Wakuletwa
Senior Member
- Oct 31, 2010
- 134
- 9
Salaam ndugu zangu, kuna utapeli umezuka kwenye huduma za benki hasa kwa wenye kutumia simu za mkononi kuhamisha au kupata huduma zozote za benki. Juzi nilikuwa NMB tawi la Morogoro road hapo Dar nilimuona dada mmoja akilalamika kuwa akaunti yake imekuwa ikihamishwa fedha na watu asiowajua. Ila chanzo kilikuwa hivi! Alipigiwa simu na watu waliojitambulisha kuwa ni watu wa benki na wanamtaka abadirishe namba yake ya siri anayotumia kwenye SIM bank kwani wanaboresha mfumo huo na alipofanya hivyo tu balaa likaanza kila akiweka hela akienda anakuta akaunti nyeupee yaani jamaa wanajichotea kama yao.
TAHADHARI usiweke wala kuandika popote namba yako ya siri ya benk weka kichwni kwako tu. Pia usikubali kuongea na yoyote kuhusu mambo yakibenki kupiatia simu. Ni bora uende benki mwenyewe.:target:
TAHADHARI usiweke wala kuandika popote namba yako ya siri ya benk weka kichwni kwako tu. Pia usikubali kuongea na yoyote kuhusu mambo yakibenki kupiatia simu. Ni bora uende benki mwenyewe.:target: