Wizara ya Nishati: Hotuba ya bajeti kambi ya upinzani 2019/2020

bagamoyo

JF-Expert Member
Jan 14, 2010
21,291
24,171
May 26, 2019

Taarifa kwa Umma Hotuba itakayosomwa na kambi ya Upinzani Wizara ya Nishati
Hotuba ya Mh. John Mnyika waziri kivuli wizara ya Nishati bajeti 2019 / 2020 ikitangulia ile ya serikali ambayo wizara itaisoma May 28, 2019.

Ndani ya wizara ya Nishati kuna sekta muhimu tatu za Umeme, Gesi na Mafuta . Mh. John Mnyika mbunge wa Jimbo la Kibamba jijini Dar es Salaam, Tanzania kupitia CHADEMA akiwa waziri kivuli anasimamia wizara hiyo muhimu kabisa inayosimamia mradi wa bwawa la umeme wa Stiegler's Gorge , Gesi ya Mtwara na utafutaji Mafuta ya petroliamu


Source : Kwanza TV

Rasimu ya hotuba ya kambi ya upinzani kuhusu bajeti ya wizara ya Nishati anayoifafanua kwa umma wa waTanzania kupitia waandishi wa habari ina kurasa 80.

Hotuba ya kambi ya upinzani ktk kuiangazia Stiegler's Gorge ripoti za upembuzi yakinifu zilizopo serikalini zinaonesha mradi huo utachukua miaka 9 mpaka 12 kumalizika wakati awamu hii ya tano inadai itachukua miezi 36 yaani miaka 3 tu kukamilisha ujenzi kunako mwaka 2022. Kambi ya upinzani inataka watanzania waelezwe ni miujiza gani itatumika kukamilisha mradi huo ndani ya miaka 3 na wala siyo miaka 9 mpaka 12.

Maana gharama mtambuka za kweli ikiwa mradi utachukua miaka 9 hadi 12 kumalizika basi bajeti ya mradi huo mkubwa wa nguvu za umeme wa bwawa la maji unaweza kuitia matatani nchi kifedha.

Serikali kukosa fedha toka wadau wa maendeleo kutokana na mradi wa umeme wa bonde la Rufiji kutishia kuharibu ekolojia na mbuga kubwa ya wanyama ya Selous.

Mh. John Mnyika anamnukuu waziri wa serikali ya CCM kuwa Mradi wa umeme wa Rufiji (Stiegler's Gorge) tayari umepewa mabilioni ya shillingi.....

Kambi ya upinzani inataka serikali itoe maelezo kwanini mradi wa gesi umetoswa wakati uligharamiwa kwa dolari za kimarekani bilioni 2 kupitia mkopo kujenga bomba la gesi linalotumika kwa kiwango cha uwezo wa asilimia 6 tu ya uwezo wake wa kusafirisha gesi toka Mtwara hadi Dsm.
 
Uzinduzi Rufiji
Serikali imekabidhi rasmi eneo la mradi wa umeme wa maporomoko ya maji ya Mto Rufiji (RHPP), kwa mkandarasi Kampuni ya Arab Contractors kwa pamoja na ile ya Elsewedy Electric zote kutoka nchini Misri.

Hatua hiyo sasa inaashiria kuanza kwa kazi ya ujenzi wa mradi huo wa umeme ambao utazalisha Megawati 2,115 ambazo zitaingizwa kwenye dridi ya Taifa na kuifanya Tanzania kuwa na umeme mwingi na wa uhakika.

Akizungumza wakati wa kukabidhi mradi huo kwa mkandarasi katika hafla iliyofanyika ndani ya Pori la Akiba la Selous, Waziri wa Nishati, Dk. Medard Kalemani, amesema kuwa hatua hiyo inatokana na uamuzi wa Rais Dk. John Magufuli kwa kusimamia uamuzi wa ujenzi wa mradi huo mkubwa.

Alisema mradi huo ulibuniwa kwa muda mrefu tangu mwaka 1970 ambapo kazi ya uchambuzi ilifanyika lakini haukutekelezwa kwa sababu ya gharama zake kuwa kibwa.

"Wakati ule (1970), mahitaji ya umeme yalikuwa megawati 100. Lakini leo mahitaji ya umeme ni makubwa sana. Na ilipangwa kwa wakati ule kutekelezwa kwa awamu ambapo ungeanza na megawati 400, awamu ya pili 800 na baadaye megawati 900. Hatua tuliyofikia leo ndiko serikali ya awamu ya tano inataka ya Tanzania ya viwanda

"Huu ni mradi wa manufaa miji yote iliyozunguka mradi huu itakuwa kwa kasi sambamba na uzalishaji wa umeme," alisema

Waziri huyo wa Nishati, alisema kuwa mkandarasi Arab Contractors, atafanyakazi ya kujenga bwawa la umeme ikiwamo kingo za kuta pamoja na kujenga vituo ya kuzalisha umeme.

