Patriote
JF-Expert Member
- Jul 13, 2011
- 1,718
- 1,047
Wizara ya Maliasili na Utalii ingeweza kuleta ufanisi mkubwa sana unaoweza kuwainua Raia wa Tanzania na kuleta unafuu wa maisha kwa watu wanaoishi pembezoni mwa maeneo ya hifadhi za wanyamapori na misitu ambao kwa sasa wanapata hasara badala ya faida. Fwatilia….
1.Sekta-Misitu
Tanzania ina ardhi yenye ukubwa wa 94.5 Milioni hekta, kati ya hizo 38 % sawa na 36 Milion hekta ni misitu na woodland. Misitu ipo katika makundi makuu mawili Reserved forests (12.5Milion hekta) na Unreseved forests (19 milion hekta) zilizobakia ni uoto wa woodland. Hadi mwaka 2006, deforestation rate ilikuwa ni hakta zaidi ya 130,000 hekta kwa mwaka, hii ni hatari. kwa rate hii miaka 100 ijayo misitu itakuwa ipo kwenye edge ya extinction.
Sekta hii imeshindwa kurealize na kuprovide benefit kwa watanzania kutokana na uvunaji holela wa misitu unaosababishwa largely na upungufu wa doria pamoja na RUSHWA ILIYOKITHIRI. Wafanyabiashara wakuu wa mbao au magogo ni either viongozi au ndugu za viongozi wanaotumia vyeo vyao/vya ndugu zao kulihujumu taifa. Ndugu zangu, biashara yoyote haramu haiwezi kufanywa na mtu wa kipato cha chini/ordinary citizen na ikafanikiwa. Ukiona biashara hiyo imefanikiwa jua kuna kigogo wa Taifa hili ndiye anayeisimamia Biashara hiyo.
Nini cha kufanya, kwanza kabisa ni kuhakikisha sera zetu za misitu zinaandaliwa in such a way that, wananchi wanaokaa maeneo yaliyojirani na misitu ndio wanakuwa wafaidika wakuu wa misitu hiyo kama vile ilivyo kwenye sera ya Madini ambapo vijiji husika vinapewa gawio. Inawezekana sasa hivi utaratibu huu umeandikwa kwenye sera zetu ila haufutwi. Kuna tafiti nyingi na takwimu za kisayansi zinazoweza kutumika kumconvince Rais kutekeleza mpango huu. Kwa kufanya hivyo naimani wananchi ndio watakuwa walinzi wakuu wa rasilimali hizi na hivyo kupunguza gharama za doria na enermity iliyopo kati ya serikali na wananchi wake.
Imagine katika kipindi kati ya mwaka 2003-2005, Takwimu za Tanzania zinaonesha kuwa Tanzania ilisafirisha jumla ya cubic meter za magogo 19,300 kwenda China. Katika kipindi hicho hicho, Takwimu za China zinaonyesha kuwa Waliingiza jumla ya cubic meter 108,505 toka Tanzania. Hii maana yake ni kwamba magogo ambayo yalisafirishwa kwenda China bila kuwepo kwenye Takwimu za Tanzania ni 89,189 cubic meter. Je ni fedha kiasi gani zimepotea hapo? Takwimu hizi zinapatikana TRAFFIC-Monitor wa Illegal Trade. Fedha hiyo ingetosha kujenga madarasa 10,000. Kikubwa kinachotakiwa kudhibiti hali hii ni kusisitiza uadilifu, kudeal na maofisa wala rushwa, kuweka system yenye uwazi na kusimamia kikamilifu rasilimali hii na kuwapa fursa wanavijiji kulinda na kufaidi matunda ya ulinzi. Aidha, wananchi wapate faida za misitu sio kwa kuwajengea tu social infrastructure bali wapate economic gains.
