Eiyer
JF-Expert Member
- Apr 17, 2011
- 28,258
- 20,709
Imekuwa ni kawaida sana kwa pande mbili hizi zinazoshutumiana lakini at the same time zikihitajiana sana. . . . . . . . . . . . . . . . . . , . . . Wanawake na Wanaume,yakimfika mwanaume atalaumu wanawake sana,na yakimfika mwanamke naye atafanya hivyo pia.Ukitembea barabarani huwezi kumkuta ambae hajatendwa,na pengine huenda kama atakua na kaumri kakubwa kama Kaunga gfsonwin au Asprin na Dark City na hata mimi (maana ka umri kameenda kidogo ebo!)wanaweza kukuambia wametendwa mara milioni kidogo.Mwanaume anamshutumu mwanamke,nae mwanamke anafanya hivyo pia. . . . . . . . , . . . . . . . . . . . .
Nimefikiri sana nimejiuliza nani mkosaji au mwenye makosa?Nikapata jibu wote ni wakosaji,na kibaya zaidi kila upande hauko tayari kukubali ukweli.Ni kurushiana mawe ya lawama. . . Ukiona thread yenye kichwa kimeandikwa "wanaume mtatuua" humo mtakuta wanawake wanawalaumu sana wanaume.Tena ukikuta nyingine imeandikwa "wanawake ni wa hovyo" humo utakuta wanaume wanawavurumishia mawe ya lawama wanawake.
Jamani mpaka lini? Jambo hili halitusaidii wala halitujengi.Kwanza kila upande unamhitaji mwingine,huo ni ukweli,tuweke silaha chini tujigeuzie kioo tujiangalie bila woga,wanaume tusemezane,wanawake nao vivyo hivyo,kisha tuache tofauti zetu. . .Tukubaliane kwamba bila kuambiana ukweli hatutajua upande upi unahitaji nini kutoka upande wa pili mpaka Yesu atarudi. Mfano,mpaka leo na umri wangu huu(zaidi ya miaka 32)sijui wanawake wanahitaji nini,na sio mimi tuko wengi,je tuendeleze lawama?
Tukubali wote tuna makosa tukae chini tuyamalize!
Nimefikiri sana nimejiuliza nani mkosaji au mwenye makosa?Nikapata jibu wote ni wakosaji,na kibaya zaidi kila upande hauko tayari kukubali ukweli.Ni kurushiana mawe ya lawama. . . Ukiona thread yenye kichwa kimeandikwa "wanaume mtatuua" humo mtakuta wanawake wanawalaumu sana wanaume.Tena ukikuta nyingine imeandikwa "wanawake ni wa hovyo" humo utakuta wanaume wanawavurumishia mawe ya lawama wanawake.
Jamani mpaka lini? Jambo hili halitusaidii wala halitujengi.Kwanza kila upande unamhitaji mwingine,huo ni ukweli,tuweke silaha chini tujigeuzie kioo tujiangalie bila woga,wanaume tusemezane,wanawake nao vivyo hivyo,kisha tuache tofauti zetu. . .Tukubaliane kwamba bila kuambiana ukweli hatutajua upande upi unahitaji nini kutoka upande wa pili mpaka Yesu atarudi. Mfano,mpaka leo na umri wangu huu(zaidi ya miaka 32)sijui wanawake wanahitaji nini,na sio mimi tuko wengi,je tuendeleze lawama?
Tukubali wote tuna makosa tukae chini tuyamalize!