OMBUDSMAN mtoto
Member
- Sep 28, 2012
- 87
- 32
Wakoloni walifukuzwa toka sehemu mbalimbali Afrika, lakini sasa wanaendelea kutuibia kwa mtindo wa ukoloni- mamboleo; ndivyo William Ngeleja anapanga kuendeleza wizi-mamboleo kupitia mikono michafu ya mkabila mwenza na rafiki wa karibu sana Mkurugenzi Mkuu wa Rubada, Aloyce Masanja.
Ngeleja amekuwa halali bali kuzunguka kwenye Ofisi za wakubwa na hatimaye mkataba umesainiwa na CEO wa Rubada ili kutekeleza Mradi wa kuzalisha umeme wa Stiegler's Gorge ambao feasibility study na business plan vinaonyesha giza totoro kwa siku za usoni!
Maswali
1. Kwa nini tujikite katika chanzo cha aina moja cha HEP kila siku ni vilio vya maji kukauka (ref. vyanzo vyote sita vya Bwawa la Mtera, Kidatu, Kihansi, New Pangani Falls, Bwawa la Nyumba ya Mungu na Hale) wakati tuna fursa za alternative energies kibao?
2. Kwa vile kuzalishwa umeme huo ni kupitia mradi wa gharama kubwa wa zaidi ya Bilioni 2 (USD) ni wazi hao Wawekezaji nao wataidai TANESCO na je hizo gharama kubwa sana hazitaishia kumfikia mtumiaji mwananchi aliyekwisha pigika na ugunu wa maisha?
3. Kama Ngeleja & Masanja wameahidiwa kukatiwa hisa katika mradi huo tunawezaje kuamini kuwa huu utakuwa mradi wa kuwakomboa watanzania tofauti na majenereta yanayoumiza Tanesco na nchi kwa ujumla?
Wezi sasa si lazima wawe mawaziri au makatibu wakuu au maCEO, tusipoangalia wanatuibia huku wakiwa mtaani kwa kuwazungukiwa MaCEO ofisini na vi-brief-case vyao!!
Tuupinge wizi mambo-leo kwa kudai tuone upembuzi yakinifu wa huu mradi toka asasi zinazoaminika na pia Taifa sasa liweke kipaumbele kwa vyazo vingine vya umeme (upepo, jua, makaa, gas n.k ) kuliko mambo ya kusubiri kuchungulia utabiri wa hali ya hewa, ngurumo, pepo za kusi na mvua za mtawanyiko ambazo hazileti mvua za masika na hivyo migao ya umeme kuwa moja ya tunu za kitaifa!!!
Ngeleja amekuwa halali bali kuzunguka kwenye Ofisi za wakubwa na hatimaye mkataba umesainiwa na CEO wa Rubada ili kutekeleza Mradi wa kuzalisha umeme wa Stiegler's Gorge ambao feasibility study na business plan vinaonyesha giza totoro kwa siku za usoni!
Maswali
1. Kwa nini tujikite katika chanzo cha aina moja cha HEP kila siku ni vilio vya maji kukauka (ref. vyanzo vyote sita vya Bwawa la Mtera, Kidatu, Kihansi, New Pangani Falls, Bwawa la Nyumba ya Mungu na Hale) wakati tuna fursa za alternative energies kibao?
2. Kwa vile kuzalishwa umeme huo ni kupitia mradi wa gharama kubwa wa zaidi ya Bilioni 2 (USD) ni wazi hao Wawekezaji nao wataidai TANESCO na je hizo gharama kubwa sana hazitaishia kumfikia mtumiaji mwananchi aliyekwisha pigika na ugunu wa maisha?
3. Kama Ngeleja & Masanja wameahidiwa kukatiwa hisa katika mradi huo tunawezaje kuamini kuwa huu utakuwa mradi wa kuwakomboa watanzania tofauti na majenereta yanayoumiza Tanesco na nchi kwa ujumla?
Wezi sasa si lazima wawe mawaziri au makatibu wakuu au maCEO, tusipoangalia wanatuibia huku wakiwa mtaani kwa kuwazungukiwa MaCEO ofisini na vi-brief-case vyao!!
Tuupinge wizi mambo-leo kwa kudai tuone upembuzi yakinifu wa huu mradi toka asasi zinazoaminika na pia Taifa sasa liweke kipaumbele kwa vyazo vingine vya umeme (upepo, jua, makaa, gas n.k ) kuliko mambo ya kusubiri kuchungulia utabiri wa hali ya hewa, ngurumo, pepo za kusi na mvua za mtawanyiko ambazo hazileti mvua za masika na hivyo migao ya umeme kuwa moja ya tunu za kitaifa!!!