Workers Compensation Fund wekeni mambo wazi kuhusu interview

ElBaradei

Member
May 4, 2017
40
14
Wakuu ninaandika swala hili kwa masikitiko makubwa sana... Ni hawa ndugu zetu wa Workers Compensation Fund..(WCF) ambao kwa mara ya kwanza mwezi march 2017 Katika website yao walitoa majina ya waliofanya written interview mnamo 18/03/2017 na baadae wakaambiwa wasubiri baada ya muda watapewa majibu kwa ajili ya oral interview.

Lakini mpaka leo hii hakuna kilichoendelea na kuna uvumi tu wengine wameshaajiriwa na wengine wanasema wamepigiwa simu kwa ajili ya interview mwezi July 2017.

Kwanini WCF WASITOE MAJINA KAMA WALIVYOTOA SHORTLIST YA KWANZA? WATOE NA WAWEKE MARKS WALIZOPATA WATU NA IFIKIE MWISHO AJULIKANE ALIYEFAULU NANI NA ALIYEFELI NANI... Ifike mwisho sasa kufichaficha mambo wakati mara ya kwanza walianika majina kwenye webiste yao......
 
Back
Top Bottom