Wizi wa aluminium kwenye jimbo la Anne Kilango Malecela...

ngwendu

JF-Expert Member
Jun 7, 2010
1,964
174
Wadau kuna taarifa kuwa kuna mtu mmoja anaitwa willy akishirikiana na foreigners wanachimba na kusafirisha aluminium kwenda Kenya. Inavyojulikana serikalini ni kuwa huyu mtu anachimba chokaa kuipeleka kenya lakini kiuhalisia ni kuwa kwenye magari yake chokaa inawekwa juu tu kuficha kilichopo ndani. Tafadhali kama kuna mhusika au kuna mtu yuko karibu na wahusika basi taarifa hizi zifanyiwe kazi. Sehemu yenyewe ni huko Ndungu milimani mkoani Kilimanjaro kwenye jimbo la mheshimiwa Anne Malecela. Sorry kwa kuileta hii thread kwenye jukwaa la siasa. Lakini mimi nimeichukulia kama issue sensitive inayogusa moja kwa moja masilahi ya taifa letu.
 
Wakuu ni evidence gani mnataka tena. Nimesema kila siku magari yanapita kutoka ndungu milimani kwenda kenya yakiwa yamepakia alminium lakini juu yakiwa yamefunikwa na chokaa kama geresha. sasa ushahidi gani tena? assume mimi ni muajiriwa hapo. ningeadikaje? Na kwa nini niongope? kwa maslahi yapi? Nitafaidikaje?
Narudia tena kama kuna mtu ana-access na wahusika akiwemo Mh Anne Kilango Malecela basi wataarifiwe.
 
Una uhakika huko Kenya inayeyushwa kuwa Alluminium? nakama ni kweli ina maana seikali yetu haijui?huyu Ndg ninavyomfahamu anafanya biashara ya mabati Arusha na Moshi na mabati anayachukulia Dar sasa hiyo biashara ya Alluminium kwanini aipeleke Kenya awache Dar anakochukuia mabati.
 
Una uhakika huko Kenya inayeyushwa kuwa Alluminium? nakama ni kweli ina maana seikali yetu haijui?huyu Ndg ninavyomfahamu anafanya biashara ya mabati Arusha na Moshi na mabati anayachukulia Dar sasa hiyo biashara ya Alluminium kwanini aipeleke Kenya awache Dar anakochukuia mabati.
Mkuu we niamini. Narudia tena kwamba hii ni taarifa wala tusilete ushabiki wa kisiasa kwenye issue serious ya uporaji wa rasilimali zetu. Please kwa ambaye ana access na wahusika let them know it.
 
Huyu vipi? Anakj kushtaki hapa kwenye JF? Nilifikiri anatupa taarifa juu ya hatua alizo chukua, any way wadau ujumbe umefika tuufuatilie
 
Wadau kuna taarifa kuwa kuna mtu mmoja anaitwa willy akishirikiana na foreigners wanachimba na kusafirisha aluminium kwenda Kenya. Inavyojulikana serikalini ni kuwa huyu mtu anachimba chokaa kuipeleka kenya lakini kiuhalisia ni kuwa kwenye magari yake chokaa inawekwa juu tu kuficha kilichopo ndani. Tafadhali kama kuna mhusika au kuna mtu yuko karibu na wahusika basi taarifa hizi zifanyiwe kazi. Sehemu yenyewe ni huko Ndungu milimani mkoani Kilimanjaro kwenye jimbo la mheshimiwa Anne Malecela. Sorry kwa kuileta hii thread kwenye jukwaa la siasa. Lakini mimi nimeichukulia kama issue sensitive inayogusa moja kwa moja masilahi ya taifa letu.

Biashara ya UCHIMBAJI 'HARAMU' TANZANIA si jambo geni sana kwa baadhi ya maafisa wetu serikalini.

Kati ya machimbo hayo, uchimbaji wa URANIUM unaendelea na baadhi tu ya maafisa wetu wa pale TUME YA NUCLEAR pale Sayansi ndio wenye undani huo zaidi na ushiriki wa wataalam toka Iran.

Hadi sasa shughuli za MACHIMBO ya aina hiyo yanaendelea nchini maeneo 7 kwa madini mbali mbali na kufanywa SIRI KUBWA wenye mali tusijue.

