Uchaguzi 2020 World Bank yapitisha Mkopo wa Zaidi ya Trillion 1 Uliopingwa na Wanasiasa pamoja na Wanaharakati

Egnecious,
Taarifa imejawa na jina Zitto kila mahala badala ya hoja nk.
Hoja za huyo nidhaifu,zakusifu na kujipendekeza kwa rais mkufunzi gani mjinga mjinga hivi?? Hiyo hela itumike vizuri kurekebisha elimu yetu tusiwe na wasomi wapumbafu.

- hajaeleza pesa hiyo itatoka lini, zitto alitaka isitolewe mapema itaingizwa kwenye kampeni za 2020.

- hajaeleza sharti la wasichana wanaopata mimba imeamuliwaje, kijana aliwaomba waibane serikali warudishwe shule nk. Hoja za zito siyo hela isitolewe no WB iibane serikali kuridhia mambo kadhaa swala ni je, hojazake zimezingatiwa?

Ukiwa msomi usiongee kama umeishia darasa la saba onesha tofauti ...stupid mkufunzi
 
Taarifa imejawa na jina Zitto kila mahala bserikali nk.
oja za uyo MTU hivi mkufunzi gani mjinga mjinga hivi?? Hiyo hela irekebishe elimu yetu tusiwe na wasomi wapumbafu.
- hajaeleza pesa hiyo itatoka lini, zitto alitaka isitolewe mapema itaingia kwenye kampeni za 2020.
- hajaelsza sharti la wasichana wanaopata mimba imeamuliwaje, kijana aliwaomba waibane serikali nk.
Ukiwa msomi usiongee kama umeishia darasa la saba onesha tofauti stupid mkufunzi
Huyo jama ni kiazi, anachosha.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Lumumba buku 7 upo kazini.

Huo mkopo mtaanza kuupokea june 2021 tena kwa awamu. Na ikitokea hesabu hazijakamilika kwenye awamu iliyopita hampewi hela.

Kama ndio mlikuwa mnazitegemea kama hela za kufanyia kampeni mwaka huu basi imekula kwenu... Egnecious,
 
Kaka mkuu amegoma tena kwa kuwakosoa WB mwenendo wake wa kutoa Mkopo Tanzania Una walakin na yeye ndo mchangiaji Maui
 
2A5FB041-289C-4E1F-B3EC-D2BB67797D34.jpeg

Hi I tunemkosea nini Kaka mkuu
 
Whether namtetea Magu kwa jinsi ufahamu wako ukutumavyo au naelezea mambo ambayo uwezo wako kwa sasa ni mdogo sana kuelewa, hayo siyo muhimu kwa sasa! Sina tatizo na hiyo fedha, ninatatizo na future ya watoto wa kike nchini ukitekeleza utaratibu unaowaonyesha kutokuwa na tangible consequences za kubeba mimba kama kupoteza nafasi ya mfumo rasmi wa shule
Huo mwongozo umeanza 2009, unataka kusema kabla ya 2009 mimba mashuleni zilikuwa chache kwavile walikuwa wanahofia hizo consequencies na hivi sasa zipo maradufu kwa sababu they have nothing to fear?

Hivi unafahamu kwamba hapa tunazungumzia watoto wenye umri kuanzia 13 years, na majority ya waathirika ni young primary school gals, na wachache wa O-Level ambao na wenyewe bado wanakuwa na ufahamu mdogo?

Hivi unaamini kabisa kwamba watoto kama hao wakiona hawawezi kufukuzwa shule ndo basi tena watazaa hovyo hovyo kwa sababu hawana cha kuhofia?!

Hivi kabisa unaamini wale wasiopata mimba hawafanyi mapenzi kwa sababu wanahofia kufukuzwa shule?!

Hivi ulishawahi kujiuliza ni kwanini hili tatizo lipo sana vijijini ambako kwa kawaida ufahamu ni mdogo zaidi ukilinganisha na mijini?

