Wizi wa Magari: Godbless Lema achunguzwa na Polisi

Hii ndiyo habari yenyewe kutoka katika gazeti la Mwananchi:


WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha amehoji kwa nini aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam (RCO), Kamishna Msaidizi wa Polisi(ACP), Abdallah Zombe hakutoa mapema taarifa za uhalifu zinazomhusisha Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.

"Huyu kwanza sasa hivi si mwajiriwa wetu, angekuwa bado ni mwajiriwa wetu kwanza mimi ningemwuliza alikuwa wapi muda wote huo kutoa taarifa hizo na kwa nini amezitoa sasa," alisema na kuongeza;

"Ndiyo ningemwuliza ni Waziri gani aliyekuwa amemsimamia nyuma yake akamzuia kuzisema na sasa hayupo ndiyo maana ameamua kuzisema?"

Alikuwa akijibu swali kuhusu hatua ambazo jeshi hilo limezichukua dhidi ya Lema kuhusiana na tuhuma hizo ofisini kwake, Dar es Salaam jana alipokutana na waandishi wa habari kuzungumzia mafanikio ya wizara hiyo katika kipindi cha miaka 50 ya uhuru na changamoto zinazoikabili. Hata hivyo, alilitaka jeshi hilo kutokuzipuuza taarifa hizo.

Aliwaagiza maofisa wa jeshi hilo kupitia kwa Kamishna wa Polisi Utawala na Fedha, Clodwig Mtweve kumuita Zombe na kumwuliza juu ya tuhuma hizo na kuzifanyia kazi.

"Sisi tunasema kwa kila taarifa inayotolewa inakuwa na chembe ya ukweli. Labda niwape mfano mmoja, nitatumia mfano mbaya kidogo... ukikutana na mlevi akakwambia kuwa katika njia hii kuna majambazi japo ni mlevi lazima utakimbia kupitia njia nyingine;
Kwa hiyo hata hizi taarifa za Zombe hatupaswi kuzipuuzia kwani hawezi mtu mzima kusimama na kutoa taarifa kama zile hadharani hivihivi tu. Kwa hiyo maofisa wa jeshi nendeni mkae naye muulize maana inaonekana ana taarifa nyingi."

Agosti Mosi mwaka huu, Zombe alimhumu Lema kuwa alikuwa na mtandao wa uhalifu wa wizi wa magari akidai kwamba anao ushahidi wa tuhuma hizo kwa kuwa alipokea taarifa hizo wakati akiwa RCO Dar es Salaam ambazo alidai kuwa alikuwa ameshaanza kuzifanyia kazi kabla ya kukamatwa na kuwekwa ndani kwa tuhuma za mauaji.

Mauaji ya wafanyabiashara wa Mahenge
Aidha, Nahodha ameahidi kufuatilia sababu za jeshi hilo kushindwa kuwakamata askari wawili waliotajwa kuhusika katika mauaji ya wafanyabiashara watatu wa madini kutoka Mahenge mkoani Morogoro na dereva teksi wa Manzese, Dar es Salaam.

Waziri Nahodha aliahidi kukaa na maofisa wa jeshi hilo kuona ni kwa nini askari hao hawajakamatwa na kuangalia hatua za kuchukua kuhakikisha kuwa wanapatikana.

Mbali na kuangalia namna ya kuwasaka pia aliahidi kufuatilia kuona kama askari hao walishafutwa kazi au wanatambulika na kama wanaendelea kulipwa mshahara na ambaye anauchukua.

Alitoa ahadi hiyo baada ya kutajiwa majina ya askari hao ambao ni pamoja na Koplo, Saad Alawi aliyekuwa akifanya kazi katika kituo cha Oysterbay ambaye ndiye alitajwa kuwaua wafanyabiashara hao kwa kuwapiga risasi, pamoja na Koplo, James Frank ambao hadi sasa haijulikani waliko.