"Ninapenda mtekeleze mradi huu kwa wakati na kwa ufanisi ili kuondoa mashaka kwa watu ambao wenye shaka. Leo mnakabidhiwa eneo la kazi ni matumaini yetu itaifanyakazi hii kwa wakati ili wananchi waweze kunufaika na umeme.

"Na kuanzia leo (jana) wakandarasi msiondoke site nyumba zipo, miundombinu ipo iwe jua, mvua jengeni mradi wakati wote na msiondoke hapa," alisema

Alisema pia kitajengwa kituo cha kupoza na kukuza umeme cha kV 400 na njia za kusafirisha umeme kwa msongo wa kV 400 kutoka eneo la mradi hadi Chalinze kwenda Dodoma na Dar es Salaam na utakamilika mwaka 2022.
Source : http://www.tanesco.co.tz/index.php/...o-la-mradi-wa-umeme-mto-rufiji-kwa-mkandarasi
 
May 15 , 2019
''Power to the people" interview with Dr. Kalemani minister of Energy. They (Tanzania) have one of the largest Natural gas, helium and Uranium deposits in the world. The goal is to make cheap energy available to their people so that they can facilitate rapid economic growth.

Source : Dr. Mumbi show
 
Elekea ripoti ya upembuzi yakinifu iliyonayo kambi rasmi ya upinzani ni ile ya mwaka 1970. Miaka hiyo technologia ilikuwa ipo chini. Kwa jinsi technologia ilivyopiga hatua kwa dunia ya sasa sishangai ikisemekana mradi utakamilika ndani ya miaka mitatu. Jamani wenzetu wanafikiria usiku na mchana kufanya kazi kwa mda mfupi na yenye ufanisi.
Sasa hivi nipo seblen naangalia mbio za langalanga. Najiuliza inakuwaje matairi mane ya gari yanabadilishwa ndani ya sekunde mbili. Katika hali ya kawaida ni Maajabu. Ndio maana inabidi tusubiri kazi ifanyike.
 
Mh. John John Mnyika (MB) CHADEMA ameishauri Serikali kuandaa jukwaa la mjadala wa kitaifa ili kuwapatia wananchi fursa ya kutosha kuihakiki serikali waliyoichagua katika utekelezaji wa miradi Stiegler's Gorge, Gesi na Mafuta kwa ajili ya nishati


Source : Millard Ayo
 
January 18, 2019
Bonn, Germany
Bunge la Ujerumani limepitisha mswada wa kuitaka serikali ya Ujerumani itafute njia mbadala ya mradi wa Tanzania wa kuzalisha nishati ya umeme kwenye bonde la Stiegler ili kulinda turathi na asili.
Vyama vilivyomo katika serikali ya mseto ya Ujerumani vimeitaka serikali itafute njia nyingine badala ya ile ya mradi wa kuzalisha nishati ya umeme kwenye bonde la Stiegler kwenye mto rufiji kusini mwa Tanzania Wabunge wa vyama vya CDU/CSU, Kijani na AFD walishiriki katika kupiga kura hiyo lakini chama cha mrengo mkali wa kulia cha AfD, hakikushiriki. Azimio la vyama vya CDU,CSU na SPD pia linatokana na mapendekezo ya kamati ya serikali ya Ujerumani ya ushirikiano wa kiuchumi.

Azimio lililopitishwa bungeni na vyama hiyvo vilivyomo katika serikali ya mseto ya Ujerumani linaitaka serikali kuu isaidie katika masuluhisho ya kukidhi mahitaji ya nishati ya Tanzania bila ya kuathiri mazingira. Katika azimio lao vyama hivyo vimesema mradi huo mkubwa wa kuzalisha nishati ya umeme utavuruga mfumo wa mto mmojawapo mkubwa barani Afrika.

Tanzania inakusudia kujenga bwawa kubwa la kuzalisha nishati ya umeme kwa kutumia nguvu ya maji kutoka kwenye mto rufiji. Sehemu hiyo ni muhimu kwa shughuli za kilimo za wakaazi. Ikiwa mradi huo utaendelea mbele bonde la Stiegler ambalo limewekwa miongoni mwa turathi za shirika la Umoja wa mataifa la UNESCO litapoteza hadhi yake na huenda likasababisha athari kubwa katika raslimali zilizopo kwenye sehemu hiyo.
Source: dw.com
 
Bunge la Ujerumani hahahah...

