Pablo
JF-Expert Member
- Apr 2, 2017
- 2,441
- 2,541
Wizi kupitia mitandao ya simu
========Sehemu ya tatu ( wakala wanavyoibiwa ===============
Habari zenu wadau. Kabla haujaendelea chini pitia uzi hapo juu kisha tusonge na hii sehemu ya tatu inayohusu mawakala wa tigo pesa, mpesa au airtel money wanavyoibiwa kizembe au kwa kutokuwa makini na kujikuta wakifunga biashara kwa kuibiwa mitaji yao.
Tusonge
Zipo njia nyingi lakini mbili ndo hutumika sana. Ya kwanza tu chukulie mfano mimi nipo Dar mbezi beach lakini nina mtu mwingine niliepanga nae kufanya wizi yeye yupo mbeya mathalani ninakuja kwenye kibanda chako nahitaji kutoa pesa million moja na laki mbili (1.2m) kabla cjaanza kutoa lazima nithibitishe kuwa pesa niitakayo inapatikana kwa kukuuliza na baada ya hapo nitaanza mchakato kwa kuchukua simu yangu mithili nafuata hatua ya kutoa pesa na wakati huo rafiki yangu aliepo mbeya naye anafuata mchakato wa kutoa pesa hyo hyo 1.2m kwa kuwa nimeshamtajia namba ya wakala niliepo. kwa kifupi mimi nipo pale kwaajiri ya kuchukua cash tuu lakini mtoaji yupo mbeya. Akishatoa pesa anantumia ile masage na nikiipokea namtaarifu wakala nimetoa 1.2m na jina lake la uwakala na namba namtajia pia, pasipo na shaka wakala atapokea masage na kuniuliza jina langu na ntamtajia na hata akihitaji sms ntamuonesha juu juu coz nimemtajia jina lake na kias cha pesa (ingawa mawakala wengi hawahitaji uthibitisho wa sms kwenye simu za wateja) baada ya kujiridhisha atanikabidhi pesa yangu nitaondoka zangu. Baada ya nusu saa yule rafiki wa mbeya atapiga simu huduma kwa wateja na kuomba arejeshewe 1.2m ametoa kwa wakala kimakosa, watoa huduma watamwambia asubiri 24hrs au hata 48hrs baada ya uchunguzi.
hapa ndo patamu teh teh teh !!!!!!!!.
uchunguzi unafanyika.
Mtoa huduma atampigia wakala husika na kumuuliza kuwa 1.2m ilitolewa kimakosa hivyo inarudishwa kwa muhusika , wakala atasema nimempa cash huyo mtu kwa kuwa alikuja hapa akatoa pesa nikampatia cash..!! Labda kwa wale msiojua kwa taarifa yenu ili pesa irudi kwa muhusika ni lazima location iangaliwe ndipo ujue nani mkweli kati ya wakala na mteja, mfano mzuri hapo juu ni kwamba alietoa pesa location yake ni mbeya na wakala location yake ni Dar kwa mantiki hiyo mtoa pesa hakuwa kwa wakala wakati anatoa pesa so ni halali na kisheria ametoa pesa kimakosa, mtoa huduma atawaunganisha call conference wote wawili na kila mmoja atavutia upande wake lakini mwisho wa yote location ndio mwamuzi wa mwisho hivyo pesa itarudishwa kwa mteja kwa kuwa wakala huna ushahidi wa kutosha. Pole..!!
Kumbuka:
1. Kila wakala anawajibika kujaza logbook za miamala iliyofanyika kila siku na kitambulisho cha mteja kinatakiwa kabla hajapewa pesa
2. Kila wakala anawajibu wa kuchukua sms za miamala katika simu ya mteja na kujiridhisha uhalali wa muamala husika
Bahati mbaya siku hizi hii sector ya "mobile money" imekuwa kwa kasi kiasi kwamba sio rahisi kwa wakala kufanya yote hayo juu kwa kila mteja kwa kuhofia kupoteza wateja wengine kwa kukaa foreni wakisubiri huduma ama kwa uzembe /uvivu na kujikuta katika risk ya kupoteza pesa zao
My take:
kama una wakala au unatarajia kufanya biashara hii kuwa makini na fuata sheria na taratibu zinazotakiwa haswa kwenye miamala mikubwa ili kuokoa uhai wa biashara yako.
Na kama wewe umeona hii ni fursa ya kufanya fraud !! Cyo rahisi kama unavyofikilia(kwa wewe wa humu jf tu)
Submitted ..
.