Tenyaaaaa.....!!!!
Shosti Marry Hunbig nina hamu ya Mchambo balaa.
Afu shost huo Ubini wa baba naufananisha na wa mdada mmoja tulimaliza nae chuo.
Hivi nyie vipi, nimeshasema wanaume hamtakiwi au nyie mashoga?
Ndio mkome kufuatilia habari zetu, haya ni mambo ya jikoni hayawahusu
Hewaaa, hapo umenena Da BADILI TABIA, na ndio maana nikahitaji wanwake tu kwenye hiki kibaraza, wanaume maroufouk kwa sababu watamtetea tu huyo mdingi.
Tumepanga juma lijalo tukalianzishe na mama yake akileta za kuleta tunamchapa yeye na bintiye maana mama yake amepinda mdomo kwa kuchonga na ndio maana haoleki yeye na wanaye, ya nini kutuletea laana na nuksi katika familia.
Mdingi hana hata haya, umri wote huo kukimbizana na vibinti, atafia kifuani akome.
Zindunaaaaaaaaa! ukitaka kula na kipofu usimshike mkono.
Kwanza mshikeni mama yenu kwa nguvu zote na mumuonyeshe baba kuwa hamna muda naye
pili jitahidini kuwa wakimyaaaaa kama vile hamjui nn kinaendelea na wala msimsemeshe baba yenu vibaya, mpeni heshima yake,
Huyo shoga yako usimnunie, jifanye mko pamoja na ushoga uendelee, ili baba akupende wewe akuone unampa support kumbe wewe ndiyo mbeba sumu No 1
Wewe si unawajua wanaume zake wote, Basi wewe chakufanya unajidai ni shoga yako wakati huo unamtengenezea mabomu ya kumlipua
jidai Uko pamoja na baba at the sama time uko na shoga
siku mtafutie shoga Bwana na mwambie huendi kusema kwa Baba yako , si atazoea na kuona wewe ni shogaye, Basi Hapo hapo unamlengeshea Baba akamuone.
Nakuapia Zinduna Baba akimfumania si ndiyo mwusho wa mchezo atapewa TALAKA YAKE mzee atarudi kwa mama
wewe utakuwa umeshamaliza kazi yako
Na pia najua hata mtoto pia ahtopewa matunzo tena , na wewe Hapo ndipo pa kumkatia Line, Unafunga vioo , weka kabisa Tinted
MM ndivyo napigana, vita yangu ni ya kimyaaaaaaaa lkn nashinda Always
Taratibu Mh. Mwenyekiti, huyo baba nae hajatulia kama Bishanga, huezi jua labda mdada wa watu shida zimemtia majaribuni! Ila mie huwa nasemaga hakuna kiumbe mbaya humu duniani kama mwanamke (mtanisamehe ila ndio ukweli) Madame B mwanamke anakuchekea huku anakuua ati. Tumenyimwaga uso wa aibu kudadadadeki!Ukute huyo shakunaku mtembelea vidole yupo humuhumu anaisoma post yake.
Nyoooo na tukikukamata,utahara kama bata.
Pashkuna mkubwa we,
Mja la lakhaana,fisadi mkubwa we.
Na ungezaa na Baba yangu (r.i.p(sorry)),
Walah nakwambia hyo mimba ningeihamishia kwa Baba yako mzazi asiejulikana alipo.
Gegedu mkubwa wee.
Nakutamani.
Taratibu Mh. Mwenyekiti, huyo baba nae hajatulia kama Bishanga, huezi jua labda mdada wa watu shida zimemtia majaribuni! Ila mie huwa nasemaga hakuna kiumbe mbaya humu duniani kama mwanamke (mtanisamehe ila ndio ukweli) Madame B mwanamke anakuchekea huku anakuua ati. Tumenyimwaga uso wa aibu kudadadadeki!
Lisa, hii ndo akili niliyokuwa nayo unajua. Nilikuwa naogopa hata kuisema. Hufai wewe, salute!
Hahahaha! Wanawake wabaya mpendwa , kama huyo rafikie Zinduna lol, anaenda kwa mama Zinduna shikamoo mama! Mama wa watu anaitika marahaba mwanangu, karibu nyumbani lol. Anamchoraaaa kudadadeki! Inauma asee acha mama wa watu presha ipande.Yani acha shost sweetlady.
Wanawake sisi wabaya sie acha tu.
Ukute hapo huyo baba akiwa nae siri zenu zoote za home anamwagia huyo Shetwani wa kike mchambia wima.
Aliekosa uso akapewa komwe.
Yani mie ningekuwa Zinduna,ningekuwa nishagawana majengo ya Serikali na huyo Kibibi-duka aliekosa bwana akaja zaa na Mshua anaetufanya tusiioteshe majani njia ya chooni.
Alaaa...
Nahs huyo Baba kama sio Bishanga basi ni Baba V au Dark City kama sio Asprin.