Hivi watarudisha lini Mjusi wetu anayewaingizia mamilioni kule Berlin, tungependa tujenge jumba la maonyesho ya wanyama wetu pale Stieglers :)
January 18, 2019
Bonn, Germany
Bunge la Ujerumani limepitisha mswada wa kuitaka serikali ya Ujerumani itafute njia mbadala ya mradi wa Tanzania wa kuzalisha nishati ya umeme kwenye bonde la Stiegler ili kulinda turathi na asili.
Vyama vilivyomo katika serikali ya mseto ya Ujerumani vimeitaka serikali itafute njia nyingine badala ya ile ya mradi wa kuzalisha nishati ya umeme kwenye bonde la Stiegler kwenye mto rufiji kusini mwa Tanzania Wabunge wa vyama vya CDU/CSU, Kijani na AFD walishiriki katika kupiga kura hiyo lakini chama cha mrengo mkali wa kulia cha AfD, hakikushiriki. Azimio la vyama vya CDU,CSU na SPD pia linatokana na mapendekezo ya kamati ya serikali ya Ujerumani ya ushirikiano wa kiuchumi.

Azimio lililopitishwa bungeni na vyama hiyvo vilivyomo katika serikali ya mseto ya Ujerumani linaitaka serikali kuu isaidie katika masuluhisho ya kukidhi mahitaji ya nishati ya Tanzania bila ya kuathiri mazingira. Katika azimio lao vyama hivyo vimesema mradi huo mkubwa wa kuzalisha nishati ya umeme utavuruga mfumo wa mto mmojawapo mkubwa barani Afrika.

Tanzania inakusudia kujenga bwawa kubwa la kuzalisha nishati ya umeme kwa kutumia nguvu ya maji kutoka kwenye mto rufiji. Sehemu hiyo ni muhimu kwa shughuli za kilimo za wakaazi. Ikiwa mradi huo utaendelea mbele bonde la Stiegler ambalo limewekwa miongoni mwa turathi za shirika la Umoja wa mataifa la UNESCO litapoteza hadhi yake na huenda likasababisha athari kubwa katika raslimali zilizopo kwenye sehemu hiyo.
Source: dw.com
 
May 28, 2019
Dodoma, Tanzania

HOTUBA YA WAZIRI WA NISHATI MH. MEDARD KALEMANI : AOMBA TRILIONI 2.1 KWA AJILI YA BAJETI YA WIZARA



Source: GLOBAL TV ONLINE

Mheshimiwa Spika hadi kufikia tarehe 15 Mei, 2019 Wizara ilikuwa imepokea jumla ya Shilingi Trilioni 1.227. Fedha hizi zinajumuisha Shilingi bilioni 688.65 ambazo ni malipo ya awali (advance payment) kwa Mkandarasi wa ujenzi wa Mradi wa kuzalisha umeme wa Rufiji na Shilingi bilioni 169.71 ambazo ni fedha za nje zilizopelekwa moja kwa moja (D-Funds) katika miradi ya REA, TANESCO na Sustainable Energy for All (SE4All). Kiasi hicho kilichopokelewa na Wizara ni sawa na asilimia 87 ya fedha zilizotarajiwa kupokelewa katika kipindi husika ambazo ni Shilingi trilioni 1.410.