2. Payment for ecosystem services scheme
Hii ni mechanism inayowapa incentive wananchi wanaoishi maeneo ambayo yanatoa ecosystem services kama vyanzo vya maji, vyanzo vya oxygen na carbon sink etc. Scheme hii imeshauriwa na wanasayansi kuwa ni nzuri katika kuwapa motisha wananchi maskin wanaoishi maeneo yanye utajiri mkubwa wa misitu na vyanzo vya maji. Kwa mfano, serikali ina-institute utaratibu huu na kuwawezesha wananchi wanaoishi maeneo yenye utajiri mkubwa wa bioanuai kama wananchi wa matombo wanaokaa chanzo cha mtu Ruvu, mto ambao unawaweka mjini wakazi wa Dar Es Salaam na vitongoji vyake. Serikali ingetoa kauli tu kuwa katika bili za maji, kama ilivyoamua kuwa EWURA wapate asilimia flani, Mimi nadhani badala ya kuwapa EWURA hiyo asilimia, Fedha hiyo ingewaendea wananchi wa Matombo na vitongoji vyake ili kuwapa motisha wasimamie kikamilifu chanzo hicho cha mto ruvu (Kimboza Forest Reserve) na kuwatoa kwenye lindi la umaskani.
Ikumbukwe kuwa wananchi hawa wanakatazwa kulima kwenye milima uluguru kwa ajili ya kuilinda bioanuai, sasa kwanini Serikali isiwafkirie watu hawa kama ilivyowafkiria watu wa Geita na Nyamongo kwenye madini? Kama serikali ingefwata ushauri huu ambao wataalam wamekwisha uona unafaa, wananchi wangekuwa na ari ya uhifadhi na kila wilaya ingekuwa na chanzo cha mapato. Kuna ugumu gani kwa serikali kupitisha sera ya aina hii ili wananchi wafaidike? Mnafurahia nini kuona wananchi wanafedhaheka kwa dhiki kuu?
3.Sekta-Wanyamapori
Sekta hii inapotential kubwa sana ya kututoa hapa tulipo kwenye kuwa omba omba wa kwanza duniani hadi kuwa watoa misaada wakuu duniani. Rasilimali ya wanyamapori haiwasaidii wananchi zaidi ya kuwatia umaskini wananchi. Ni kweli ipo misaada wananchi wanapewa na TANAPA, NCAA na WD lakini misaada hii bado haijaweza kuwapa motisha ya kutosha wananchi kuwafanya waache ujangili na wasaidie uhifadhi. Sababu kubwa ya michango hiyo kuwa midogo inawezekana ni ufinyu wa budget za Mashirika hayo au ni uchezeaji wa hela zinazokusanywa na mashirika hayo.
a) Ufinyu wa fedha zinazokusanywa
Hili ni lakujitakia, Bei za wanyama wetu kupitia uwindaji wa kitalii ni ndogo sana. Bei hizi zimekuwa zikipandishwa kwa kuongeza kiasi kidogo sana kwa sababu ya Rushwa. Akitokea waziri anataka bei za wanyamapori wanaowindwa zipande, waziri huyo atapigwa vita na wala hatodumu kwenye wizara hii. Lakini tujiulize, je ni kwa faida ya nani bei hizi zipo chini? Wapo wawindaji wanaokubaliana na kupanda kwa bei kwa maana wanaona bei tunazowatoza ni dhuruma kwa wananchi wa Tanzania. Ila wapo wawekezaji ambao ukitangaza tu ongezeko la bei watatoa mlio kwa kigezo cha kumuumiza mzawa etc na mwisho wa siku bei hizo zitapanda kwa $5.
Huu ni unyonyaji/uhujumu uchumi. Hivi lengo la Tanzania ni kuua wanyama wengi na kupata fedha kidogo au ni kuwinda wanyama wachache na kupata fedha nyingi?? Tutapata hasara gani kama tukangeweka bei ya juu ili waje matycoon 50 tu kwa mwaka na tukapata hela ambazo zingelipwa na wawindaji wababaishaji 500 ndio tuzipate???Are we really for the quality experience kweli kama sera zetu zinavyotabanaisha???
Hapa pia vigogo wa Taifa hili ndio wameweka mizizi. Utaskia vitalu vya watu wa NEC-CCM, Watoto wa Kawawa, Mwinyi, Ndugu wa Mkapa, Sokoine, Ndugu wa flani na flani. Kwa hiyo kimsingi wanapokataa bei zisipande, wanaokwamisha haya ni viongozi wetu na si vinginevyo. Mimi nadhani wananchi tukomae kuliokoa Taifa hili mana viongozi wetu hawana nia njema, wapo kwa ajili ya maslahi yao na si vinginevyo.
