WPFD 2022: Maadhimisho yaanza rasmi Nchini Tanzania. Ripoti ya Dunia yaonesha Uhuru wa Habari unazidi kuporomoka

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Apr 18, 2017
2,807
11,969
47a3f203-233f-4f29-995c-09348b019be0.jpg


Kuelekea Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari (Mei 03, 2022), Maadhimisho hapa Nchini yameanza rasmi leo Mei 01, 2022 Jijini Arusha

Kaulimbiu ya Siku hii kwa Mwaka 2022 inasema "Uandishi wa Habari na Changamoto za Kidijiti"

Msemaji Mkuu wa Serikali, Gerson Msigwa amesema changamoto zipo katika Tasnia ya Habari, na ni muhimu kutafuta suluhu ili kusonga mbele. Ameeleza kuwa, Serikali ipo tayari kushirikiana na Wadau wa Habari

Akizungumza leo katika uzinduzi wa Maadhimisho ya Siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari, ametoa rai kwa Wanahabari kuendelea kutimiza wajibu wa licha ya mazingira kuwa na changamoto kadhaa

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania (TEF), Deodatus Balile amesisitiza Serikali inatakiwa kuwa tayari kushirikiana na Wadau wa Tasnia ya Habari

1651392599687.png


1651392575641.png


HALI ILIVYO DUNIANI

World Trends in Freedom of Expression and Media Development: Global Report 2021/22 (UNESCO)


Katika miaka mitano iliyopita, maombi ya Serikali kutaka maudhui yaondolewe kwenye majukwaa makubwa mtandaoni yameongezeka maradufu

Kati ya Mwaka 2016 hadi mwishoni mwa Mwaka 2021, Waandishi wa Habari 455 waliuawa wakiwa kazini au kutokana na kazi zao

Aidha, 85% ya Idadi ya Watu duniani kote walipitia hali ya kuzorota kwa Uhuru wa Vyombo vya Habari katika miaka mitano iliyopita

B3D8F051-7EF5-4869-BCAD-10132EB0C372.jpeg


89E981D8-119D-4005-8F25-E2CFEA0DB430.jpeg


5B45F5C8-1864-4629-9D80-76216894D06A.jpeg


MAXENCE MELO: DIJITALI INACHOCHEA MAMLAKA KUCHUKUA HATUA MAPEMA

Mkurugenzi Mtendaji wa Jamii Forums, Maxence Melo anasema Dijitali imetoa fursa kwa Maudhui ambayo huenda yasingekuwa rahisi kuruhusiwa na Mhariri au Chombo cha Habari

Ameeleza, "Katika safari hii ya Dijitali najua kuna uoga wa mabadiliko. Changamoto kubwa ninayoona ni dijitali imekuwa ikidhibitiwa kisiasa"

HAKI YA FARAGHA INALINDA UTU WA WATU

Mkurugenzi Mtendaji wa JamiiForums amesema katika dunia ambayo Nchi haiweki Sheria ya Faragha, utu wa watu wake unaweza kuwa matatani

Ameeleza, "Utu wako katika ulimwengu wa kidijiti ni wa kupigania kwa nguvu zote. JamiiForums kwa kushirikiana na Wadau mbalimbali tunaendesha mafunzo ya usalama wa kidijiti. Tunaahidi kufanya mafunzo haya kwa Waandishi wa Habari"

624ED68A-E63F-4AC8-8D8E-4E71FC779975.jpeg


C03AF0BA-AD01-498D-AAF8-D309297578AB.jpeg


81B67244-DE04-46B6-B980-9A0A144FF91C.jpeg
 
Back
Top Bottom