Mara baada ya katiba mpya mengi tu ya uvunguni yanaanza kuanikwa mezani kwa faida ya Umma na ustawi mzuri wa taifa letu kwa ujumla wake.
 
JF mbona inakuwa hivi? Mtu kaleta taarifa nyie mnamletea siasa, ndio maana mgao wa umeme unatupiga na tupo kama mikondoo tu. Kama kuna waandishi wa habari inabidi wafuatilie na kulipeleka hili swala kwenye vyombo vya dola. Sasa kama huyu mleta taarifa anaishi milima ya upare let say myamba. Kule hakuna vituo vya polisi wewe unayemshauri aende kituo cha polisi si uende wewe? Kwani wewe sio mtanzania? Kama huna cha kuchangia basi changia kuhusu dowans huko na mgoa wa umeme

Ivuga na mtoa mada thanks a lot! Hivi JF tumekumbwa na nini mtu ameleta data tunamshushua sasa tunatakaje jamani? Mimi sijaenda huko lakini nimepigiwa simu na mtu anataka kukodi magari yangu kupeleka huo udongo kiwanda cha cement Nairobi. Kwa jinsi nilivyomhoji though ni kupitia kwa simu nahisi kuna mchezo mchafu unafanyika hapo kwa kweli. Hata kama ni chokaa I'm sure taratibu kibao zitakuwa hazifuatwi believe it or not. Mimi nitalifiatilia hili jambo kadiri nitakavyoweza then nitaleta feedback.
 
Ivuga na mtoa mada thanks a lot! Hivi JF tumekumbwa na nini mtu ameleta data tunamshushua sasa tunatakaje jamani? Mimi sijaenda huko lakini nimepigiwa simu na mtu anataka kukodi magari yangu kupeleka huo udongo kiwanda cha cement Nairobi. Kwa jinsi nilivyomhoji though ni kupitia kwa simu nahisi kuna mchezo mchafu unafanyika hapo kwa kweli. Hata kama ni chokaa I'm sure taratibu kibao zitakuwa hazifuatwi believe it or not. Mimi nitalifiatilia hili jambo kadiri nitakavyoweza then nitaleta feedback.

Ndugu zangu Wa-Tanzania KWA KUDAI EVIDENCE wakati mji unahamishwa?? Kwani na Tanzanite kuibukia Kenya kuongoza kwa export yake ilhali yapatikana Tanzania tu nako mliletewa evidence sio????????
 
Wadau kuna taarifa kuwa kuna mtu mmoja anaitwa willy akishirikiana na foreigners wanachimba na kusafirisha aluminium kwenda Kenya. Inavyojulikana serikalini ni kuwa huyu mtu anachimba chokaa kuipeleka kenya lakini kiuhalisia ni kuwa kwenye magari yake chokaa inawekwa juu tu kuficha kilichopo ndani. Tafadhali kama kuna mhusika au kuna mtu yuko karibu na wahusika basi taarifa hizi zifanyiwe kazi. Sehemu yenyewe ni huko Ndungu milimani mkoani Kilimanjaro kwenye jimbo la mheshimiwa Anne Malecela. Sorry kwa kuileta hii thread kwenye jukwaa la siasa. Lakini mimi nimeichukulia kama issue sensitive inayogusa moja kwa moja masilahi ya taifa letu.
Mkuu kama utaweza kunipatia jina la pili la huyo Willy, itakuwa rahisi kulifutilia?
 
..suala hili linajulikana tayari. labda hatua ndiyo hazijachukuliwa.

..majuzi nimesikia Waziri Maige kamtimua afisa misitu wa wilaya.

..labda kilio hiki kipelekwe kwa Waziri mapema kabla hajaijua fedha na kuzama kwenye ufisadi.

Shadrack Sagati said:
Biashara ya udongo mwekundu yaangamiza msitu Shengena

Safari yangu ya kuufikia msitu Shengena haikuwa rahisi. Baada ya kuondoka Dar es Salaama nilielekezwa nishuke katika Mji wa Same nisubiri basi linalotoka Moshi kuelekea katika Kata ya Chome. Kwa wanaoifahamu Chome waliniambia kuwa basi hilo linafika Same saa 8 na linaondoka saa 9 alasiri. Siku hiyo niliondoka mapema Dar es Salaam ili saa nane niwe nimeshafika Same.