Imagine bei ya Simba kwenye auction ya Safari Club International mwaka juzi ilikuwa ni $ 150,000 kuwinda South Africa. Simba wa Tanzania ana nini kinachompunguzia ubora hadi serikali isione hasara kumuuza kwa $ 4000???kwanini tembo wetu, chui wetu wauzwe kwa bei ya hasara kwenye uwindaji? Sisi tupandishe bei, wasipo kuja wanyama wetu wataendelea kuongezeka. After all, uwindaji ni mchezo wa matycoon wa nchi zilizoendelea, wao matycoon wanalipa hela nying sana kwa ma agent na kwa wenye makampuni ya uwindaji. Sisi kama taifa ndo tunaoingizwa mkenge na hawa wanaojiita outfitters ambao kimsingi ni familia za Kawawa, Sokoine, Mkapa na vigogo wengne , We unadhani kama hakuna wanachopata kwanini wamiliki wa vitalu ni wao wenyewe vigogo??? Si waachie wengine kama wao wanaona ni biashara ya hasara??Hatukatai wazawa kufanya biashara ya uwindaji, wafanye biashara kwa kufwata kanuni na kulpatia mapato stahili sio ujanja ujanja na kuwaibia watanzania kwa kukwepa kodi na kutumia majina yao kutunyonya. Wanaoongoza kuendesha seka ya Utalii South Africa ni wazawa ila wanalipa kodi zote stahiki na sio ujanja ujanja. Lakini pia wananchi tujiulize, Mbona kwenye madini Serikali inawapendelea zaidi wawekezaji kutoka nje???Iweje kwenye uwindaji neno uzawa ndo limesurface zaidi???Chanzo cha hizi double standards ni Rushwa tu na kutaka kumiliki rasilimali za nchi wao na familia zao.
Wataalam walipendekeza hunting blocks zitolewe kwa Auctioning, ili watu washindanishwe na anayetangaza dau kubwa apewe kitalu. Utaratibu huu ungeliingizia taifa fedha nyingi sana na kufanya tasnia ya uwindaji iwe juu. Lakini kwa kuwa vigogo ndio wanataka wamiliki vitalu hivyo kwa kulipa fedha kidogo wakaona utaratibu huu uachwe kwani walijua wangefanya auctioning, wasingepata vitalu hivi wananvyomiliki sasa hivi. Tulipoteza mapato mengi sana, wanaweka kigezo cha uzawa ili wao na familia zao wagawane rasilimali zetu kwa bei chee.Chukueni rasilimali zetu, fedha zetu na mapato yetu mtulipe. Haipo hivyo. Kampuni ya Kawawa ilinyimwa kitalu kwa kushindwa kulipa kodi na michango mingine katika uwindaji, wagawa Hunting blocks wakamnyima kawawa kitalu Maige akawapa kinyemela. Yaliyotokea wote mlisikia bungeni. Kampuni ya malagarasi inayomilikiwa na Dk. Leakey pia inaubabaishaji huo huo pamoja na nyingine nyingi za wazawa. Wanataka kuendesha biashara hizi, uwezo hawana, taratibu hawazifuati, wakinyimwa vigogo wana wakingia kifua wanawapa tena. Tutafika kweli??? Nchi hii sio yenu peke yenu jamani, tupo watanzania 40 milioni, hivyo mnavyoyafanya haya mjue mnawafanyia dhuruma watu milioni 40.
