Wabunge wengi wanajifanya wanapenda mipango ya mpendwa wetu Magufuli lakini kelele zote za kusema Mama afanye ya Magufuli ni woga wa uchaguzi huru. Kama wabunge wanafanya kazi ya wananchi na wamechaguliwa kihalali uoga wa nini?
Tuwape siri tu mipango yenu sio mipango ya Mungu na kama wewe umepata kinyemela Mungu atatafuta njia za kurekebisha ili haki ipatikane.
Mama anapenda haki na sio muda ataweka viongozi kwenye tume ya uchaguzi ambao wana nia ya kupeleka nchi mbele na sio kutumia pesa kunyanyasa wananchi. Mama katokea Zanzibar ambao kule kuna ushindani ukiacha huu uchaguzi haramu wa mwaka jana. Sio kitu cha ajabu kule Zanzibar kufanya kazi pamoja kwasababu wanajua fika jinsi gani uhasama unaweza kuzuia maendeleo.
Hivyo ndugu zangu tuwapuuzie hawa wabunge ambao hawana nia na nchi. Badala ya kujali nchi wanajali matumbo mpaka leo hawana lipya. Hii ni awamu ya sita na Mama atanyoosha nchi kwasababu ana akili, anajua kujieleza, anaelewa mifumo ya serikali na matatizo ya Watanzania. Lakini Mama vilevile anajua cha kufanya ni nini. Kaimu wake Mpango anajua miradi yote ya Tanzania.
Tusubiri Tanzania iende mbele zaidi. Kuna watu wanapenda ugomvi kila siku watapata shida maana mama hana drama hizo.
Tuwape siri tu mipango yenu sio mipango ya Mungu na kama wewe umepata kinyemela Mungu atatafuta njia za kurekebisha ili haki ipatikane.
Mama anapenda haki na sio muda ataweka viongozi kwenye tume ya uchaguzi ambao wana nia ya kupeleka nchi mbele na sio kutumia pesa kunyanyasa wananchi. Mama katokea Zanzibar ambao kule kuna ushindani ukiacha huu uchaguzi haramu wa mwaka jana. Sio kitu cha ajabu kule Zanzibar kufanya kazi pamoja kwasababu wanajua fika jinsi gani uhasama unaweza kuzuia maendeleo.
Hivyo ndugu zangu tuwapuuzie hawa wabunge ambao hawana nia na nchi. Badala ya kujali nchi wanajali matumbo mpaka leo hawana lipya. Hii ni awamu ya sita na Mama atanyoosha nchi kwasababu ana akili, anajua kujieleza, anaelewa mifumo ya serikali na matatizo ya Watanzania. Lakini Mama vilevile anajua cha kufanya ni nini. Kaimu wake Mpango anajua miradi yote ya Tanzania.
Tusubiri Tanzania iende mbele zaidi. Kuna watu wanapenda ugomvi kila siku watapata shida maana mama hana drama hizo.