Wosia....

Mbu

JF-Expert Member
Jan 11, 2007
12,753
7,844
...bANDUGU wAPENZI...

Kila tunapokaribia mwisho wa mwaka, ajali na vifo huwa ni kama hitimisho la mwaka. Hebu tukumbushane yaliyo muhimu, sio kila siku kusifia Infidelity tu, roho ikiacha mwili tunawaachia wafiwa kivumbi.

Hivi, kuna umuhimu katika wosia kuwataja watoto ulokuwa umemficha mwandani wako? au ndio potelea mbali, watajuana wenyewe?

Sio siri, wapo kina dada waliozaa enzi za sekondari, watoto wakarithiwa na bibi bila mume kujua mpaka kifo kilipotenganisha, ...kama ilivyo kwa wanaume waliozalisha na kuficha watoto mpaka siku ya msiba, ndipo kijana au binti alipoletwa.

Kwa mtizamo wako na itavyokugusa habari hii, nini unaona ni nafuu kwako. Kuujua Ukweli toka kwa wosia wa marehemu mke/mume? au bora ya kitendawili anachofukiwa nacho -hakuona haja ya kukwambia?
 
kweli haya yanatokea sana...
hata mimi nilizani tu watatu kwenye familia yetu ..
mapaka nilipo mpoteza mzazi wangu mmoja ndo tukajua tuko watano..

kwa kweli unauma sana miaka 20 na kitu unadhani we ndo wa kwanza au we ndo wa mwisho lakini sio...
na cha kushangaza zaidi ni pale yule ambaye mlikuwa hamumjui ndo kafanana fika na mzazi...

kwa kweli mi naona ni bora mtu aseme tu kabla kifo hakija mkuta...
kwa mimi naona ni borea ka unawajua ndugu zako wote....

haya matatitoza yanaweza kuwa mkubwa zaidi baadaye pale ndugu wanapokutana halafu hawajuani....
ni damu yako hata ukikataa kwa hiyo ningependa kusema jamani hakikisha watoto wako wote wanajuana...
ile ya mtu anakuja kwenye mazishi halafu anasema mi ni kaka au dada yako ni mbaya sana.
hujui sasa uliye au ucheke..
 
kweli haya yanatokea sana...
hata mimi nilizani tu watatu kwenye familia yetu ..
mapaka nilipo mpoteza mzazi wangu mmoja ndo tukajua tuko watano..

kwa kweli unauma sana miaka 20 na kitu unadhani we ndo wa kwanza au we ndo wa mwisho lakini sio...
na cha kushangaza zaidi ni pale yule ambaye mlikuwa hamumjui ndo kafanana fika na mzazi...

kwa kweli mi naona ni bora mtu aseme tu kabla kifo hakija mkuta...
kwa mimi naona ni borea ka unawajua ndugu zako wote....

haya matatitoza yanaweza kuwa mkubwa zaidi baadaye pale ndugu wanapokutana halafu hawajuani....
ni damu yako hata ukikataa kwa hiyo ningependa kusema jamani hakikisha watoto wako wote wanajuana...
ile ya mtu anakuja kwenye mazishi halafu anasema mi ni kaka au dada yako ni mbaya sana.
hujui sasa uliye au ucheke..

...dah, pole sana afrodenzi.
kuna msemo 'mficha maradhi, kilio kitamuumbua...'
siku ya msiba badala watu kuomboleza, panageuka sehemu ya kustaajabiana.

Na akishajitokeza mmoja, mnabakia na wasiwasi huenda kuna mwingine ataibuka pia...
Misibani kuna vituko, acheni tu.
 
Naomba kueleweshwa kitu hapa... Mbu plz...

Wosia... Lazima uandikwe na Baba tu? Mama katika hili suala na masuala mengine (kwa mfano Mama anakuwa amejenga majumba au Miradi ambayo Mume haijui, au ana watoto ambao alizaa kabla) hatakiwi kiandika wosia?

Ni vizuri watoto wakifahamiana, unaweza kukuta hawajuani na mwisho wa siku wakawa wachumba... Bora uondoe fedheha...

 
Kama watoto hawajulikani ndani ya ndoa, ni hatari sana kuwataja kwenye usia, utakuwa unaleta ugomvi usiomithilika, na kwa binafsi yangu hata ukiwaandikaje kwenye wosia wako hawapati hata mia ya urithi...Maliza kesi mapema watambulishe watoto wako kwa mkeo, na mbele ya wanandugu, then uwaaandike kwenye wosia!
 