Kuna tatizo lingine kubwa sana kwenye viwanja vya kujenga mahoteli ndani ya mbuga zetu, Huko pia ndio kichekesho. Kwani mtu anapewa kiwanja bila kutoa tsh hata moja. Jamani hata shamba la huko Kazuramimba/Mbekenyela ni lazma utoe kiasi fulani. Iweje viwanja katika maeneo haya muhimu vitolewe bure????Kigogo anapewa kiwanja, then anaweza kumuuzia mtu mwingine kwa mamilioni au kumpangisha mwekezaji mwingine ndo aendeshe biashara. Akianza kuoperate ndio anaanza kulipa mapato ya serikali. System ya kukusanya mapato hayo ipo very porous na kuna alot of leakages za mapato ya serikali. Viwanja hivi pia vimegawiwa kwa vigogo wale wale, familia ya Meghji ni moja ya wanufaika. Hivi kwa nini utaratibu wa serikali usifwate katika kugawa viwanja hivi???kwann wasitangaze watu wakashindanishwa ili kupata mwekezaji bora na sio bora mwekezaji???Kwann tukubali wanufaika wa rasilimali za nchi yetu wawe ni watu hao hao wachache ilhali taifa linapata hasara na lina watu zaidi ya 40m ????
b) Uchezeaji wa fedha katika mashirika ya uhifadhi TANAPA, NCAA, WD/TWPF
Mashirika yanayosimamia uhifadhi yamekuwa yakifanya matumizi holela na ya anasa kanakwamba mashirika haya yanamilikiwa na nchi Tajiri sana. Ukiangalia taratibu za utendaji kazi wa mashirika haya utagundua kuwa almost chote wananchopata, wanakifaidi wenyewe. Kwa utaratibu huu hatuwezi kufika. Kama wale waliopo kwenye madini wakila chote, TRA wakila chote wanancho kusanya, bandari wakila chote hakika hatutofika. Kwa bahati mbaya serikali imekaa kimya ikiangalia haya yakitokea. Mali hizi ni zetu sote, wananofanya kazi ktk mashirika haya wanawawakilisha wananchi wengine walio maeneo mengine. Kila kinachokusanya, inapaswa kitumike wisely, after all mkumbuke biashara ya utalii ni fragile business hivyo sustainability yake bado ni questionable.
Utakuta Tanzania inapeleka maafisa 15 kwenye maonyesho ya utalii Marekani, Kati ya hao watu watano kutoka Bodi ya Utalii TTB (SHIRIKA LENYE DHAMANA KUTANGAZA UTALII TANZANIA) watu 10 Kutoka TANAPA, WD na NCAA. Hivi huu sio uchezeaji wa hela? Sio dublication ya efforts? Kwani TTB wanaenda kutangaza vivutio gani kama sio hifadhi za Taifa, Ngorongoro na game reserves/uwindaji??Kama vipi basi muende kwa rotation ili kupunguza lundo la watu huko nje.
Serikali inalifahamu hili ila inalifumbia macho, Ona budget za mashirika haya kwenye kusafiri nje ya nchi kwenye maonyesho ya utalii. Takwimu/Tafiti zinaonyesha watalii wanaokuja nchini hawaji kutokana na watangazaji hawa wa Tanzania, yaani sio matangazo au mahudhurio ya TTB/Tanapa/NCAA inayowafikia wateja huko nje, Wataje/watalii wengi wanapata information za Tanzania kupitia maagent wa kubwa wa utalii Duniani, TTB/TANAPA/NCAA wanajua hili ila ndo kwanza wanabeef up budget zao za kwenda kutangaza utalii nje ya nchi. Takwimu zingetumika kukataza wafujaji hawa wa nchi yetu kwenda kufanya shopping ulaya na kwingineko, at least ningeelewa kuwa watu hawa wanakwenda Training ya conservation genetics na masomo mengine ambayo technologia yake haijafika bado hapa nchin. Hali haipo hivyo. Ona budget za mashirika haya kwenye ununuzi wa magari ya kifahari.
Wakati Pinda anadanganya taifa kuwa atasitisha ununuzi wa mashangingi kwa viongozi wa serikali, Huko Tanapa Mkuu wa hifadhi anapewa shangingi, Huko ngorongoro mkuu wa kitengo anapewa V8. Hivi tutafika kweli kwa ulifist huu? Kwanini hizo hela tusizielekeze kwenye kupambana na ujangili ambao unacause additive mortailty to legal hunting? We need to change.