Awali Waziri Nahodha alionyesha kutokuwa na taarifa rasmi juu ya kesi hiyo ya Zombe na askari hao waliotoroka, pamoja na uamuzi wa Mahakama Kuu, lakini baada ya kufafanuliwa na waandishi kuwa askari hao wanafahamika alionekana kushangaa kidogo na kutoa ahadi hiyo.

"Kama walikuwa ni waajiriwa wa jeshi la polisi mimi sioni linaloshindikana, maana kama hao 13 walikamatwa kwa nini hawa wawili, mimi nadhani hili halishindikani, nitaakaa na maafisa wa jeshi kuona namna ya kulifanyika kazi."

Mafanikio ya Wizara hiyo

Kuhusu mafanikio ya wizara hiyo alisema pamoja na mambo mengine, imewaingiza askari wote katika Mfuko wa Taifa wa Bima ya Afya ili kuwawezesha kupata huduma za afya za uhakika wao na familia zao kwa lengo la kuwaongezea ari.

Pia alisema jeshi limejenga nyumba za ghorofa 30 jijini Dar es Salaam eneo la Kurasini, Barabara ya Kilwa kwa ajili ya familia 120 na nyingine katika Mikoa ya Mara, Mwanza, Iringa na Kaskazini Pemba.

"Ili kuwajengea wafungwa uwezo wa kujitegemea Jeshi la Magereza linawapatia wafungwa mafunzo ya ushonaji wa nguo, utengenezaji wa sabuni, uzalishaji wa bidhaa zinazotokana na mkonge na utengenezaji wa chumvi, samani na kilimo."
Katika jitihada za kutumia nishati mbadala, Jeshi la Magereza limeanzisha matumizi ya makaa ya mawe katika Magereza ya Ruanda, Tukuyu na Songwe mkoani Mbeya. Utumiaji wa biogas umeanza katika Chuo cha Maofisa Magereza Ukonga.

Kuhusu kuimarisha uoto wa asili ulioko kwenye maeneo ya Magereza, miti 3,701,594 imepandwa katika eneo la ekari 6,136 katika Magereza ya Malya, Bariadi, Isupilo, Msalato na Idete kwa lengo la kuhifadhi mazingira.

Waziri Nahodha aliongeza kuwa jeshi hilo limeanzisha programu ya maboresho wa miaka 10 kwa lengo la kuwajengea uwezo askari na weledi, mazingira bora ya kazi.

Licha ya mafanikio mengine kama kupambana na kupunguza uhalifu kama ujambazi wizi na wahamiaji haramu, alisema bado wizara yake inakabiliwa na changamioto nyingi ambazo alizitaja kuwa ni pamoja na ujambazi kwa baadhi ya maeneo ajali za barabarani, wahamiaji haramu na msongamano katika Magereza.

Alisisitiza kuwa licha ya changamoto hizo wizara yake imeweka mikakati ya kuendelea kulinda amani na usalama wa raia kwa kuwa bila amani maendeleo hayawezi kupatikana.

Akizungumza kuhusu mradi wa vitambulisho vya taifa alieleza kushangazwa na mbunge aliyehoji kutengewa Sh300bilioni akisema kuwa mradi huo una faida kubwa katika suala zima la ulinzi na usalama kwa kuwa utawezesha kuwatambua Watanzania na wageni wanaoingia nchini kwa nia mbaya.

Hata hivyo alifafanua kuwa si kwamba fedha hizo zitatolewa kwa wakati mmoja, bali ni katika kipindi cha miaka mitano.

Mazungumzo ya Wizara na Kampuni ya Barrick

Kampuni ya Barick inayomiliki Mgodi wa Madini Nyamongo imekubali kutoa mrabaha wa asilimia moja ya faida yake ya madini yanayouzwa pamoja na Dola za Marekani 100,000 kwa vijiji saba vinavyozunguka mgodi huo kwa ajili ya shughuli za maendeleo ya wananchi.