Hivi ulishawahi kujiuliza ni kwanini mimba za hovyo hovyo vyuoni hazipo ingawaje sio haramu kupata mimba vyuoni?!!

Au hapa natakiwa kukukumbusha kwmba hizi mimba zinapatikana kutokana na kukosa uelewa na wala si kwa sababu ya kufanya ngono, na ndio maana wasichana kuanzia A-Level hadi vyuo "hawapati" mimba licha kwamba huenda wao ndio wanacharazwa zaidi kuliko hao wanaopata mimba!!!

Tunafahamu moja ya sheria kali kabisa Tanzania ni kumpa ujauzito mwanafunzi!

Now take an example of this gal: she's 15 or even less! Kwa sababu yoyote ile, anapata ujauzito! Unamtimua shule! Aliyempa mimba anaenda jela miaka 30! Na si ajabu anatoka kwenye poor family!!

Ulishawahi kujiuliza ni namna gani future ya mtoto kama huyo na yule atakayemzaa itakavyokuwa?!

Sheria zetu, na karibu duniani kote ukifanya ngono na msichana chini ya miaka 18 unaambiwa umembaka, na ukisema "alikubali mwenyewe" unaonekana mpuuzi!

Kwanini sheria inasema hivyo?! Au hapa unatakiwa tena kukumbushwa kwamba inaonekana msichana wa aina hiyo hana uwezo wa kufanya maamuzi sahihi?!

Sasa ikiwa hata 17 years girl anaonekana hana ukomavu wa akili wa kuweza kufanya maamuzi sahihi, what about wale wa primary schools ambao majority wapo under 15?!
Sitaki hata kuwaza kizazi gani tutakachokuwa tunatengeneza(kizazi cha watoto wazazi)
Tangu muanze kuwatimua shule, hicho kizazi cha watoto wazazi kimepungua?!

Narudia tena, misimamo yenu inaowaumiza ni watoto wa maskini wa vjijini kuliko watoto wa wenye uwezo na wale wa mijini! Ni kutokana na hilo ndo maana akina Zitto walisema wazi kwamba WB wakitoa mkopo watakuwa wanatoa mkopo unao-stimulate ubaguzi kati ya watoto walio nacho na wasio nacho!!

Hata mtoto wa Mwalimu wa Shule ya Msingi hawezi kupata mimba na akashindwa kuendelea na masomo, LAZIMA ATASOMA tu... tatizo ni kwa maskini!
 
Chige,
Tangu lini zito akajali masikini ww? Hicho ni kiini macho na siasa za maji taka! Zito aliwajali acasia na wenzie! Na ustake kutuaminisha mimba wanabeba watoto wa maskini! Na pointi hapa ni kuzuia mimba hizo za utotoni zisitokee!

Na kwa kiasi kikubwa sheria zetu ziliwatisha watoto waliokuwa wakijitambua kutoshiriki mapenzi kwa kuhofia kukatiza ndoto zao za kufikia malengo yao kiuchumi! Wakati huohuo hazikuwatisha kivile wale watoto mbulula wasiojitambua na wasio na malengo waliojipangia kuamua kufupisha safari! Pia kuna wazazi ambao wao waliwashawishi watoto wao kutoendelea na masomo na badala yake waolewe! Kijumlisha na matukio ya ubakaji wa kibabe, Sceneria zote hizi ndio zilipelekea idadi hiyo ambayo kimsingi ni ndogo ya watoto kuwa wazazi!

Huo muongozo japokuwa ni wa 2009, haujawa 'implemented' kwa kuwa unapingana na all norms za kitz! Hauna mantiki, na hata walioupitisha tungetamani kuwajua!

Hao wanaolazimisha wazazi wasome darasa moja na watoto! Ili iweje? Huyu mzazi hata network yake inakuwa imebadirika, akimuwaza mwanae, mapenzi ya baba mtoto, na hata kuwazia makuzi ya mwanae ambae atakuja kumuona babae miaka 30 ijayo!

Huyu mzazi anahitaji akae kwenye darasa la watu wazima ili asaidiwe kimawazo na wazazi wenzake!

Tangu elimu bure ianze kuwa implemented, wazazi waliokuwa wakishawishi binti zao kutoendelea na masomo wamepungua kama sio kuisha kabisa! Hizo hela zinalenga kuongeza nguvu ktk kufanya maboresho!

Wapuuzi kama akina Zito wakijua jinsi hilo litakavyoipaisha serikali ya awamu hii na hivyo kutokuwa na upinzani 2020...kwa faida za kisiasa za kwake binafsi zito na wapuuzi wengine wakajiokoteza vijisababu visivyokuwa na kichwa wala kiwiliwili kwenda kuzuia mkopo huo kwa msaada wa mabwana zao mabeberu!

Hii ni hujuma kwa nchi na wananchi kwa sbb ya roho mwaya na ubinafsi wa hali ya juu wa Zito na wahuni wenzie! Na kwa hili wamechemsha sana maana wamejisababishia povu kwa wananchi ambalo linaendelea kumiminika mpaka uchaguzi!

Hata hivyo, mkopo huo ulilenga kuboresha mazingira ya mtoto wa kike ili asome pasi bugudha!
 
Tigershark,
Mtapata taabu saaaana mkuu! SHETANI HAJAWAHI KUMSHINDA MWENYE HAKI, zitto mwenyewe katoa pongezi kupitia twiter! Naubaya sasa nayeye zitto yupo copyd.

Niaibu ya mchana kweupe, naitakuwa moja ya siraha yakumpigia zanziber na kigoma.
 
Usiseme wazazi na wanafunzi,sema wanafunzi waliozaa na ambao hawajazaa!
Halafu tumia tafiti,je kuna madhara gani kufanya hivyo?Sio kuendeshwa kwa hisia tu!
Hakuna madhara kwa kweli hata kwenye Ilani ya CCM ya 2015 imewekwa vizuri tu kuwa watarudi shule kuendelea na masomo.

Shida inatokana na huyu Dikteta Magufuli ambaye anataka HULKA yake kwa kitu chochote iwe sera ya Taifa. Kama kwa mfano yeye anapenda kukariri takwimu mbali mbali basi anataka hata wale ma DED kwenye ziara akiwauliza maswali watoe majibu ya kukariri.

Kuhusu wanawake kwa ujumla, Magufuli ni misogynist, yaani ni kati ya wanaume wanaonyanyasa wake zao. Hana heshima kabisa kwa mwanamke na ushahidi upo. Kwa hiyo kama nchi lazima tupinge kwa nguvu zote nchi kuendenshwa kwa hulka za mtu mmoja.
 
Egnecious,
Huna haja ya kukuza mambo, kumbeza mtu mmoja na kumtukuza mwingine! Almost kilichofanyika ndicho kilikua kilio cha wanaharakati wote kwamba ni lazima yafanyike maboresho ili watoto waliokatiza masomo wapate fursa ya kuendelea na masomo.

Kama umeielewa hiyo article bila shaka utagundua kua mapungufu yaliyopigiwa kelele yameboreshwa. Tusipende kua bendera fuata upepo!
 
Wapi tunaweza ingilia ili kuichallenge hii ripoti ya wasomi wa Benki ya Dunia ndugu yangu Light?

Labda tuwa challenge kwenye hizo data za enrollment au dropouts au kwenye gender gap au wapi sijui ndugu Light au ngoja tutafute usaidizi kutoka kwao Karl Peters ingawa nao sasa wako busy na COVID-19!

Sijui tufanye nini sasa kwani hayo mapesa yatakuwa disbursed anytime. Ibilisi tusaidie katika hili!
 
Back
Top Bottom