wote tusome hii.

Edson

JF-Expert Member
Mar 7, 2009
9,846
5,076
habari za siku ndugu zangu

napenda kushea pamoja nanyi japo kwa ufupi juu ya mazungumzo niliyofanya mimi na baba yangu alipokuja kunitembela huku nilipo pamoja na kuhudhuria sherehe za ubazo wa mjuu wake.
nilimuuliza baba juu ya mambo mbalimbali kuhusu taifa langu Tanazania na wapi linaelekea.


Edson: baba, vipi huko nyumbani kwa ujumla kuna jipya? i meana mabadiliko yoyote ya kiuchumi?

baba: kwa ujumla nyumbani hatujambo na wote wanakusalimia sana na kuhusu nchi, amani ipo ila utulivu ndo umenza kutoweka taratibu.

edson : kwa nini baba una maana gani kusema hivyo?

baba: ninaposema utulivu umeanza kuondoka ni hiv edson, kwa sasa hali ya maisha ni ngumu sana, kila kitu kimepanda bei mara dufu, yale walioahidiwa hawayaoni na mda unazidi kwenda na kikubwa kinachotia hasira ni kwamba hakuna mikakati madhubuti ya kuonyesha kuna njia mbadala inayofanyika ili walau makali ya maisha yapungue, wao huko serikalini tunasikia kuna baadhi yao wana kesi za kufuja mali ya umma lakini ndo hivyo hukumu bado.watu wamenza kukata tamaa sana na siku hizi kuvumiliana hakupo.

edson: duh! kipindi kile natoka huko niliacha sakata la richmond, vip baba akina edward walifikishwa mahakamani?

baba: edward yup? lowassa au hosea?

Edson; wote wawili.

baba: wote wapo mtaani, hiv unadhani lowassa anaweza kufikishwa mahakamani?! au huyu hosea? thubutu

edson : kwa nini baba

baba: huyu hosea waliunda sijui tume mara wakafikishwa kwa waziri mkuu, pinda akasema atatoa maamuz lakini mapaka leo ni kimya, mimi sijasiki kitu labada kama wametangaza leo iwapo wamechukuliwa hatua yoyote.

Edson: hapa majuzi nilisikia kupia mtandao, hasa jamii forum, kuwa kuna madhara yatokanayo na migodi uko musoma, watu wanadhurika sana ngozi, eti baba serikali yetu inasemaje, na hvi haya madini siku hizi vip tunafaidika nayo au ndo hakuna kabisa?

baba:jamii forum ndio nin?

edson:jamii forum ni forum inayojumuisha watu makini na wa rika tofaut kupita mtandao ambapo watu wanatoa mada na kuzijadili kwa uwazi zaid,na hapo ndipo huwa napata taarifa nying i sana juu ya matukio ya huko nyumbani

baba: unajua mwanangu, tanzania sio maskini. we are not poor by accident; we are poor by choice.nchi yetu ina kila kitu, yaani kila kitu kipo sasa hiv wanatafuta mafuta, inasemekana yapo, sisi tumekuwa kama wawindaji, unajua nini edy;

edson:ndio baba

baba. muwindaji siku zote yeye, ana tabia moja, akienda kuwinda anaweza kushinda porini siku nzima anakimbiza swala,na akirudi nyumbani jioni anarudi na swala mmoja tu.lakini kumbuka ameshinda siku nzima porin.

edson: ehe

baba: na kikubwa zaidi au tatizo kubwa zaidi au kibaya zaidi kwa lugha nyingine ni kwamba anaua kile alichopata, anakula na kesho asubuhi huyo anarud porini kuwinda.ndivyo tanzania ilivyo.

eedson: sijakuelewa baba hapo

baba; hujaelewa nini, yaani kuja kwako huku ulaya na kusoma kote huku bado hujaelewa nilichokisema!!?

edson: kweli baba, maneno magumu hayo;

baba:sikiliza nikwambie edy, kuna watu wanazaliwa tumbo moja baba mmoja na mama mmoja, wanalelewa na wazazi wao mpaka wanakuwa watu wazima lakini baadae katika maisha unakuta mmoja wao ana mwisho mbaya sana, maisha magumu nk.

edson: yaan sasa hapo baba umenipoteza kabisa!

baba: ni hiv, sisi siku zote tumekuwa kama wawindaji, kila tunachokipata tunakiua,na ndio maana hatuendelei kabisa, madini yapo ya kila aina lakini hali za kiuchumu za watu ni duni sana.tumeuza na kuwapa wazungu hawa kila kitu faida ni kdogo na hata wakati mwingine hatuioni kabisa. viongozi wapo lakini porojo nyingi. kuna nchi ngapi tumepata uhuru pamoja, lakini wenzetu wako mbali.raisi mzima anatoka na ujumbe wa watu zaidi ya100 kuja huku ulaya namarekani eti kutafuta misaada na kujifunza toka huku. huu ni uppuzi wa hali ya juu sana. kuna nchi kana rwanda na burundi wale majuzi hapa wamepigana sana, wamemalizana kama kuku lakini nenda pale leo uone nchi inavyopiga hatua, kwa nini wasiende rwanda kujifunza?!

edson: yahh ni kweli baba, sasa wewe unafikiri tatizo liko wapio kwa nchi yetu:
baba: kwanza viongozi,kuanzia raisi hadi hawa wa chini huku hawana dira wapo tu bora liende, mimi nawanbia wanangu kama elimu zenu hizi mnazopata hamtazitumia kwa makini mtakufa nafanya kazi za watu.unaajiliwa tuuuuu mpaka mwisho. serikali imekosamwelekeo afadhali na kipindi kile cha nyuma, siku hizi wziri mwizi,mwnasheria mkuu anakula rushwa, jaji yaani wote.

edson: sasa baba nini kifanyike ili tuondokane na khali kama hii

baba: hv kwanza nikuulize, kwa nini umeamua kuoa huku na si nyumbani?

edson: baba tutaliongea hilo wakati mwingine lakini kwa kifupi ni uamzi tu nimefanya

baba: anyaway sawa lakini uwe makini sana, hawa watoto wapajue uliokotoka sio wakae huku na kwa nini umemwita jina hili (blanca) na si jina la mama yako kama ilivyo desturi yetu?

edson: ni jina tu baba nimemwita mwenyewe wala sikusukumwa na mtu. naomba turudi kwenye mada yetu

baba : sawa, sasa sikia kuhusu hili kwanza inabidi viongozi wache njaa, unajua ukiwa na njaa mambo mawili au matatu lazima uyapate:

edson : yapi hayo baba?

baba: kwanza utafanya maamuzi ambayo si sahihi, yaani ukiwa na njaa some one can buy you very cheap!!!. na mara nyingi mikataba mibovu ya nchii yetu iko hivyo, unakuta waziri ana njaa yake, anataka rushwa, mara mwingine afutie kodi makampuni mengine ili mradi tu amepata chake nk; raisi mwenye hatoi hotuba za kuwafanya watanzania wajitegemee kifikra zaidi. yeye akiongea sana sana utamsikia anasema '' nchi yetu bila wahisani hatuwezi kuendelea kwa hiyo safariza nje ni muhimu sana'' yaan anaongea ongea tu.lazima tujifunze kutunza kile kidogo tulicho nacho tukizalishe ili kitusaidie, muwinda mwenye akili ni yule anayewinda na anapopata anakitunza, anakizalisha ili kimsaidie kesho asikimbie tena porini kwenda kuwinda. vinginevyo tutakuwa omba omba kila siku.

edson: nafikri hiyo itasaidia kidogo na pengine watu wakitumia elimu zao vizuri, kwa manufaa ya umma na kwa taifa kwa ujumla.

baba: masomo unamaliza lini na unategemea kurudi lini nyumbani au tayari umeomba uraia huku ( huku akicheka)

edson: masomo mwaka kesho, na nitarudi tu ila namsubiri kwana huyu( mama blanca) naye amalize wakati huo mimi nitakuwa naendela na kazi.sijaomba uraia baba.

baba; sawa na sasa mahali inakwaje?

Edson: sijatoa, kwa kuwa uko huko tutaangalia uwezekano maana wazaz wote wa pande mbili mpo huku

baba: najisikia kuchoka sana,
edson: unaweza kwenda kuonga maana pilika za sherehe zilikuwa sio mchezo.
 
Mkuu hongera sana inaonesha huwa una document mazungumzo na baba yako, ngoja na mimi nikiwa naongea na kikongwe changu niwe nadocument kinaweza kikawa kina tema ma points tupo kama baba ya edson
 
dada jocyline sikia, laptop yangu ina uwezo wa kurecord na wakati huo inaandika kile inachorecord! new version ya toshiba, ni swala la kuset tu, hasa ukizingatia mimi ni mtaalam wa computer.

copy that!
 