Pia kampuni hiyo imekubali kutenga Dola 4.5milioni kwa ajili ya kuwaendeleza wachimbaji wadogo katika mgodi huo ambazo zitatumika kwa ajili ya kununulia vifaa vya kisasa ikiwa ni pamoja na kuwajengea uwezo wa kitaalamu katika shughuli zao.

Kampuni hiyo imekubali kutenga fedha hizo yakiwa ni makubaliano yaliyofikiwa katika mazungumzo baina yake na Waziri Nahodha alipofanya ziara katika mgodi huo kutokana na mgogoro ulipo baina ya kampuni hiyo na wananchi.
 
Mi naona huyu mjinga mjinga aliyewaua ndg ze2 na bado akaachiwa huru ingali kifungo cha maisha kikiwa wazi akaachiwa na chama cha magamba, sasa naona anataka kurudi gezerezani na miguu yake miwili akafie huko. Yeye anafikiri ndg ze2 aliyewaua tumewasahau,hakika hawaja2toka lakini naona ana2kumbusha aliyo2tendeya. Mi naona atafika patamu sasa kwani atakuwa gereza anajitafutia mwenyewe. Tusubirie na 2taona hakika!
 
Kishongo ni kubwa jinga siku zote... Kama kishongo wewe ni me basi ni lazima utakuwa sio riziki manake unavyowashwaga..kama ni ke basi wewe ni muuza kuku!
 
Jipe moyo, lakini ukweli ni kwamba Mhe Lema anaonekana kukosa raha tangu Zombe aanze kumtaja juu ya uhalifu wake wa zamani. Ni kama kutonesha kidonda, alidhania hayo mambo hayataibuka na sasa rekodi zake za kihalifu ambazo zipo hata mahakamani zitakapowekwa hadharani zitasababisha kifo chake kisiasa.<br />
Anavuna alichopanda.
<br />
<br />
hii yote ni kutokana na viapo vya kijuha, kumbuka ulipoapa na kusema; naapa naahidi mbele ya chama, mapinduzi nitakulinda mpaka kufa. hangaika weeee! lakini hamtoki kifikra wala kimkakati, mmefeli.
 
Kishongo ni kubwa jinga siku zote... Kama kishongo wewe ni me basi ni lazima utakuwa sio riziki manake unavyowashwaga..kama ni ke basi wewe ni muuza kuku!

Acha kuvuta bangi....haya ndiyo madhara yake kwako.....kubwabwaja hovyo.
 
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha amehoji kwa nini aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam (RCO), Kamishna Msaidizi wa Polisi(ACP), Abdallah Zombe hakutoa mapema taarifa za uhalifu zinazomhusisha Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.<br />
<br />
Alikuwa akijibu swali kuhusu hatua ambazo jeshi hilo limezichukua dhidi ya Lema kuhusiana na tuhuma hizo ofisini kwake, Dar es Salaam jana alipokutana na waandishi wa habari kuzungumzia mafanikio ya wizara hiyo katika kipindi cha miaka 50 ya uhuru na changamoto zinazoikabili. Hata hivyo, alilitaka jeshi hilo kutokuzipuuza taarifa hizo.<br />
<br />
Aliwaagiza maofisa wa jeshi hilo kupitia kwa Kamishna wa Polisi Utawala na Fedha, Clodwig Mtweve kumuita Zombe na kumwuliza juu ya tuhuma hizo na kuzifanyia kazi.<br />
<br />
“Sisi tunasema kwa kila taarifa inayotolewa inakuwa na chembe ya ukweli. Labda niwape mfano mmoja, nitatumia mfano mbaya kidogo... ukikutana na mlevi akakwambia kuwa katika njia hii kuna majambazi japo ni mlevi lazima utakimbia kupitia njia nyingine;<br />
Kwa hiyo hata hizi taarifa za Zombe hatupaswi kuzipuuzia kwani hawezi mtu mzima kusimama na kutoa taarifa kama zile hadharani hivihivi tu. Kwa hiyo maofisa wa jeshi nendeni mkae naye muulize maana inaonekana ana taarifa nyingi.”<br />
<br />
Agosti Mosi mwaka huu, Zombe alimhumu Lema kuwa alikuwa na mtandao wa uhalifu wa wizi wa magari akidai kwamba anao ushahidi wa tuhuma hizo kwa kuwa alipokea taarifa hizo wakati akiwa RCO Dar es Salaam ambazo alidai kuwa alikuwa ameshaanza kuzifanyia kazi kabla ya kukamatwa na kuwekwa ndani kwa tuhuma za mauaji.<br />
<br />
Source: Gazeti Mwananchi.<br />
<br />
<b><u>My Comment</u></b>: Muda si mrefu rangi halisi za huyu mbunge zitakuwa hadharani. <br />
Waliopoteza kura zao kumchagua imekula kwao.
<br />