164. Mheshimiwa Spika, Bajeti ya Mwaka 2019/20 inalenga kutekeleza dhamira ya Serikali ya kuhakikisha kuwa inazalisha umeme wa kutosha, wa uhakika, unaotabirika na wenye gharama nafuu. Vilevile, bajeti imelenga kuimarisha shughuli za utafutaji na biashara ya mafuta na gesi asilia pamoja na kuwezesha wananchi kunufaika na rasilimali hizo. Lengo ni kuiwezesha Serikali kufikia azma ya kujenga uchumi wa viwanda na kufikia uchumi wa kati ifikapo mwaka 2025. 165. Mheshimiwa Spika, katika Mwaka 2019/20, Wizara ya Nishati inakadiria kutumia jumla ya Shilingi trilioni 2.142 ikilinganishwa na Shilingi trilioni 1.692 iliyotengwa kwa Mwaka 2018/19, sawa na ongezeko la asilimia 26.6. Ongezeko hili limetokana na kuanza kutekelezwa kwa mradi mkubwa wa Rufiji utakaozalisha MW 2,115.
166. Mheshimiwa Spika, fedha nyingi za ndani za miradi ya maendeleo zilizotengwa kwa mwaka 2019/20 zimeelekezwa katika miradi mitatu (3) ya kimkakati ambazo ni
117
Shilingi trilioni 1.86, sawa na asilimia 95.1 ya Bajeti yote ya Ndani. Miradi hiyo ni: Mradi wa Kuzalisha Umeme katika Mto Rufiji, MW 2,115 (Shilingi trilioni 1.44); Mradi Kabambe wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu (Shilingi bilioni 363.11); na Mradi wa Kuzalisha Umeme wa Kinyerezi I Extension MW 185 (Shilingi bilioni 60). 167. Mheshimiwa Spika, naomba kutoa hoja kwamba Bunge lako Tukufu sasa liidhinishe bajeti ya jumla ya Shilingi 2,142,793,309,000 kwa ajili ya matumizi ya Wizara ya Nishati na Taasisi zake. Mchanganuo wa fedha hizo ni kama ifuatavyo: (i) Shilingi 2,116,454,000,000 sawa na asilimia 98.8 kwa ajili ya Miradi ya Maendeleo. Kati ya fedha hizo za maendeleo, Shilingi 1,956,372,000,000 ni fedha za ndani na Shilingi 160,082,000,000 ni fedha za nje; na (ii) Shilingi 26,339,309,000 sawa na asilimia 1.2 kwa ajili ya Matumizi ya Kawaida. Kati ya fedha hizo Shilingi 15,025,821,000 kwa ajili ya Matumizi Mengineyo (OC) na Shilingi 11,313,488,000 kwa ajili ya mishahara (PE) ya watumishi wa Wizara na
118
Taasisi zilizo chini yake. 168. Mheshimiwa Spika, naomba tena nitoe shukrani zangu za dhati kwako na kwa Waheshimiwa Wabunge wote kwa kunisikiliza. Hotuba hii pia inapatikana katika Tovuti ya Wizara kwa anuani ya www.nishati.go.tz.
 
Charles Mwijage katika kuchangia hoja ya bajeti ya wizara ya Nishati, sekta ya mafuta inachangia asilimia 50 % TRA nini maana ya Energy / Power MIX, umeme utakaozalishwa na Stiegler's Gorge hauwezi kutosha , bomba la mafuta la Uganda....



Source: Millard Ayo
 
May 28, 2019
Dodoma, Tanzania
Stiegler's Gorge ,Two Other Projects To Gobble Up Sh. 1.9 Trillion in Tanzania's 2019 / 2020 budget
The Minister for Energy, Dr Medard Kalemani, asked the Parliament to approve a total of Sh2.142 trillion for his ministry for the financial year 2019/20 on Tuesday, May 28, 2019, saying 95.1 per cent of the cash will be spent on three strategic projects.
The amount sought for approval during the 2019/20 financial year is an increase from the Sh1.69 trillion that was endorsed during the 2018/19 budget.

The three strategic projects include: the Stiegler's Gorge Hydroelectric Dam, the third phase of the Rural
Electrification Agency (Rea) and extension of the Kinyerezi 1 gas-to-power project.

A joint venture, comprising Egyptian firms Arab Contractors and Elsewedy Electric, is currently building the $2.95 billion (Sh6.6 trillion) Stiegler's Gorge Hydroelectric Dam which will add a total of 2,100MW to the national grid upon completion.

Last month, the project received a boost when CRDB Bank Plc and United Bank for Africa (Tanzania) joined Africa Export-Import Bank (Afreximbank) and some Egyptian lenders to provide $737.5 million in bank guarantees to Tanzania Electric Supply Company (Tanesco), paving the way for the project execution.

And speaking in Parliament on Tuesday, Dr Kalemani said the three projects will consume Sh1.86 trillion in total during the coming financial year.

The breakdowns show that the Stiegler's Gorge Project will consume Sh1.44 trillion. The Rea project will cost Sh363.11 billion while the remaining Sh60 billion will be spent on Kinyerezi 1 Extension.

Dr Kalemani, who doubles as Member of Parliament (MP) for Chato, said in total Sh2.11 trillion will be spent as development expenditure during the coming financial year.

Out of the money, Sh1.95 trillion will be sourced locally while only Sh160 billion will come from foreign sources.
Only Sh26.33 billion, equivalent to 1.2 per cent of the budget will be for recurrent expenditure.
Source: http://www.ortakida.com.ng/Read.csh...r-projects-to-gobble-up-sh1-9-trillion-in-tan
 
Back
Top Bottom