Ya Kandoro inatisha... Ajiuzia gari la TZS milioni 300 kwa milioni 2 tu!

ntamaholo

JF-Expert Member
Aug 30, 2011
12,904
6,904
Mkuu wa mkoa wa Mwanza, mteule wa JK mh. ABASI KANDORO, amefanya kufuru ya mwaka kwa kujiuzia gari la kifalme lililogarimu wavuja jasho zaidi ya milion 300/= ambalo wanaharakati tumekuwa tukiyapigia kelele kwa pesa za kitanzania Tsh. 2,000,000 tu.

Gari hilo ni VX TOYOTA LANDCRUISER, LENYE SPEED MITA 240, namba za usajili STK 3643 lililonunuliwa na mtangulizi wake kwa matummizi ya OFISI YA MKUU WA MKOA wa Mwanza.

Gari hilo lililonuliwa na mkuu wa mkoa kabla ya Kandoro bado ni mpya na hali yake ni nzuri sana, wala halijamaliza hata miaka 10 likitumika.

Baada ya kandoro kufika mwanza, alilikataa kulitumia na kusema kuwa halifai kuwa la mkuu wa mkoa na hivyo alitenga fedha la kununua gari lingine la kifahari zaidi LANDCRUISER V8, BEI MILLION 400/= speed mita 260 ambalo ndilo analolitumia mpaka sasa.

Baada ya kununua gari hilo la kifalme, gari la awali lilipewa namba za serikali STK 3643 na kupaki kwenye ofisi za mkoa na mara chache sana kutumika mkoani.

Ndipo Mh. Abasi kandoro akaunda mbinu za kujiuzia gari hilo alilolikataa kwa madai kwamba halifai kuwa la mkuu wa mkoa, akijiuzia kwa Tsh. 2,000,000/= milion mbili pesa za kitanzania.

Kwa sasa yuko kwemnye hatua za mwisho za kupata kibali, ili aondoe hiyo STK, na kubandika namba za kiraia anze kula maisha na gari hilo la kifahari lililogarimu pesa za walipa kodi karibu au zaid ya 300,000,000/= na kuuzwa kwa bei ya kifisadi 2,000,000 tu.

Nawasilisha tafadhali.

 
Kama haya uliyoyaandika yana ukweli asante kwa taalifa. Tutampelekea Dk Slaa aongeze idadi ya mafisadi kwenye orodha yake.
 
Kandoro si wa kwanza kufanya hivyo huo ni utaratibu wa kawaida tu kwa viongozi wengi hasa wa serikali kuu na Taasisi mbalimbali kujiuuzia magari ya thamani kubwa kwa bei sawa na bure.

Tena hizo milioni 2 za kandoro ni nyingi sana kuna watu wananunua GX kwa laki tisa (900,000/=) tu, yaani ufisadi ni mkubwa sana serikali kuu na kwenye taasisi za serikali ila chakushangaza watu wanapiga kelele kuwa halmashauri zinaongoza wakati sio kweli, asilimia kubwa ya wizi kwenye halmashauri ni chini ya milioni 10 tu.
 
unashangaa ya mwanza?ccm kila kona mtindo ndio huo ila sasa inakula kwao muda si mrefu,
tusuburi waislam wawanzishie ili na sisi tuzibuke masikio.
 
aliacha 'maumivu' Dar es Salaam ya kufidia kuhamisha wakazi wa Tabata dampo ambapo inasemekana ililipwa Billion 20 (20b) kwenye kiwanja ambacho hata milioni 500' hakifikii. Yaani hakulidhika tu!? ...kweli ukila nyama ya binadamu huwezi acha!
Kandoro si wa kwanza kufanya hivyo huo ni utaratibu wa kawaida tu kwa viongozi wengi hasa wa serikali kuu na Taasisi mbalimbali kujiuuzia magari ya thamani kubwa kwa bei sawa na bure. Tena hizo milioni 2 za kandoro ni nyingi sana kuna watu wananunua GX kwa laki tisa (900,000/=) tu, yaani ufisadi ni mkubwa sana serikali kuu na kwenye taasisi za serikali ila chakushangaza watu wanapiga kelele kuwa halmashauri zinaongoza wakati sio kweli, asilimia kubwa ya wizi kwenye halmashauri ni chini ya milioni 10 tu.
 