Sikujua kama Nahodha ni Mgonjwa kichwani,Hauwezi kusema kila tuhuma ina chembe ya ukweli,ths is bullshit,kwani hakuna Mashtaka ya Uongo duniani?

Mm nikisema yeye Nahodha katika Ujana wake alishawahi kuwa Shoga tuseme hapa kuwa kwamba kuna chembe ya ukweli kwa sababu tu ni Mashtaka?

Yeye angesema tunafanyia kazi tuhuma hizo kubaini kama zina Ukweli au la lakini he shudnt not have preconceived assumptions!!
Na kama hivyo ndivyo,basi wafanyie kazi tuhuma zingine nzito na waanze kuzungumzia wizi wa Shimbo!!
<br />
 
uchunguzi ufanyike haraka iwezekanavyo
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha amehoji kwa nini aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam (RCO), Kamishna Msaidizi wa Polisi(ACP), Abdallah Zombe hakutoa mapema taarifa za uhalifu zinazomhusisha Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.

Alikuwa akijibu swali kuhusu hatua ambazo jeshi hilo limezichukua dhidi ya Lema kuhusiana na tuhuma hizo ofisini kwake, Dar es Salaam jana alipokutana na waandishi wa habari kuzungumzia mafanikio ya wizara hiyo katika kipindi cha miaka 50 ya uhuru na changamoto zinazoikabili. Hata hivyo, alilitaka jeshi hilo kutokuzipuuza taarifa hizo.

Aliwaagiza maofisa wa jeshi hilo kupitia kwa Kamishna wa Polisi Utawala na Fedha, Clodwig Mtweve kumuita Zombe na kumwuliza juu ya tuhuma hizo na kuzifanyia kazi.

“Sisi tunasema kwa kila taarifa inayotolewa inakuwa na chembe ya ukweli. Labda niwape mfano mmoja, nitatumia mfano mbaya kidogo... ukikutana na mlevi akakwambia kuwa katika njia hii kuna majambazi japo ni mlevi lazima utakimbia kupitia njia nyingine;
Kwa hiyo hata hizi taarifa za Zombe hatupaswi kuzipuuzia kwani hawezi mtu mzima kusimama na kutoa taarifa kama zile hadharani hivihivi tu. Kwa hiyo maofisa wa jeshi nendeni mkae naye muulize maana inaonekana ana taarifa nyingi.”

Agosti Mosi mwaka huu, Zombe alimhumu Lema kuwa alikuwa na mtandao wa uhalifu wa wizi wa magari akidai kwamba anao ushahidi wa tuhuma hizo kwa kuwa alipokea taarifa hizo wakati akiwa RCO Dar es Salaam ambazo alidai kuwa alikuwa ameshaanza kuzifanyia kazi kabla ya kukamatwa na kuwekwa ndani kwa tuhuma za mauaji.

Source: Gazeti Mwananchi.