Naomba kwa leo niishie hapa, toa mchango wako wa nini kifanyike kwenye sekta hii ya maliasili ili wote tufaidi urithi huu tulioachiwa na mwenyezi mungu. Next time ntaiangalia sekta ua Utalii, katika wizara hii ya Maliasili
1.Sekta-Misitu
Tanzania ina ardhi yenye ukubwa wa 94.5 Milioni hekta, kati ya hizo 38 % sawa na 36 Milion hekta ni misitu na woodland. Misitu ipo katika makundi makuu mawili Reserved forests (12.5Milion hekta) na Unreseved forests (19 milion hekta) zilizobakia ni uoto wa woodland. Hadi mwaka 2006, deforestation rate ilikuwa ni hakta zaidi ya 130,000 hekta kwa mwaka, hii ni hatari. kwa rate hii miaka 100 ijayo misitu itakuwa ipo kwenye edge ya extinction.
Sekta hii imeshindwa kurealize na kuprovide benefit kwa watanzania kutokana na uvunaji holela wa misitu unaosababishwa largely na upungufu wa doria pamoja na RUSHWA ILIYOKITHIRI. Wafanyabiashara wakuu wa mbao au magogo ni either viongozi au ndugu za viongozi wanaotumia vyeo vyao/vya ndugu zao kulihujumu taifa. Ndugu zangu, biashara yoyote haramu haiwezi kufanywa na mtu wa kipato cha chini/ordinary citizen na ikafanikiwa. Ukiona biashara hiyo imefanikiwa jua kuna kigogo wa Taifa hili ndiye anayeisimamia Biashara hiyo.
Nini cha kufanya, kwanza kabisa ni kuhakikisha sera zetu za misitu zinaandaliwa in such a way that, wananchi wanaokaa maeneo yaliyojirani na misitu ndio wanakuwa wafaidika wakuu wa misitu hiyo kama vile ilivyo kwenye sera ya Madini ambapo vijiji husika vinapewa gawio. Inawezekana sasa hivi utaratibu huu umeandikwa kwenye sera zetu ila haufutwi. Kuna tafiti nyingi na takwimu za kisayansi zinazoweza kutumika kumconvince Rais kutekeleza mpango huu. Kwa kufanya hivyo naimani wananchi ndio watakuwa walinzi wakuu wa rasilimali hizi na hivyo kupunguza gharama za doria na enermity iliyopo kati ya serikali na wananchi wake.
Imagine katika kipindi kati ya mwaka 2003-2005, Takwimu za Tanzania zinaonesha kuwa Tanzania ilisafirisha jumla ya cubic meter za magogo 19,300 kwenda China. Katika kipindi hicho hicho, Takwimu za China zinaonyesha kuwa Waliingiza jumla ya cubic meter 108,505 toka Tanzania. Hii maana yake ni kwamba magogo ambayo yalisafirishwa kwenda China bila kuwepo kwenye Takwimu za Tanzania ni 89,189 cubic meter. Je ni fedha kiasi gani zimepotea hapo? Takwimu hizi zinapatikana TRAFFIC-Monitor wa Illegal Trade. Fedha hiyo ingetosha kujenga madarasa 10,000. Kikubwa kinachotakiwa kudhibiti hali hii ni kusisitiza uadilifu, kudeal na maofisa wala rushwa, kuweka system yenye uwazi na kusimamia kikamilifu rasilimali hii na kuwapa fursa wanavijiji kulinda na kufaidi matunda ya ulinzi. Aidha, wananchi wapate faida za misitu sio kwa kuwajengea tu social infrastructure bali wapate economic gains.