Kama watoto hawajulikani ndani ya ndoa, ni hatari sana kuwataja kwenye usia, utakuwa unaleta ugomvi usiomithilika, na kwa binafsi yangu hata ukiwaandikaje kwenye wosia wako hawapati hata mia ya urithi...Maliza kesi mapema watambulishe watoto wako kwa mkeo, na mbele ya wanandugu, then uwaaandike kwenye wosia!

Hivi mali zilizochumwa kwa pamoja katika ndoa....nani mwenye mamlaka ya kuziweka katika wosia??? Mke au mme???? Mke ana nafasi gani katika wosia/mirathi ya mme....?
 
kweli haya yanatokea sana...
hata mimi nilizani tu watatu kwenye familia yetu ..
mapaka nilipo mpoteza mzazi wangu mmoja ndo tukajua tuko watano..

kwa kweli unauma sana miaka 20 na kitu unadhani we ndo wa kwanza au we ndo wa mwisho lakini sio...
na cha kushangaza zaidi ni pale yule ambaye mlikuwa hamumjui ndo kafanana fika na mzazi...

kwa kweli mi naona ni bora mtu aseme tu kabla kifo hakija mkuta...
kwa mimi naona ni borea ka unawajua ndugu zako wote....

haya matatitoza yanaweza kuwa mkubwa zaidi baadaye pale ndugu wanapokutana halafu hawajuani....
ni damu yako hata ukikataa kwa hiyo ningependa kusema jamani hakikisha watoto wako wote wanajuana...
ile ya mtu anakuja kwenye mazishi halafu anasema mi ni kaka au dada yako ni mbaya sana.
hujui sasa uliye au ucheke..

ni kweli kabisa afro yaani wazazi sijui huwa wanawaza nini ni bora watu mjuane kabisa sio kustukizana siku ya msiba na kuanza kugombani sijui kijumba alichoacha mzazi. Hilo la kufanana mara nyingi watoto wa nje huwa wanafanana sana na baba sijui kwa nini, mimi mwenyewe nasikia baba ana watoto wawili huko nje tena wakubwa lakini hajawahi hata kutuonyesha na nasikia ndio wamefanana haifai mimi naona bora ijulikane tu mapema na watoto wajuane
 
Hivi mali zilizochumwa kwa pamoja katika ndoa....nani mwenye mamlaka ya kuziweka katika wosia??? Mke au mme???? Mke ana nafasi gani katika wosia/mirathi ya mme....?


mh! hii naona itaanza kuleta mkanganyiko maana zamani baba ndio alikua kila kitu anafanya kazi yeye na mali zote zilikua zake sasa siku hizi wote mnafanya kazi wote labda mmechangia kujenga nyumba etc. sasa kama baba ana watoto wa nje sijui ndio watapata urithi ama? hii ni ngumu kidogo. Mimi naona tuwafunze watoto kutafuta mali zao wenyewe na wasiwe na mawazo ya kurithi mali za mzazi, mpe mtoto elimu nzuri, mfundishe maadili mema hata hao watoto wenu wa nje wapeni elimu nzuri hata kama kutakua na ambae si msikivu labda anaweza kuwa mmoja tu na hata mzazi akifa wale wengine waliojitafutia mali watamuachia tu kwani wanazo zao hii itapunguza watoto kugombania mali ambazo hata hawajui zimepatikanaje
 
...dah, pole sana afrodenzi.
kuna msemo 'mficha maradhi, kilio kitamuumbua...'
siku ya msiba badala watu kuomboleza, panageuka sehemu ya kustaajabiana.

Na akishajitokeza mmoja, mnabakia na wasiwasi huenda kuna mwingine ataibuka pia...
Misibani kuna vituko, acheni tu.
yaani mi nakwambia ni balaa tu halafu huyo mtoto wa nje ni mkubwa tu
na ye anawatoto wawili.. yaani wajukuu..
eti mi shangazi ambaye hata nilikuwa sijui ..
kwa kweli lakini utafanyeje..
ambaye unataka kumuuliza haya maswali mazito uliyonayo moyoni ndo kasha toweka hivyo..
mpaka mkutane tena kwemye makao mapya..
kwa hiyo sisi nikupendana tu nakusaidiana sasa...( kwani haya si makosa yao kabisa)
haina tena maana ya kugombana....
Yaani kilicho bakia ni kumwomba Mwenyezi Mungu atusaidie tu ...
 
Mbu:

Sisi kwetu tumezaliwa 34, sasa sijui "Will" itaandikwaje? Wote tunafahamiana na Mama zetu wote wapo!
 
ni kweli kabisa afro yaani wazazi sijui huwa wanawaza nini ni bora watu mjuane kabisa sio kustukizana siku ya msiba na kuanza kugombani sijui kijumba alichoacha mzazi. Hilo la kufanana mara nyingi watoto wa nje huwa wanafanana sana na baba sijui kwa nini, mimi mwenyewe nasikia baba ana watoto wawili huko nje tena wakubwa lakini hajawahi hata kutuonyesha na nasikia ndio wamefanana haifai mimi naona bora ijulikane tu mapema na watoto wajuane

yaani mi nakwambia saa nyingine wazazi hawatendei haki watotot wao..
sijui wanavyokaataa inamaanisha nini..... yaani mambo yakiuupuzi kama haya yananiudhi sana..
sisi tumesha kuwa ni watu wazima sasa.... tunatakiwa tuelezwe kila kitu kuhusu familia zetu..
yaani Maty mwaya mi nakuomba sana uwajue hao ndugu zako watafute mwenyewe..
yasije yakakukuta yaliyotukuta sisi..
usikute na we ni shangazi ambaye hujijui kama mimi hapa..
au mshike shati baba mpaka akwambie..
Pole sana mwaya... na usijali kama kweli ni ndugu zako utawajua tu damu ni nzito kuliko maji...
 
Mbu:

Sisi kwetu tumezaliwa 34, sasa sijui "Will" itaandikwaje? Wote tunafahamiana na Mama zetu wote wapo!

Unaandika mali a+b+c gawanya kwa 34 ndo urithi kila mtu....jinsi ya kugawa mtajua...
 
Naomba kueleweshwa kitu hapa... Mbu plz...

Wosia... Lazima uandikwe na Baba tu? Mama katika hili suala na masuala mengine (kwa mfano Mama anakuwa amejenga majumba au Miradi ambayo Mume haijui, au ana watoto ambao alizaa kabla) hatakiwi kiandika wosia?

Ni vizuri watoto wakifahamiana, unaweza kukuta hawajuani na mwisho wa siku wakawa wachumba... Bora uondoe fedheha...

...kwa ninavyoelewa usia lazima uandikwe/utamkwe na baba/mume na mama/mke. Wote tuna haki sawa.

Kama watoto hawajulikani ndani ya ndoa, ni hatari sana kuwataja kwenye usia, utakuwa unaleta ugomvi usiomithilika, na kwa binafsi yangu hata ukiwaandikaje kwenye wosia wako hawapati hata mia ya urithi...Maliza kesi mapema watambulishe watoto wako kwa mkeo, na mbele ya wanandugu, then uwaaandike kwenye wosia!

...PJ, kimila na kiserikali ikithibitika watoto ni wa marehemu, wanahaki ya kupata sehemu ya urithi. Watapata wanachostahili.

Hivi mali zilizochumwa kwa pamoja katika ndoa....nani mwenye mamlaka ya kuziweka katika wosia??? Mke au mme???? Mke ana nafasi gani katika wosia/mirathi ya mme....?

...mnh, RR hiyo inategemeana zaidi na matakwa ya marehemu na makubaliano ya wanandugu, ingawa kidini na kiserikali kuna miongozo yake. Si vibaya tukakumbushana tofauti ya Wasia (wosia) na Mirathi vile vile.

wasia nm maagizoya mtu kwa watu wakeambayo anataka yatimizwe iwapo atakufa au kuondoka; usia.

mirathi nm 1 vitu na mali yanayoachwa na mtu aliyekufa na kupewa watu wakekwa mujibu wa mipango maalumu

[/SIZE][/B]

mh! hii naona itaanza kuleta mkanganyiko maana zamani baba ndio alikua kila kitu anafanya kazi yeye na mali zote zilikua zake sasa siku hizi wote mnafanya kazi wote labda mmechangia kujenga nyumba etc. sasa kama baba ana watoto wa nje sijui ndio watapata urithi ama? hii ni ngumu kidogo. Mimi naona tuwafunze watoto kutafuta mali zao wenyewe na wasiwe na mawazo ya kurithi mali za mzazi, mpe mtoto elimu nzuri, mfundishe maadili mema hata hao watoto wenu wa nje wapeni elimu nzuri hata kama kutakua na ambae si msikivu labda anaweza kuwa mmoja tu na hata mzazi akifa wale wengine waliojitafutia mali watamuachia tu kwani wanazo zao hii itapunguza watoto kugombania mali ambazo hata hawajui zimepatikanaje

...kweli kabisa Maty, no wonder wazazi tunashurutishwa urithi muhimu kwa watoto ni ELIMU!

Mbu:

Sisi kwetu tumezaliwa 34, sasa sijui "Will" itaandikwaje? Wote tunafahamiana na Mama zetu wote wapo!

...Baba Enock, madhali wote mnafahamiana na kwa idadi, hakuna kilicho kigumu kwenye kugawana mirathi iwapo Urithi utajumuishwa kwenye usia/wasia. Kumbuka, Usia ni mwongozo tu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom