa maarufu (Bongo Celeb),
1. Hakukuwa na haja ya Viongozi wengi wa ngazi za juu kuacha shughuli nyingine nyeti za Taifa kwenda msibani, kusaini vitabu na kuhudhuria mazishi. Ni bayana kuwa huyu hakuwa Kiongozi wa Serikali, hata Wawakilishi tu wa hao wakubwa wetu wangeweza kuwawakilisha vyema. Fikiri kuwa Waziri (na Naibu wake) wa habari, Vijana na Michezo wote hawakuonekana kujibu swali husika katika Kikao cha 7 cha Bunge la 10 eti kwa kuwa walikuwa kwenye msiba wa Msanii maarufu! Wapi vipaumbele vyetu kama Taifa.
2. Ilishangaza Waziri kutangaza kutoa mchango wa Tshs.15 M (kwa niaba ya Serikali) na pia (tulisikia) kuwa Serikali iligharimia maziko yake. Ni kigezo gani kimetumika kuamua hivyo na pia kwa uamuzi wa nani aliyeidhinisha matumizi hayo? Ni Bongo Stars wangapi wamefariki bila hata mchango wowote (toka Serikalini) na hata kama tungelinganisha michango yao katika jamii mfano akina Sembuli, Remmy, TX Moshi, Marijani n.k basi hata tungesikia kiwango kama hicho au hata angalau nusu yake. Utashangaa kusikia kuwa mimi babu yangu alifariki na alikuwa Mwenyekiti (mwadilifu) wa CCM (M) na Mjumbe kwenye Jumuiya ya CCM (T) lakini cha ajabu hata hatukuona hata salamu tu za maandishi za rambirambi toka kwa Mwenyekiti wa CCM (T) kwa wafiwa hata Mjane wa babu yetu hajawahi kutembelewa wala kupewa mkono wa pole hata siku moja! Vitendo kama hivi vinatafsirika kuwa ni matumizi zaidi ya hisia (feelings) kuliko taratibu na kanuni zinazotuongoza na huleta manungúniko ambayo hayataisha kwa wengine wengi (nimewataja wachache tu).
3. Inasikitisha Watu wengi (akiwamo Mchungaji Muongoza Mazishi, Mkuu wa Nchi na Waziri wa HVM) tunapotoa Wasifu wa Kanumba, eti "Kijana mwenye TABIA nzuri ya mwenendo wa maisha wa kuigwa katika Jamii" nayo ni sifa yake. Je, hii ni kweli? Kwa vile wakati pumzi ya mtu imekoma huwa hatusemi mabaya basi tungeishia hapo tu katika kumsifia Weledi wake katika kazi ya sanaa ya kuigiza na filamu. Kusema kuwa vijana wengine waige tabia ya mwenendo wa maisha yake ni kuvumbika changa ambayo itawaletea vijana wanaoiga wale mbovu!
Tuwe wakweli na tuwasaidie Wasanii wengi, Wasomi na pia Wanasiasa maarufu hasa katika kipengele cha mienendo ya maisha yao ili waendelee kuishi maisha marefu wakitoa michango yao mbalimbali ya vipawa walivyojaliwa na Mungu.
Nami Mungu anisamehe na muendelee kuniombea maana katika hili nami si mfano wa kuigwa kabisa!
Pamoja na hayo, zipo hisia, maneno na matendo yaliyoibuka wakati wa msiba hadi mazishi yake ambayo sikubaliani nayo. Hapa nimeamua kuwashirikisha maana konzo ya maji haifumbatiki kiganjani, itapenya tu! Pamoja na kwamba alikuwa maarufu (Bongo Celeb),
1. Hakukuwa na haja ya Viongozi wengi wa ngazi za juu kuacha shughuli nyingine nyeti za Taifa kwenda msibani, kusaini vitabu na kuhudhuria mazishi. Ni bayana kuwa huyu hakuwa Kiongozi wa Serikali, hata Wawakilishi tu wa hao wakubwa wetu wangeweza kuwawakilisha vyema. Fikiri kuwa Waziri (na Naibu wake) wa habari, Vijana na Michezo wote hawakuonekana kujibu swali husika katika Kikao cha 7 cha Bunge la 10 eti kwa kuwa walikuwa kwenye msiba wa Msanii maarufu! Wapi vipaumbele vyetu kama Taifa.
2. Ilishangaza Waziri kutangaza kutoa mchango wa Tshs.15 M (kwa niaba ya Serikali) na pia (tulisikia) kuwa Serikali iligharimia maziko yake. Ni kigezo gani kimetumika kuamua hivyo na pia kwa uamuzi wa nani aliyeidhinisha matumizi hayo? Ni Bongo Stars wangapi wamefariki bila hata mchango wowote (toka Serikalini) na hata kama tungelinganisha michango yao katika jamii mfano akina Sembuli, Remmy, TX Moshi, Marijani n.k basi hata tungesikia kiwango kama hicho au hata angalau nusu yake. Utashangaa kusikia kuwa mimi babu yangu alifariki na alikuwa Mwenyekiti (mwadilifu) wa CCM (M) na Mjumbe kwenye Jumuiya ya CCM (T) lakini cha ajabu hata hatukuona hata salamu tu za maandishi za rambirambi toka kwa Mwenyekiti wa CCM (T) kwa wafiwa hata Mjane wa babu yetu hajawahi kutembelewa wala kupewa mkono wa pole hata siku moja! Vitendo kama hivi vinatafsirika kuwa ni matumizi zaidi ya hisia (feelings) kuliko taratibu na kanuni zinazotuongoza na huleta manungúniko ambayo hayataisha kwa wengine wengi (nimewataja wachache tu).
3. Inasikitisha Watu wengi (akiwamo Mchungaji Muongoza Mazishi, Mkuu wa Nchi na Waziri wa HVM) tunapotoa Wasifu wa Kanumba, eti "Kijana mwenye TABIA nzuri ya mwenendo wa maisha wa kuigwa katika Jamii" nayo ni sifa yake. Je, hii ni kweli? Kwa vile wakati pumzi ya mtu imekoma huwa hatusemi mabaya basi tungeishia hapo tu katika kumsifia Weledi wake katika kazi ya sanaa ya kuigiza na filamu. Kusema kuwa vijana wengine waige tabia ya mwenendo wa maisha yake ni kuvumbika changa ambayo itawaletea vijana wanaoiga wale mbovu!
Tuwe wakweli na tuwasaidie Wasanii wengi, Wasomi na pia Wanasiasa maarufu hasa katika kipengele cha mienendo ya maisha yao ili waendelee kuishi maisha marefu wakitoa michango yao mbalimbali ya vipawa walivyojaliwa na Mungu.
Nami Mungu anisamehe na muendelee kuniombea maana katika hili nami si mfano wa kuigwa kabisa!