Mkosi wa safari yangu ulianzia Ubungo, nilipanga nipande basi liendalo kasi kuliko mabasi mengine yaendayo Arusha na Moshi yaani Buffalo, lakini nikachelewa. Akili yangu ikanituma nipande Ngorika nayo nikakuta imejaa. Hata hivyo basi nililopanda la Shabaha halikuniangusha maana nilifika saa 6.30 mchana pale Same. Na kwa vile mwenyeji wangu alishaniambia kuwa gari linafika pale saa nane sikuwa na wasiwasi zaidi ya kufika na kwenda mahali angalau kupata chochote cha tumboni.

Ilipotimu saa 7.30 nilijongea kwenye kituo cha basi nilichoelekezwa na mhudumu wa hoteli niliyopata chakula. Kwa mbali niliona basi likiwa kituoni hapo, nikafurahi kwamba nimeliwahi, lakini kuulizia kama linaenda Chome nikajibiwa kuwa basi la Chome limeshaondoka.

“Limeondoka kama dakika 10 hivi,” alinijibu dada mmoja anayefanya kwenye duka moja la karibu na kituo hicho cha mabasi. Niliishiwa nguvu iweje basi hilo lisiende na ratiba yake kama ilivyo siku zingine. Nikapata jibu kuwa siku hiyo lilikuwa na abiria wengi kwani lilijazwa na wanafunzi wa moja ya sekondari zilizoko huko Chome. Sikupanga kulala Same hivyo nililazimika kutafuta usafiri mwingine wa kuondoka katika mji huo.

“Hapa hakuna njia ni lazima ulale, hata kama ukichukua gari ndogo kule Chome ni milima ni vigumu kufika, labda chukua pikipiki ilifukuze hilo basi unaweza kulikuta pale Shamba. Nilikodi pikipiki ili ilifukuze hilo basi njia sio nzuri sana, ila katika shida, hakukuwa na namna. Bahati nzuri tulilikuta basi lenyewe njia panda ya Shamba likiwa linajiandaa kupanda Chome. Maeneo ya Chome nimekuwa nayasikia kutokana na kuwa na rafiki zangu kadhaa wanaotoka maeneo hayo

Lakini picha niliyoikuta kule sikuamini kama niko Upareni. Madhari ya kijani ndiyo ninayoiona, lakini Chome yenye vijiji vitatu vilivyoungana naiona kama bakuli kama ilivyo Ngorongoro Crater. Imezungukwa na milima huku chemichem cha maji zikimiminika kutoka milimani.

Ni umbali wa kilometa 46 kutoka Same kufika Chome moja ya vijiji vinavyounda Kata ya Chome. Nilifika jioni na kushukia katika kijiji hicho, sikupata shida kuwapata wenyeji wangu. Kwa vile katika eneo hilo hakuna nyumba ya kulala wageni nililazimika kulala kwenye nyumba ya mtu.

Sikuhisi tofauti kwani nilijiona kama nimewatembelea ndugu zangu kwa wema niliofanyiwa na mwenyeji wangu huyu aliyejitambulisha kwangu kwa jina la Sylvester. Ila muda wa jioni ilikuwa shida kwangu kutokana na hali ya hewa kugeuka na kuwa baridi kali. Sikujiandaa kwa hali ya hewa ya namna ile, nilijua Upareni ni joto.

Wenyeweji wangu niliokuwa nazungumza nao ile jioni waligundua hiyo hali hivyo wakanipatia nguo nzito za kujikinga na hiyo baridi. Kesho yake ilikuwa ni siku ya kupanda Mlima Shengena kuelekea kwenye Hifadhi ya Msitu wa Shengena. Nilienda huko kujionea namna msitu huo ulivyovamiwa na wachimbaji wadogo wa dhahabu. Wenyeji wangu walinionya kuwa ni kazi ya hatari “wale watu wako tayari kuua wakiona unafuatilia mambo yao, hivyo ukienda huko ni lazima uchukue tahadhari.”

Kesho yake saa moja asubuhi nilianza safari ya kwenda msitu Shengena. Niliambatana na wenyeji wangu wawili kwa ajili ya kunionyesha maeneo hayo yanayochimbwa dhahabu lakini pia kunikinga na hasira za wachimbaji hao. Kuupanda mlima huu kwa mwenyeji ni nusu saa, lakini kwangu mimi ilinichukua saa moja na robo hadi kufika kileleni.