So touchy jinsi unavyoelewana na baba yako amini kuna wengine wako buzy kucitafuta faranga kiasi cha kutokuwa na muda mrefu wa mazungumzo. Wao hao wangeishia tu baba karibu sana hawajambo huko? . Sawa natoka naenda kibaruani (kumbe anakwenda clubbing!
 
habari za siku ndugu zangu

napenda kushea pamoja nanyi japo kwa ufupi juu ya mazungumzo niliyofanya mimi na baba yangu alipokuja kunitembela huku nilipo pamoja na kuhudhuria sherehe za ubazo wa mjuu wake.
nilimuuliza baba juu ya mambo mbalimbali kuhusu taifa langu Tanazania na wapi linaelekea.


Edson: baba, vipi huko nyumbani kwa ujumla kuna jipya? i meana mabadiliko yoyote ya kiuchumi?

baba: kwa ujumla nyumbani hatujambo na wote wanakusalimia sana na kuhusu nchi, amani ipo ila utulivu ndo umenza kutoweka taratibu.

edson : kwa nini baba una maana gani kusema hivyo?

baba: ninaposema utulivu umeanza kuondoka ni hiv edson, kwa sasa hali ya maisha ni ngumu sana, kila kitu kimepanda bei mara dufu, yale walioahidiwa hawayaoni na mda unazidi kwenda na kikubwa kinachotia hasira ni kwamba hakuna mikakati madhubuti ya kuonyesha kuna njia mbadala inayofanyika ili walau makali ya maisha yapungue, wao huko serikalini tunasikia kuna baadhi yao wana kesi za kufuja mali ya umma lakini ndo hivyo hukumu bado.watu wamenza kukata tamaa sana na siku hizi kuvumiliana hakupo.

edson: duh! kipindi kile natoka huko niliacha sakata la richmond, vip baba akina edward walifikishwa mahakamani?

baba: edward yup? lowassa au hosea?

Edson; wote wawili.

baba: wote wapo mtaani, hiv unadhani lowassa anaweza kufikishwa mahakamani?! au huyu hosea? thubutu

edson : kwa nini baba

baba: huyu hosea waliunda sijui tume mara wakafikishwa kwa waziri mkuu, pinda akasema atatoa maamuz lakini mapaka leo ni kimya, mimi sijasiki kitu labada kama wametangaza leo iwapo wamechukuliwa hatua yoyote.

Edson: hapa majuzi nilisikia kupia mtandao, hasa jamii forum, kuwa kuna madhara yatokanayo na migodi uko musoma, watu wanadhurika sana ngozi, eti baba serikali yetu inasemaje, na hvi haya madini siku hizi vip tunafaidika nayo au ndo hakuna kabisa?

baba:jamii forum ndio nin?

edson:jamii forum ni forum inayojumuisha watu makini na wa rika tofaut kupita mtandao ambapo watu wanatoa mada na kuzijadili kwa uwazi zaid,na hapo ndipo huwa napata taarifa nying i sana juu ya matukio ya huko nyumbani

baba: unajua mwanangu, tanzania sio maskini. we are not poor by accident; we are poor by choice.nchi yetu ina kila kitu, yaani kila kitu kipo sasa hiv wanatafuta mafuta, inasemekana yapo, sisi tumekuwa kama wawindaji, unajua nini edy;

edson:ndio baba

baba. muwindaji siku zote yeye, ana tabia moja, akienda kuwinda anaweza kushinda porini siku nzima anakimbiza swala,na akirudi nyumbani jioni anarudi na swala mmoja tu.lakini kumbuka ameshinda siku nzima porin.

edson: ehe

baba: na kikubwa zaidi au tatizo kubwa zaidi au kibaya zaidi kwa lugha nyingine ni kwamba anaua kile alichopata, anakula na kesho asubuhi huyo anarud porini kuwinda.ndivyo tanzania ilivyo.

eedson: sijakuelewa baba hapo

baba; hujaelewa nini, yaani kuja kwako huku ulaya na kusoma kote huku bado hujaelewa nilichokisema!!?

edson: kweli baba, maneno magumu hayo;

baba:sikiliza nikwambie edy, kuna watu wanazaliwa tumbo moja baba mmoja na mama mmoja, wanalelewa na wazazi wao mpaka wanakuwa watu wazima lakini baadae katika maisha unakuta mmoja wao ana mwisho mbaya sana, maisha magumu nk.

edson: yaan sasa hapo baba umenipoteza kabisa!