My Comment: Muda si mrefu rangi halisi za huyu mbunge zitakuwa hadharani.
Waliopoteza kura zao kumchagua imekula kwao.
 
Line up ya post hii na waungaji mkono wake ni dhahiri ni siasa za maji taka; kama siyo basi ni matokeo ya chama legelege kuongoza serikali legelege ikitetewa wa wachangiaji legelege humu. HAKUNA MAREFU YASIYO NA NCHA
 
Kama ni mwizi, sheria ichukue mkondo wake....kama ni mipango ya kumdhalilisha, shame on you!
 
Na tetesi za kwamba IGP aliyepita alikua na kikosi kazi cha majambazi zichunguzwe....na tetesi kwamba mtoto wa nanilii anauza dawa za kulevya zichunguzwe....na tetesi kwamba mbunge wa sasa wa Rorya ana kikosi kazi zichunguzwe....patam hapo!!
 
Ningekuwa mimi ndo serikali ningemkamata zombe na kumuweka ndani maana yeye alikuwa mtumishi wa jeshi hilo na kama alikuwa anajuwa hayo kwa nini hakuchukua hatua?
 
Angekuwa mbunge wa chama cha magamba asingechunguzwa. ya kwao yamewashinda ya kwetu wataweza?
 
Angekuwa mbunge wa chama cha magamba asingechunguzwa. ya kwao yamewashinda ya kwetu wataweza?/QUOTE]

Mh. Lema peke yake ndiye anayejua alichosema zombe kama ni ukweli au uongo. Humu ndani tutatukanana wee! lakini at the end of the day kama ni kweli itabakia hivyo na kama ni uongo utabakia kuwa uonngo!!......so lets wait who knows Mh. lema ataongea siku moja na tutajua msimamo wake!!!
 
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha amehoji kwa nini aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam (RCO), Kamishna Msaidizi wa Polisi(ACP), Abdallah Zombe hakutoa mapema taarifa za uhalifu zinazomhusisha Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.

Alikuwa akijibu swali kuhusu hatua ambazo jeshi hilo limezichukua dhidi ya Lema kuhusiana na tuhuma hizo ofisini kwake, Dar es Salaam jana alipokutana na waandishi wa habari kuzungumzia mafanikio ya wizara hiyo katika kipindi cha miaka 50 ya uhuru na changamoto zinazoikabili. Hata hivyo, alilitaka jeshi hilo kutokuzipuuza taarifa hizo.

Aliwaagiza maofisa wa jeshi hilo kupitia kwa Kamishna wa Polisi Utawala na Fedha, Clodwig Mtweve kumuita Zombe na kumwuliza juu ya tuhuma hizo na kuzifanyia kazi.

"Sisi tunasema kwa kila taarifa inayotolewa inakuwa na chembe ya ukweli. Labda niwape mfano mmoja, nitatumia mfano mbaya kidogo... ukikutana na mlevi akakwambia kuwa katika njia hii kuna majambazi japo ni mlevi lazima utakimbia kupitia njia nyingine;
Kwa hiyo hata hizi taarifa za Zombe hatupaswi kuzipuuzia kwani hawezi mtu mzima kusimama na kutoa taarifa kama zile hadharani hivihivi tu. Kwa hiyo maofisa wa jeshi nendeni mkae naye muulize maana inaonekana ana taarifa nyingi."

Agosti Mosi mwaka huu, Zombe alimhumu Lema kuwa alikuwa na mtandao wa uhalifu wa wizi wa magari akidai kwamba anao ushahidi wa tuhuma hizo kwa kuwa alipokea taarifa hizo wakati akiwa RCO Dar es Salaam ambazo alidai kuwa alikuwa ameshaanza kuzifanyia kazi kabla ya kukamatwa na kuwekwa ndani kwa tuhuma za mauaji.

Source: Gazeti Mwananchi.