Katika kilele cha mlima huu kuna tambarare yenye udongo mwekundu maarufu kama boxide ambao nao unawindwa na wafanyabiashara. Hivyo kabla ya kuufikia msitu nilianza kushuhudia mashimo makubwa ambako udongo huu ambao kitaalamu unaitwa Bauxite unachimbwa. Lakini pia Kwa namna mazingira hayo yalivyoharibiwa, mwenyeji wangu Sylvester ananiambia kuwa biashara hiyo hainufaishi wana kijiji badala yake kuna baadhi ya viongozi ndio wanaofaidika. “Huu udongo unaochimbwa sisi wanakijiji hatufaidiki kwa chochote, ila viongozi wetu ndio wanaojua biashara hii,” anasema Sylvester.

Sylvester anasema maeneo hayo yanayopakana na misitu yalitunzwa vizuri na wazee wa eneo hilo ili kulinda uoto wa asili. Lakini kwa tamaa za viongozi wamewaruhusu wafanyabiashara kuchimba mchanga huo kwa ajili ya kwenda kuuza nchini Kenya. Kibaya zaidi anasema hata maeneo ambayo yanamilikiwa na baba yake aliyejitahidi kupanda miti, leo hii uongozi wa Kata ya Chome umetumia nguvu kumchanganya na kuwauzia wafanyabiashara hao.

“Nikilalamika mtendaji anasema yeye ndiye mwakilishi wa Rais, hivyo ardhi iko chini yake hivyo ana uwezo wa kuiuza kwa yeyote yule,” anasema Sylvester. Kauli hii ya Sylvester inanipa mawazo ya kumtafuta kiongozi wa Kata ya Chome ili wazungumzie biashara hii ya mchanga mwekundu kwa namna ambavyo wana kijiji wanavyofaidika.

Siku hii ya kwanza niliposhuka chini nilienda kumtafuta kwanza Diwani wa Kata ya Chome Amini Kalalu, ili aweze kuzungumzia biashara hii. Kalalu alipatikana na kukiri kuwapo biashara hiyo ya mchanga. “Ni kweli kule kuna wafanyabiashara wanachimba mchanga wanaupeleka nje ya nchi, sisi kama Kata hatupati fedha yoyote,” anasema Kalalu.

Kalalu anasema anayefahamu kwa undani kuhusu biashara hiyo ni mtendaji kata pamoja na viongozi wa vijiji vya kata hiyo ambao alisema ndio wanaohusika kuwauzia wafanyabiashara maeneo hayo. Anasema kuwa anazo taarifa kuwa kuna asilimia ya mapato yanayotokana na biashara hiyo yanaingizwa kwenye akaunti za vijiji lakini sio kata.

Diwani huyu anasema kuwa awali wakati wachimbaji hao wanaomba maeneo hayo waliahidi kufanya uchimbaji wa kitaalamu ili kutoathiri mazingira lakini wameshindwa kutimiza ahadi hiyo. “Mimi naona kama ni utapeli na sijui kama vijiji vinapata mapato yoyote,” anasema Kalalu na kuongeza kuwa biashara ya udongo mwekundu ni ya muda mrefu, lakini wananchi na vijiji hawapati faida yoyote.

Anasema “yawezekana biashara ya udongo huu inawaingizia watu fedha nyingi, hebu fikiria anakodi lori moja kwa Sh 140,000 kutoka hapa hadi Makanya, nadhani udongo huu una madini mengine ambayo sisi hatujayagundua. “Haiwezekani hawa watumie fedha nyingi kukodi magari kuja kuchukua mchanga huu, ni lazima itakuwa ni biashara inayolipa zaidi,” anasema diwani huyu ambaye anaonekana kutokuwa na habari na biashara hii ya mchanga.

Anapoulizwa kwa nini vijiji visiweke mageti ili angalau kila lori linalopita litozwe ushuru, diwani anasema ni wazo zuri kwani hadi sasa hawajui idadi ya malori inayokwenda katika mlima huo kusoma mchanga kwa siku. Naye Mtendaji wa Kata ya Chome, Togolani Kiondo anasema biashara ya mchanga huo ni miradi ya vijiji na watu binafsi. Anasema vijiji vinalipwa asilimia 20 ya mapato yanayotozwa na halmashauri.