2. Payment for ecosystem services scheme
Hii ni mechanism inayowapa incentive wananchi wanaoishi maeneo ambayo yanatoa ecosystem services kama vyanzo vya maji, vyanzo vya oxygen na carbon sink etc. Scheme hii imeshauriwa na wanasayansi kuwa ni nzuri katika kuwapa motisha wananchi maskin wanaoishi maeneo yanye utajiri mkubwa wa misitu na vyanzo vya maji. Kwa mfano, serikali ina-institute utaratibu huu na kuwawezesha wananchi wanaoishi maeneo yenye utajiri mkubwa wa bioanuai kama wananchi wa matombo wanaokaa chanzo cha mtu Ruvu, mto ambao unawaweka mjini wakazi wa Dar Es Salaam na vitongoji vyake. Serikali ingetoa kauli tu kuwa katika bili za maji, kama ilivyoamua kuwa EWURA wapate asilimia flani, Mimi nadhani badala ya kuwapa EWURA hiyo asilimia, Fedha hiyo ingewaendea wananchi wa Matombo na vitongoji vyake ili kuwapa motisha wasimamie kikamilifu chanzo hicho cha mto ruvu (Kimboza Forest Reserve) na kuwatoa kwenye lindi la umaskani.
Ikumbukwe kuwa wananchi hawa wanakatazwa kulima kwenye milima uluguru kwa ajili ya kuilinda bioanuai, sasa kwanini Serikali isiwafkirie watu hawa kama ilivyowafkiria watu wa Geita na Nyamongo kwenye madini? Kama serikali ingefwata ushauri huu ambao wataalam wamekwisha uona unafaa, wananchi wangekuwa na ari ya uhifadhi na kila wilaya ingekuwa na chanzo cha mapato. Kuna ugumu gani kwa serikali kupitisha sera ya aina hii ili wananchi wafaidike? Mnafurahia nini kuona wananchi wanafedhaheka kwa dhiki kuu?
3.Sekta-Wanyamapori
Sekta hii inapotential kubwa sana ya kututoa hapa tulipo kwenye kuwa omba omba wa kwanza duniani hadi kuwa watoa misaada wakuu duniani. Rasilimali ya wanyamapori haiwasaidii wananchi zaidi ya kuwatia umaskini wananchi. Ni kweli ipo misaada wananchi wanapewa na TANAPA, NCAA na WD lakini misaada hii bado haijaweza kuwapa motisha ya kutosha wananchi kuwafanya waache ujangili na wasaidie uhifadhi. Sababu kubwa ya michango hiyo kuwa midogo inawezekana ni ufinyu wa budget za Mashirika hayo au ni uchezeaji wa hela zinazokusanywa na mashirika hayo.
a) Ufinyu wa fedha zinazokusanywa
Hili ni lakujitakia, Bei za wanyama wetu kupitia uwindaji wa kitalii ni ndogo sana. Bei hizi zimekuwa zikipandishwa kwa kuongeza kiasi kidogo sana kwa sababu ya Rushwa. Akitokea waziri anataka bei za wanyamapori wanaowindwa zipande, waziri huyo atapigwa vita na wala hatodumu kwenye wizara hii. Lakini tujiulize, je ni kwa faida ya nani bei hizi zipo chini? Wapo wawindaji wanaokubaliana na kupanda kwa bei kwa maana wanaona bei tunazowatoza ni dhuruma kwa wananchi wa Tanzania. Ila wapo wawekezaji ambao ukitangaza tu ongezeko la bei watatoa mlio kwa kigezo cha kumuumiza mzawa etc na mwisho wa siku bei hizo zitapanda kwa $5.
Huu ni unyonyaji/uhujumu uchumi. Hivi lengo la Tanzania ni kuua wanyama wengi na kupata fedha kidogo au ni kuwinda wanyama wachache na kupata fedha nyingi?? Tutapata hasara gani kama tukangeweka bei ya juu ili waje matycoon 50 tu kwa mwaka na tukapata hela ambazo zingelipwa na wawindaji wababaishaji 500 ndio tuzipate???Are we really for the quality experience kweli kama sera zetu zinavyotabanaisha???
Hapa pia vigogo wa Taifa hili ndio wameweka mizizi. Utaskia vitalu vya watu wa NEC-CCM, Watoto wa Kawawa, Mwinyi, Ndugu wa Mkapa, Sokoine, Ndugu wa flani na flani. Kwa hiyo kimsingi wanapokataa bei zisipande, wanaokwamisha haya ni viongozi wetu na si vinginevyo. Mimi nadhani wananchi tukomae kuliokoa Taifa hili mana viongozi wetu hawana nia njema, wapo kwa ajili ya maslahi yao na si vinginevyo.
Imagine bei ya Simba kwenye auction ya Safari Club International mwaka juzi ilikuwa ni $ 150,000 kuwinda South Africa. Simba wa Tanzania ana nini kinachompunguzia ubora hadi serikali isione hasara kumuuza kwa $ 4000???kwanini tembo wetu, chui wetu wauzwe kwa bei ya hasara kwenye uwindaji? Sisi tupandishe bei, wasipo kuja wanyama wetu wataendelea kuongezeka. After all, uwindaji ni mchezo wa matycoon wa nchi zilizoendelea, wao matycoon wanalipa hela nying sana kwa ma agent na kwa wenye makampuni ya uwindaji. Sisi kama taifa ndo tunaoingizwa mkenge na hawa wanaojiita outfitters ambao kimsingi ni familia za Kawawa, Sokoine, Mkapa na vigogo wengne , We unadhani kama hakuna wanachopata kwanini wamiliki wa vitalu ni wao wenyewe vigogo??? Si waachie wengine kama wao wanaona ni biashara ya hasara??Hatukatai wazawa kufanya biashara ya uwindaji, wafanye biashara kwa kufwata kanuni na kulpatia mapato stahili sio ujanja ujanja na kuwaibia watanzania kwa kukwepa kodi na kutumia majina yao kutunyonya. Wanaoongoza kuendesha seka ya Utalii South Africa ni wazawa ila wanalipa kodi zote stahiki na sio ujanja ujanja. Lakini pia wananchi tujiulize, Mbona kwenye madini Serikali inawapendelea zaidi wawekezaji kutoka nje???Iweje kwenye uwindaji neno uzawa ndo limesurface zaidi???Chanzo cha hizi double standards ni Rushwa tu na kutaka kumiliki rasilimali za nchi wao na familia zao.
Wataalam walipendekeza hunting blocks zitolewe kwa Auctioning, ili watu washindanishwe na anayetangaza dau kubwa apewe kitalu. Utaratibu huu ungeliingizia taifa fedha nyingi sana na kufanya tasnia ya uwindaji iwe juu. Lakini kwa kuwa vigogo ndio wanataka wamiliki vitalu hivyo kwa kulipa fedha kidogo wakaona utaratibu huu uachwe kwani walijua wangefanya auctioning, wasingepata vitalu hivi wananvyomiliki sasa hivi. Tulipoteza mapato mengi sana, wanaweka kigezo cha uzawa ili wao na familia zao wagawane rasilimali zetu kwa bei chee.Chukueni rasilimali zetu, fedha zetu na mapato yetu mtulipe. Haipo hivyo. Kampuni ya Kawawa ilinyimwa kitalu kwa kushindwa kulipa kodi na michango mingine katika uwindaji, wagawa Hunting blocks wakamnyima kawawa kitalu Maige akawapa kinyemela. Yaliyotokea wote mlisikia bungeni. Kampuni ya malagarasi inayomilikiwa na Dk. Leakey pia inaubabaishaji huo huo pamoja na nyingine nyingi za wazawa. Wanataka kuendesha biashara hizi, uwezo hawana, taratibu hawazifuati, wakinyimwa vigogo wana wakingia kifua wanawapa tena. Tutafika kweli??? Nchi hii sio yenu peke yenu jamani, tupo watanzania 40 milioni, hivyo mnavyoyafanya haya mjue mnawafanyia dhuruma watu milioni 40.
Kuna tatizo lingine kubwa sana kwenye viwanja vya kujenga mahoteli ndani ya mbuga zetu, Huko pia ndio kichekesho. Kwani mtu anapewa kiwanja bila kutoa tsh hata moja. Jamani hata shamba la huko Kazuramimba/Mbekenyela ni lazma utoe kiasi fulani. Iweje viwanja katika maeneo haya muhimu vitolewe bure????Kigogo anapewa kiwanja, then anaweza kumuuzia mtu mwingine kwa mamilioni au kumpangisha mwekezaji mwingine ndo aendeshe biashara. Akianza kuoperate ndio anaanza kulipa mapato ya serikali. System ya kukusanya mapato hayo ipo very porous na kuna alot of leakages za mapato ya serikali. Viwanja hivi pia vimegawiwa kwa vigogo wale wale, familia ya Meghji ni moja ya wanufaika. Hivi kwa nini utaratibu wa serikali usifwate katika kugawa viwanja hivi???kwann wasitangaze watu wakashindanishwa ili kupata mwekezaji bora na sio bora mwekezaji???Kwann tukubali wanufaika wa rasilimali za nchi yetu wawe ni watu hao hao wachache ilhali taifa linapata hasara na lina watu zaidi ya 40m ????