baba: ni hiv, sisi siku zote tumekuwa kama wawindaji, kila tunachokipata tunakiua,na ndio maana hatuendelei kabisa, madini yapo ya kila aina lakini hali za kiuchumu za watu ni duni sana.tumeuza na kuwapa wazungu hawa kila kitu faida ni kdogo na hata wakati mwingine hatuioni kabisa. viongozi wapo lakini porojo nyingi. kuna nchi ngapi tumepata uhuru pamoja, lakini wenzetu wako mbali.raisi mzima anatoka na ujumbe wa watu zaidi ya100 kuja huku ulaya namarekani eti kutafuta misaada na kujifunza toka huku. huu ni uppuzi wa hali ya juu sana. kuna nchi kana rwanda na burundi wale majuzi hapa wamepigana sana, wamemalizana kama kuku lakini nenda pale leo uone nchi inavyopiga hatua, kwa nini wasiende rwanda kujifunza?!

edson: yahh ni kweli baba, sasa wewe unafikiri tatizo liko wapio kwa nchi yetu:
baba: kwanza viongozi,kuanzia raisi hadi hawa wa chini huku hawana dira wapo tu bora liende, mimi nawanbia wanangu kama elimu zenu hizi mnazopata hamtazitumia kwa makini mtakufa nafanya kazi za watu.unaajiliwa tuuuuu mpaka mwisho. serikali imekosamwelekeo afadhali na kipindi kile cha nyuma, siku hizi wziri mwizi,mwnasheria mkuu anakula rushwa, jaji yaani wote.

edson: sasa baba nini kifanyike ili tuondokane na khali kama hii

baba: hv kwanza nikuulize, kwa nini umeamua kuoa huku na si nyumbani?

edson: baba tutaliongea hilo wakati mwingine lakini kwa kifupi ni uamzi tu nimefanya

baba: anyaway sawa lakini uwe makini sana, hawa watoto wapajue uliokotoka sio wakae huku na kwa nini umemwita jina hili (blanca) na si jina la mama yako kama ilivyo desturi yetu?

edson: ni jina tu baba nimemwita mwenyewe wala sikusukumwa na mtu. naomba turudi kwenye mada yetu

baba : sawa, sasa sikia kuhusu hili kwanza inabidi viongozi wache njaa, unajua ukiwa na njaa mambo mawili au matatu lazima uyapate:

edson : yapi hayo baba?

baba: kwanza utafanya maamuzi ambayo si sahihi, yaani ukiwa na njaa some one can buy you very cheap!!!. na mara nyingi mikataba mibovu ya nchii yetu iko hivyo, unakuta waziri ana njaa yake, anataka rushwa, mara mwingine afutie kodi makampuni mengine ili mradi tu amepata chake nk; raisi mwenye hatoi hotuba za kuwafanya watanzania wajitegemee kifikra zaidi. yeye akiongea sana sana utamsikia anasema '' nchi yetu bila wahisani hatuwezi kuendelea kwa hiyo safariza nje ni muhimu sana'' yaan anaongea ongea tu.lazima tujifunze kutunza kile kidogo tulicho nacho tukizalishe ili kitusaidie, muwinda mwenye akili ni yule anayewinda na anapopata anakitunza, anakizalisha ili kimsaidie kesho asikimbie tena porini kwenda kuwinda. vinginevyo tutakuwa omba omba kila siku.

edson: nafikri hiyo itasaidia kidogo na pengine watu wakitumia elimu zao vizuri, kwa manufaa ya umma na kwa taifa kwa ujumla.

baba: masomo unamaliza lini na unategemea kurudi lini nyumbani au tayari umeomba uraia huku ( huku akicheka)

edson: masomo mwaka kesho, na nitarudi tu ila namsubiri kwana huyu( mama blanca) naye amalize wakati huo mimi nitakuwa naendela na kazi.sijaomba uraia baba.

baba; sawa na sasa mahali inakwaje?

Edson: sijatoa, kwa kuwa uko huko tutaangalia uwezekano maana wazaz wote wa pande mbili mpo huku

baba: najisikia kuchoka sana,
edson: unaweza kwenda kuonga maana pilika za sherehe zilikuwa sio mchezo.