Kiondo anasema biashara hiyo imeanza kukua lakini anadai hana taarifa kama imechangia uharibifu wa mazingira katika eneo la situ wa Shengena. Kauli yake kuwa ni mradi wa vijiji inakanushwa na Mwenyekiti wa Kijiji cha Marieni, Msafiri Mkodo ambaye anadai kuwa biashara hiyo awali ilikuwa imepangwa mapato yaingie kwenye vijiji, lakini hadi sasa vijiji havijanufaika.

Mwenyekiti huyu anasema anayesimamia mapato hayo ni Mtendaji wa Kata ambaye anatakiwa ajue idadi ya malori yanayongia Chome na kutoka ili aweze kudhibiti ushuru. “Hata hao wafanyabiashara wanajua ushuru wanatakiwa walipe ofisi ya Mtendaji Kata, lakini sisi vijiji hatujafaidika,” anasema Mkodo. Mwenyekiti huyo anasema awali vijiji viliingia makubaliano na wafanyabiashara hao.

Na moja ya makubaliano ni watoe ajira kwa wakazi wa Chome na waimarishe usalama na amani kwa wananchi wanaozunguka eneo la machimbo. Sharti lingine ni huduma za afya ziwapo eneo la machimbo kama vyoo, elimu na watoe elimu kuhusu Ukimwi na kipindupindu. Anasema makubaliano mengine ni mwekezaji achangie sehemu ya pato lake kwa kupeleka maendeleo katika Kata ya Chome kama ujenzi wa barabara na shule.

Mkodo anaongeza kuwa makubaliano mengine ilikuwa ni mwekezaji afuate sheria zinazolinda mazingira na wapande miti sehemu ambazo wanachimba udongo huo. Pamoja na kuwapo makubaliano hayo, mwandishi alishuhudia maeneo hayo yakiwa na mashimo na hakuna miti yoyote inayopandwa. Kama hatua hazitachukuliwa kuzuia uchimbaji huu wa mchanga ni wazi kuwa msitu wa Shengena uko hatarini kutoweka.
 
..naona hapa mwandishi wa raia mwema naye anaripoti suala hilohilo.

..inaelekea watawala wamekuwa wazito kuchukua hatua.

Johnson Mbwambo/Raia Mwema said:
Mfano mwingine wa maamuzi mabovu ya watawala ni kuhujumiwa kwa milima ya Tao la Mashariki ambayo tunaambiwa kuwa katika Afrika milima ya aina hiyo inapatikana Cameroun tu. Milima hiyo ya Tao la Mashariki inajumuisha milima ya Uluguru (Morogoro), milima ya Usambara na Milima ya Pare.

Hujuma inayoendelea ni ya ukataji miti holela katika misitu ya milima hiyo kiasi kwamba milima hiyo ya aina yake duniani, na ambayo inaviumbe hai wengi (kama ndege) wasiopatikana kokote, itapoteza hadhi yake muda si mrefu.

Katika msitu wa Shengena wa milima ya Pare (kwa mfano), watawala wamewaruhusu wafanyabiashara kuvamia eneo la msitu na kuchimba udongo wa asili unaojulikana kitaalamu kama bouxite. Udongo huo ambao ni malighafi katika kutengeneza vyombo vya udongo, rangi za magari na vifaa vya umeme, husafirishwa kwenda Kenya. Zaidi ya tani 70 za udongo husafirishwa kwenda Kenya kila siku.

Watawala wameruhusu uchimbaji huo unaoteketeza msitu wa Shengena eti kwavile ni chanzo chao cha mapato! Katika wastani wa tani 70 za udongo zinazochimbwa kila siku, Halmashauri ya Wilaya ya Same huchukua asilimia 98 ya kodi na kijiji huambulia asilimia 2 tu.

Sina haja ya kusisitiza hapa kwamba kwa kasi hiyo ya uchimbaji huo, ulioanza mwaka 2007, muda si mrefu msitu wa Shengena utatoweka. Na tusisahau kuwa msitu huo ndiyo chimbuko la maporomoko ya maji ya pili kwa ukubwa barani Afrika (Thornton Falls) baada ya yale ya Victoria Falls ya Zimbabwe.
 