b) Uchezeaji wa fedha katika mashirika ya uhifadhi TANAPA, NCAA, WD/TWPF
Mashirika yanayosimamia uhifadhi yamekuwa yakifanya matumizi holela na ya anasa kanakwamba mashirika haya yanamilikiwa na nchi Tajiri sana. Ukiangalia taratibu za utendaji kazi wa mashirika haya utagundua kuwa almost chote wananchopata, wanakifaidi wenyewe. Kwa utaratibu huu hatuwezi kufika. Kama wale waliopo kwenye madini wakila chote, TRA wakila chote wanancho kusanya, bandari wakila chote hakika hatutofika. Kwa bahati mbaya serikali imekaa kimya ikiangalia haya yakitokea. Mali hizi ni zetu sote, wananofanya kazi ktk mashirika haya wanawawakilisha wananchi wengine walio maeneo mengine. Kila kinachokusanya, inapaswa kitumike wisely, after all mkumbuke biashara ya utalii ni fragile business hivyo sustainability yake bado ni questionable.
Utakuta Tanzania inapeleka maafisa 15 kwenye maonyesho ya utalii Marekani, Kati ya hao watu watano kutoka Bodi ya Utalii TTB (SHIRIKA LENYE DHAMANA KUTANGAZA UTALII TANZANIA) watu 10 Kutoka TANAPA, WD na NCAA. Hivi huu sio uchezeaji wa hela? Sio dublication ya efforts? Kwani TTB wanaenda kutangaza vivutio gani kama sio hifadhi za Taifa, Ngorongoro na game reserves/uwindaji??Kama vipi basi muende kwa rotation ili kupunguza lundo la watu huko nje.
Serikali inalifahamu hili ila inalifumbia macho, Ona budget za mashirika haya kwenye kusafiri nje ya nchi kwenye maonyesho ya utalii. Takwimu/Tafiti zinaonyesha watalii wanaokuja nchini hawaji kutokana na watangazaji hawa wa Tanzania, yaani sio matangazo au mahudhurio ya TTB/Tanapa/NCAA inayowafikia wateja huko nje, Wataje/watalii wengi wanapata information za Tanzania kupitia maagent wa kubwa wa utalii Duniani, TTB/TANAPA/NCAA wanajua hili ila ndo kwanza wanabeef up budget zao za kwenda kutangaza utalii nje ya nchi. Takwimu zingetumika kukataza wafujaji hawa wa nchi yetu kwenda kufanya shopping ulaya na kwingineko, at least ningeelewa kuwa watu hawa wanakwenda Training ya conservation genetics na masomo mengine ambayo technologia yake haijafika bado hapa nchin. Hali haipo hivyo. Ona budget za mashirika haya kwenye ununuzi wa magari ya kifahari.
Wakati Pinda anadanganya taifa kuwa atasitisha ununuzi wa mashangingi kwa viongozi wa serikali, Huko Tanapa Mkuu wa hifadhi anapewa shangingi, Huko ngorongoro mkuu wa kitengo anapewa V8. Hivi tutafika kweli kwa ulifist huu? Kwanini hizo hela tusizielekeze kwenye kupambana na ujangili ambao unacause additive mortailty to legal hunting? We need to change.
Naomba kwa leo niishie hapa, toa mchango wako wa nini kifanyike kwenye sekta hii ya maliasili ili wote tufaidi urithi huu tulioachiwa na mwenyezi mungu. Next time ntaiangalia sekta ua Utalii, katika wizara hii ya Maliasili