Watanzania tupunguze majungu tufanye kazi. Kila taasisi ina kitu kinaitwa "Disposal Policy" kwamba gari likifikisha Kilometer/miaka flani linauzwa linanunuliwa lingine. Wengi hutumia Kilometer 250,000 au miaka mitano. Hata kama gari lilinunuliwa kwa 300 million baada ya kutumika miaka mitano thamani yake haitabaki kuwa 300 milion tena kutokana na uchakavu ambao utakuwa umekadiriwa kuwa 60 million kwa mwaka kama Policy yao ni miaka mitano.

Ila kwa swala la kuuzwa 2 million, kama ndio bei iliyopatikana kwa ushindani "Tender process" bado mtu hawezi kuhoji. Ila kabla ya kutangaza tender ilitakiwa gari hili lifanyie "valuation" kujua market value na hivyo lisingeweza kuuzwa chini ya "market value
 
Wakuu, unajua mimi mpaka kesho huwa sielewi Toyota kuuzwa milioni sijui 300 au 400, Toyota haimo kabisa kwenye hiyo ligi. can someone pls explain to me??????

Mkuu hiyo ni bei maalum kwa serikali ya Tanzania, hujui kuwa watanzania ni mamilionea hivyo hata bei zetu huwa ni special teh teh teh teh!

Hiyo ndio bongo mkuu!
 
Wakuu, unajua mimi mpaka kesho huwa sielewi Toyota kuuzwa milioni sijui 300 au 400, Toyota haimo kabisa kwenye hiyo ligi. can someone pls explain to me??????

Hata mimi huwa nashangaa pengine ni ufisadi tu kati ya watumishi wa serikali na Toyota Tanzania
 
Mkuu hiyo ni bei maalum kwa serikali ya Tanzania, hujui kuwa watanzania ni mamilionea hivyo hata bei zetu huwa ni special teh teh teh teh!

Hiyo ndio bongo mkuu!

Nadhani itakuwa hivyo maana hizo ni bei za magari ya kiitaliano!!!!!!!!!
 
Watanzania tupunguze majungu tufanye kazi. Kila taasisi ina kitu kinaitwa "Disposal Policy" kwamba gari likifikisha Kilometer/miaka flani linauzwa linanunuliwa lingine. Wengi hutumia Kilometer 250,000 au miaka mitano. Hata kama gari lilinunuliwa kwa 300 million baada ya kutumika miaka mitano thamani yake haitabaki kuwa 300 milion tena kutokana na uchakavu ambao utakuwa umekadiriwa kuwa 60 million kwa mwaka kama Policy yao ni miaka mitano.

Ila kwa swala la kuuzwa 2 million, kama ndio bei iliyopatikana kwa ushindani "Tender process" bado mtu hawezi kuhoji. Ila kabla ya kutangaza tender ilitakiwa gari hili lifanyie "valuation" kujua market value na hivyo lisingeweza kuuzwa chini ya "market value
Hizi sayansi zenu za uhasibu ndio zinatufanya mtuibie pesa zetu........eti gari zima bado linatembea na linang'aa mnatuaniambia lina zero value kisa sijui wenyewe mnaita "depreciation", cha kushangaza mtu akishalinunua hilo gari utakuta anakaa nalo hadi miaka 15 au zaidi, sasa hiyo depreciation ni kwa serikali tu, kwa watu binafsi hai-apply?

Nyie wasomi ndio mnatuharibia nchi. Mwizi ni mwizi tu, hata ukiiba kwa kalamu wewe ni mwizi tu!
 
Nazidi kuamini ccm hakuna msafi hata kidogo na chakushangaza wanaendelea wakidhani bado watz wa mwaka jana ni sawa na waleo iko siku kwani mwosha huoshwa
 
20 Reactions
Reply
Back
Top Bottom