Wana JF habari hizo tusizipuuzie kwani zinawafaidisha jirani zetu, huku Hombolo, Dodoma kuna kiwanda kinachotengeneza Wine na kilevi (alcohol) inayotoa Valuu inayonunuliwa na Konyagi.
Kinamilikiwa na viongozi waandamizi wazawa na hisa nyingine inamilikiwa na M-Italia ambaye naye anachimba madini na kuyapeleka nje, wote tunamuona na nyumba yake ipo mlangoni mwa Chuo cha Serikali za Mitaa cha Waziri Mkuu.
Tumenyamaza Je? tukashtaki wapi na Kituo cha POLISI kipo hapohapo ndege zinztua huko porini na kuondoka, anayebisha afike Hombolo.
Milima hiyo kwa nyuma yake (kaskazini, unapoelekea Wilaya ya Kondoa haohao wa-Italia wakishirikiana na wa-Korea wananunua madini wanayoyaita Granite (yana rangi ya kijani) wanachimbua bila woga na vitalu wamenunua ofisi za Madini Makao makuu hapa Dodoma
hivyo mdau ngwendu mwenye hii thread unaweza kukuta wanakibali kutoka Madini zaidi ya hapo tunaibiwa, kama vile Mpwapwa (dhahabu), Bahi (Uranium) Manyoni (dhahabu) WANAOHUSIKA TUOKOENI MADINI TUNAIBIWA KAMA BULYANKULU, MWADUI, MIRERANI NA KWINGINEKO
 
Wana JF habari hizo tusizipuuzie kwani zinawafaidisha jirani zetu, huku Hombolo, Dodoma kuna kiwanda kinachotengeneza Wine na kilevi (alcohol) inayotoa Valuu inayonunuliwa na Konyagi.
Kinamilikiwa na viongozi waandamizi wazawa na hisa nyingine inamilikiwa na M-Italia ambaye naye anachimba madini na kuyapeleka nje, wote tunamuona na nyumba yake ipo mlangoni mwa Chuo cha Serikali za Mitaa cha Waziri Mkuu.
Tumenyamaza Je? tukashtaki wapi na Kituo cha POLISI kipo hapohapo ndege zinztua huko porini na kuondoka, anayebisha afike Hombolo.
Milima hiyo kwa nyuma yake (kaskazini, unapoelekea Wilaya ya Kondoa haohao wa-Italia wakishirikiana na wa-Korea wananunua madini wanayoyaita Granite (yana rangi ya kijani) wanachimbua bila woga na vitalu wamenunua ofisi za Madini Makao makuu hapa Dodoma
hivyo mdau ngwendu mwenye hii thread unaweza kukuta wanakibali kutoka Madini zaidi ya hapo tunaibiwa, kama vile Mpwapwa (dhahabu), Bahi (Uranium) Manyoni (dhahabu) WANAOHUSIKA TUOKOENI MADINI TUNAIBIWA KAMA BULYANKULU, MWADUI, MIRERANI NA KWINGINEKO

Hao mnaowapigia kelele wachukue hatua hawana hata habari na wengine ndio wanashirikiana na hao wanaowabia madini/udongo wenu kama vipi chukueni hatua wenyewe..
 
Mkuu kama utaweza kunipatia jina la pili la huyo Willy, itakuwa rahisi kulifutilia?
Mkuu huyo mtu na project zake anajulikana kama Willy Enterprises. Kibali alichonacho ni cha kuchimba huo udongo kama walivyoandika wengine humu ndani, lakini kiuhalisia kinachosafirishwa ni Allminium, na hiyo wanapakia toka juu milimani halafu akishuka huku chini kidogo anaweka huo udongo kwa ajili ya kuficha kilichopo ndani. Nawafanyakazi wote wanajua hilo dili linalofanyika.
Kuhusi hizo habai za Dom, is so sad to me. Jamani wahusika wajibikeni, mbona uroho umezidi? Hivi jamani kwanza mnapata mishahara kwa kodi zetu sasa badala mtuhudumie nyinyi mnachofanya ni kutuibia? hivi nyinyi ni watu gani ambao hamridhiki? Hamna huruma na watanzania wenzeni ambao kupitia kwao ndo mnapata mishahara?
Issue hizi za kijinga mziache ama sivyo nyakati zitawaachisha.
 
Back
Top Bottom