Jamani mnasikia??! Karekodi /kadocument, sio issue kikubwa ni kwamba nyie watu mnaosomeshwa huko majuu mnakaa huko uko kikubwa mnachungulia JF na kukoroma kidogo na kurudi kwenye raha zenu. Mnauliza nchi yenu inaendaje, bila ya nyinyi kurudi kama kina Nyerere walivyorudi huku na kumtoa mkoloni ndo hivyo sie wazazi wenu tunaibiwa kura, tunanyang'anywa ardhi, migodi inachukuliwa ili mradi kwani wasomi ni wachache wengi ndo mmebaki huko au mnaenda Nairobi, Botswana, Namibia, swazi, SA nk kujenga nchi za watu. TUBADILIKE!
 
dada jocyline sikia, laptop yangu ina uwezo wa kurecord na wakati huo inaandika kile inachorecord! new version ya toshiba, ni swala la kuset tu, hasa ukizingatia mimi ni mtaalam wa computer.

copy that!

kuna fiks hapo mkuu. naziona laivu. huwezi ukazungumza formally hivyo na baba yako
 
Kwanza Hongera sana ndugu mmegusa mengi sana. Ingefaa kama hii convrsation ungeitupa kwenye one of these news paper. So natural. Safi sana.

Jamani mnasikia??! Karekodi /kadocument, sio issue kikubwa!
Kweli si issue ya kuzingatia. Lets deal with the content.

ni kwamba nyie watu mnaosomeshwa huko majuu mnakaa huko uko kikubwa mnachungulia JF na kukoroma kidogo na kurudi kwenye raha zenu. Mnauliza nchi yenu inaendaje, bila ya nyinyi kurudi kama kina Nyerere walivyorudi huku na kumtoa mkoloni ndo hivyo sie wazazi wenu tunaibiwa kura, tunanyang'anywa ardhi, migodi inachukuliwa ili mradi kwani wasomi ni wachache wengi ndo mmebaki huko au mnaenda Nairobi, Botswana, Namibia, swazi, SA nk kujenga nchi za watu. TUBADILIKE.

Hapo ndo tunatofautiana ndugu. Kwanini mtu arudi huku tz. Arudi ili apoteze ramani zote au? Mimi simshauri mtu arudi bongo, ataishia kuwa frustrated and so. Fanyeni kazi huko huko mkipata kitu tumeni nyumbani kwa ajili ya kuwekeza ukirudi hamna utakachoweza kubadilisha the way system ilivyo. Endeleeni kutumia Jamii forums na likes inaweza kusaidia rather than you coming. Tupambane mafisadi waishe then ndo mnaweza rudi.
 
tatizo sio kurikodi au nini ndugu alichotaka ni jinsi gani maudhui yamekufikia kuhusu msatakabali wa nchi na matatizo yalivyo cha msingi ni kujadili tu.yawezekana huyu bwana yupo hapa bongo
 
Kwanza Hongera sana ndugu mmegusa mengi sana. Ingefaa kama hii convrsation ungeitupa kwenye one of these news paper. So natural. Safi sana.


Kweli si issue ya kuzingatia. Lets deal with the content.



Hapo ndo tunatofautiana ndugu. Kwanini mtu arudi huku tz. Arudi ili apoteze ramani zote au? Mimi simshauri mtu arudi bongo, ataishia kuwa frustrated and so. Fanyeni kazi huko huko mkipata kitu tumeni nyumbani kwa ajili ya kuwekeza ukirudi hamna utakachoweza kubadilisha the way system ilivyo. Endeleeni kutumia Jamii forums na likes inaweza kusaidia rather than you coming. Tupambane mafisadi waishe then ndo mnaweza rudi.


Chukua tano babake

Nirudi bongo pahali penyewe interest rate ya mikopo inakuwa noma?? Ngoja tutarudi siyo kesho lakini. Ila nadhani hakuna asiyetuma fedha nyumbani.
 
acha fiksi,
mlipokuwa mnaongea ulikuwa unaandika, au unarecord na simu/ laptop
Aaah Joy, acha kutukatia stimu. Maongezi mazuri sana, hata kama hayajaandikwa word-to-word kama yalivyozungumzwa, lakini mazingira yanaleta ujumbe! Mkuu mshua wako yuko makini sana, ila huyo Blanca ungempa jina la kimatumbi ili utuconvince kwamba utarudi home badala ya kubadili uraia!
 
Kweli si issue ya kuzingatia. Lets deal with the content.



Hapo ndo tunatofautiana ndugu. Kwanini mtu arudi huku tz. Arudi ili apoteze ramani zote au? Mimi simshauri mtu arudi bongo, ataishia kuwa frustrated and so. Fanyeni kazi huko huko mkipata kitu tumeni nyumbani kwa ajili ya kuwekeza ukirudi hamna utakachoweza kubadilisha the way system ilivyo. Endeleeni kutumia Jamii forums na likes inaweza kusaidia rather than you coming. Tupambane mafisadi waishe then ndo mnaweza rudi.

No ndugu yangu tena kuweni sana hapa JF na pia tafuteni kujua ya home ok, na pia hatutaki mradi na ki degree moja au bila kuwa mmeridhika kuwa mmeelimika na kuchuma vya kutosha, kwani hamtatufaidia sisi wala nyie wenyewe, issue ni je huo uraia na familia mnazotengeneza huko mnania kweli ya kuchuma na kuja kuwekeza au kushika nchi au ndo mkienda ndo buriani? Mtarudi kukibalika - Nani anabadili??? Hata kupigania muweze kupiga kura mkiwa huko naona hamna haja kabisa jamani
 
Edison hongera sana mkuu.nimeipenda style yako ya maongezi na Babu yake Blanca.
 
Thanx for sharing with us. Msalime Blanca na Babu yake. Plz mfahamishe Babu Blanca ajiunge na JF kuna vitu vingi sana atatusaidia hapa..
 
kuna fiks hapo mkuu. naziona laivu. huwezi ukazungumza formally hivyo na baba yako
Big up Edson , mie nakufagilia sana coz kwa mwenye akili zake atazingatia zaidi ujumbe wa thread yako kuliko methods zilizotumika,
Mkuuu MZIWANDA usiwe na mawazo hasi kwa vitu ambavyo hujawahi kuona au kusikia au kuexpirience, hiyo conversation ipo na inawezekana kabisa depends na wewe kama mzazi unamleaje na kumpa maadili gani mwanao, sasa kama wewe ni baba au mama ndio ujifunze umlee mwanao siku moja muweze kuongea kwa syle hii au zaidi ya hiii, yale mazoea ya kusikia gari la baba au sauti ya baba nje watoto wote wanakimbia sebuleni wanakimbilia vyumbani kwao imepitwa na wakati tuwafanye watoto zetu kuwa marafiki zetu ili tuweze kujua shida zao na kuwashauri tuwezavyo.
 
asante sana josm.nimekuelewa vizuri kwenye private essage yako! ruksa kaka
 
tatizo sio kurikodi au nini ndugu alichotaka ni jinsi gani maudhui yamekufikia kuhusu msatakabali wa nchi na matatizo yalivyo cha msingi ni kujadili tu.yawezekana huyu bwana yupo hapa bongo


Na hii ndiyo mantiki ya msg hii yaani ni kasi gani taifa letu linaenda. Yuko wapi hii haituhusu shida hapa ni matukio gani yanatukia katika taifa letu.
 
tatizo sio kurikodi au nini ndugu alichotaka ni jinsi gani maudhui yamekufikia kuhusu msatakabali wa nchi na matatizo yalivyo cha msingi ni kujadili tu.yawezekana huyu bwana yupo hapa bongo
Nakubaliana na wewe Mkuu, binafsi sioni haja ya kuuchunguza uhalisia wa mwandishi. Inawezekana kweli ni mazungumzo kati yake ba baba yake hii inategemea sana staili ya malezi, inawezekana pia mkuu yupo masomoni ughaibuni na wala hakuna ubaya katika hili, lakini inawezekana pia ni staili ya mwandishi kufikisha mawazo yake kwa jamii, na inawezekana pia mwandishi yuko hapahapa bongo. Kikubwa nadhani ni kuyatafakari maudhui ya mazungumzo (ya eddy na baba yake) tunakubali kuendelea kuishi kama wawindaji?
 
naona somo limeanza kuwaingia wazee wetu,maana wao ndio wapigaji wakuu wa kura kuliko vijana.nimepata faraja sana kusoma hii thread maana wakati mwingine hua nashikwa na hasira sana napoona vijana wenzangu wanakuwa washabiki wakubwa wa siasa lakini siku ya hukumu ikifika(kupiga kura) unakuta mistari mireefu wamejipanga wazee tu,hivyo babu yake blanca ni kielelezo cha ushahidi kuwa wazee wetu wamechoka na porojo za wanasiasa na sasa wanaangalia utekelezaji wa ahadi na ILANI za chama tawala.hivyo naamini 2010 CCM watakuwa na wakati mgumu sana na namuomba MWENYEZI MUNGU iwe hivyo.
 
Back
Top Bottom