ntamaholo
JF-Expert Member
- Aug 30, 2011
- 12,904
- 6,904
Mkuu wa mkoa wa Mwanza, mteule wa JK mh. ABASI KANDORO, amefanya kufuru ya mwaka kwa kujiuzia gari la kifalme lililogarimu wavuja jasho zaidi ya milion 300/= ambalo wanaharakati tumekuwa tukiyapigia kelele kwa pesa za kitanzania Tsh. 2,000,000 tu.
Gari hilo ni VX TOYOTA LANDCRUISER, LENYE SPEED MITA 240, namba za usajili STK 3643 lililonunuliwa na mtangulizi wake kwa matummizi ya OFISI YA MKUU WA MKOA wa Mwanza.
Gari hilo lililonuliwa na mkuu wa mkoa kabla ya Kandoro bado ni mpya na hali yake ni nzuri sana, wala halijamaliza hata miaka 10 likitumika.
Baada ya kandoro kufika mwanza, alilikataa kulitumia na kusema kuwa halifai kuwa la mkuu wa mkoa na hivyo alitenga fedha la kununua gari lingine la kifahari zaidi LANDCRUISER V8, BEI MILLION 400/= speed mita 260 ambalo ndilo analolitumia mpaka sasa.
Baada ya kununua gari hilo la kifalme, gari la awali lilipewa namba za serikali STK 3643 na kupaki kwenye ofisi za mkoa na mara chache sana kutumika mkoani.
Ndipo Mh. Abasi kandoro akaunda mbinu za kujiuzia gari hilo alilolikataa kwa madai kwamba halifai kuwa la mkuu wa mkoa, akijiuzia kwa Tsh. 2,000,000/= milion mbili pesa za kitanzania.
Kwa sasa yuko kwemnye hatua za mwisho za kupata kibali, ili aondoe hiyo STK, na kubandika namba za kiraia anze kula maisha na gari hilo la kifahari lililogarimu pesa za walipa kodi karibu au zaid ya 300,000,000/= na kuuzwa kwa bei ya kifisadi 2,000,000 tu.
Nawasilisha tafadhali.
Gari hilo ni VX TOYOTA LANDCRUISER, LENYE SPEED MITA 240, namba za usajili STK 3643 lililonunuliwa na mtangulizi wake kwa matummizi ya OFISI YA MKUU WA MKOA wa Mwanza.
Gari hilo lililonuliwa na mkuu wa mkoa kabla ya Kandoro bado ni mpya na hali yake ni nzuri sana, wala halijamaliza hata miaka 10 likitumika.
Baada ya kandoro kufika mwanza, alilikataa kulitumia na kusema kuwa halifai kuwa la mkuu wa mkoa na hivyo alitenga fedha la kununua gari lingine la kifahari zaidi LANDCRUISER V8, BEI MILLION 400/= speed mita 260 ambalo ndilo analolitumia mpaka sasa.
Baada ya kununua gari hilo la kifalme, gari la awali lilipewa namba za serikali STK 3643 na kupaki kwenye ofisi za mkoa na mara chache sana kutumika mkoani.
Ndipo Mh. Abasi kandoro akaunda mbinu za kujiuzia gari hilo alilolikataa kwa madai kwamba halifai kuwa la mkuu wa mkoa, akijiuzia kwa Tsh. 2,000,000/= milion mbili pesa za kitanzania.
Kwa sasa yuko kwemnye hatua za mwisho za kupata kibali, ili aondoe hiyo STK, na kubandika namba za kiraia anze kula maisha na gari hilo la kifahari lililogarimu pesa za walipa kodi karibu au zaid ya 300,000,000/= na kuuzwa kwa bei ya kifisadi 2,000,000 tu.
Nawasilisha tafadhali.