My Comment: Muda si mrefu rangi halisi za huyu mbunge zitakuwa hadharani.
Waliopoteza kura zao kumchagua imekula kwao.






Kweli hii Tanzania sijui inakoelekea!
Yaani inavyoonekana hapo kwenye red ni kwamba Zombe ameanza kuwa mtaji wa serikali hahahaaa ila masikini hwajijui!!!
Kwanini hizo tuhuma hazikufanyiwa kazi siku zote hizo??? Au walkua wanashirikiana nae kuiba hayo magari?????
CCM wanatapatapa kama wafa maji........
Kumtumia Zombe kwa hilo ni kujimaliza kabsaa.
Zombe alieua watanzania wasio na hatia leo anakua mtaji wao!!???
Pole zao.........
 
WAZIRI wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Shamsi Vuai Nahodha amehoji kwa nini aliyekuwa Mkuu wa Upelelezi wa Mkoa wa Dar es Salaam (RCO), Kamishna Msaidizi wa Polisi(ACP), Abdallah Zombe hakutoa mapema taarifa za uhalifu zinazomhusisha Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema.

Alikuwa akijibu swali kuhusu hatua ambazo jeshi hilo limezichukua dhidi ya Lema kuhusiana na tuhuma hizo ofisini kwake, Dar es Salaam jana alipokutana na waandishi wa habari kuzungumzia mafanikio ya wizara hiyo katika kipindi cha miaka 50 ya uhuru na changamoto zinazoikabili. Hata hivyo, alilitaka jeshi hilo kutokuzipuuza taarifa hizo.

Aliwaagiza maofisa wa jeshi hilo kupitia kwa Kamishna wa Polisi Utawala na Fedha, Clodwig Mtweve kumuita Zombe na kumwuliza juu ya tuhuma hizo na kuzifanyia kazi.

“Sisi tunasema kwa kila taarifa inayotolewa inakuwa na chembe ya ukweli. Labda niwape mfano mmoja, nitatumia mfano mbaya kidogo... ukikutana na mlevi akakwambia kuwa katika njia hii kuna majambazi japo ni mlevi lazima utakimbia kupitia njia nyingine;
Kwa hiyo hata hizi taarifa za Zombe hatupaswi kuzipuuzia kwani hawezi mtu mzima kusimama na kutoa taarifa kama zile hadharani hivihivi tu. Kwa hiyo maofisa wa jeshi nendeni mkae naye muulize maana inaonekana ana taarifa nyingi.”

Agosti Mosi mwaka huu, Zombe alimhumu Lema kuwa alikuwa na mtandao wa uhalifu wa wizi wa magari akidai kwamba anao ushahidi wa tuhuma hizo kwa kuwa alipokea taarifa hizo wakati akiwa RCO Dar es Salaam ambazo alidai kuwa alikuwa ameshaanza kuzifanyia kazi kabla ya kukamatwa na kuwekwa ndani kwa tuhuma za mauaji.

Source: Gazeti Mwananchi.

My Comment: Muda si mrefu rangi halisi za huyu mbunge zitakuwa hadharani.
Waliopoteza kura zao kumchagua imekula kwao.






Kweli hii Tanzania sijui inakoelekea!
Yaani inavyoonekana hapo kwenye red ni kwamba Zombe ameanza kuwa mtaji wa serikali hahahaaa ila masikini hwajijui!!!
Kwanini hizo tuhuma hazikufanyiwa kazi siku zote hizo??? Au walkua wanashirikiana nae kuiba hayo magari?????
CCM wanatapatapa kama wafa maji........
Kumtumia Zombe kwa hilo ni kujimaliza kabsaa.
Zombe alieua watanzania wasio na hatia leo anakua mtaji wao!!???
Pole zao.........
 
Ni baada ya kuwachan bungeni. Watumie hoja si nguvu ya dola wajibu kwa hoja ya nguvu.! Lema hawamuwezi!
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom