WORLD BANK: Tanzania economic growth will drop sharply to 2.5% in 2020 from the projected 6.9% by the government due to effects brought by COVID-19

Benki ya Dunia: Ukuaji wa uchumi wa Tanzania kupungua sana

Benki ya Dunia imekadiria kuwa kutokana na mlipuko wa COVID-19, ukuaji wa uchumi wa Tanzania mwaka huu utapungua sana na kufikia asilimia 2.5 kutoka asilimia 6.9 kama ilivyokadiriwa na serikali mwaka 2019.

Benki ya Dunia imesema uchumi wa Tanzania utaathiriwa na janga la COVID-19 na msukosuko wa uchumi wa dunia.

Ripoti hiyo iliyotolewa na Benki ya Dunia imesema kuwa serikali ya Tanzania imechukua hatua, na inatarajiwa kuendelea kuchukua hatua za ziada za kiafya na kiuchumi, ili kupunguza athari hasi.

Lakini ripoti hiyo, ambayo ni ya 14 ya Benki ya Dunia kuhusu uchumi wa Tanzania, pia imeonya kuwa, kama hatua za ziada zitacheleweshwa au hazitafanya kazi, na kama mazingira ya nje hayataboreka mwaka huu, ukuaji wa uchumi wa Tanzania huenda utapungua zaidi.

Tathmini ya ripoti hiyo ya Benki ya Dunia inaonyesha kuwa janga la COVID-19 limevuruga maisha ya wananchi wa kawaida ambapo imetabiriwa kuwa Watazania nusu milioni wataingia katika kundi la watu wanaoishi chini ya mstari wa umasikini. Watakaoathirika zaidi ni watoto wanaoishi mijini ambao wamejiajiri na wenye biashara ndogo ndogo.

4bva0b7fa481da1o4it_800C450.jpg


Sent from my JSN-L21 using JamiiForums mobile app
 
Ripoti hiyo imepunguza ukuaji wa uchumi wa Kenya hadi asilimia 1% hivyo wako sahihi kwa kuzingatia mwenendo wabiashara za kimataifa na vitu kama utalii ambavyo kwa kweli umeathirika sana. Labda tungejadili ni vipaumbele gani kwa sasa serikali iwekeze huko ili basi athari za covid zisiwe kubwa sana kwenye uchumi wetu
 
Kumbe unalijua hilo, sasa mbona huwa mnakomalia kwenye kuathirika kwa uchumi wa Kenya.
Kuathirika kupo ila kinachotofautiana ni kiwango cha kuathirika kama tunategemea kuwauzia ninyi chakula na ninyi hamna ela mmefungiwa ndani kwa akili ya kawaida lazima nasi tuathirike.
 
Kuathirika kupo ila kinachotofautiana ni kiwango cha kuathirika kama tunategemea kuwauzia ninyi chakula na ninyi hamna ela mmefungiwa ndani kwa akili ya kawaida lazima nasi tuathirike.

Hela tunazo siku zote, jeuri ya hela inatuwezesha kununua chakula popote duniani, msio na hela ndio mtateseka maana hamjafikia middle income, mko huko chini maskini wa kutupwa kuleeeeeee.
 
Tuliishakosea kwa kuwa na vipaumbele visivyostahili sasa ikiongezeka na huo mdororo wa uchumi ndio itakuwa kaburi letu.
 
Kumbe unalijua hilo, sasa mbona huwa mnakomalia kwenye kuathirika kwa uchumi wa Kenya.
Kenya itakuwa chini ya 1%, upo? Na vyakula mtakuwa hamna na muendelee kututukana vizuri tutaheshimiana tu
 
... ni kweli ila unadhani uchumi wa Marekani au Japan au Canada ukishuka hadi 0.5% na wa Tanzania ukikua kwa 3% kwa kipindi hicho hicho unadhani ni nchi ipi itaathirika zaidi kwa maana ya hali ya maisha ya mwananchi wa kawaida? Elewa WB wanachomaanisha!
Wewe ndiye ume misinterpret point yangu.Mimi nilimaanisha tu hakuna nchi ambayo haitatetereka kiuchumi kipindi hiki! That's the essence of my point and kindly stick on it.
 
Back
Top Bottom