mkiluvya
JF-Expert Member
- May 23, 2019
- 802
- 725
Waziri wa Kilimo Japheti Hassunga leo amekutana na Menejimenti ya wizara,wakuu wa Taasisi na Wenyeviti wa Bodi za Mazao zilizopo chini ya Wizara.
Lengo la mkutano huu wa siku mbili unaofanyika katika ukumbi wa wizara Jijini Dodoma ni kujadili maandalizi ya sera mpya ya kilimo ya mwaka 2019 na kuondoa mapungufu yaliopo katika sera ya mwaka 2013.
Akiongea katika kikao kazi hicho Waziri Hasunga ameeleza umuhimu wa kuwa na sera mpya ya kilimo ni kufanya kilimo kuwa na tija na cha kibiashara ,hivyo kuleta maendeleo makubwa katika sekta ya kilimo
“Tunataka sera mpya ya kilimo ilenge kukifanya kilimo kuwa shughuli kuu ya kiuchumi itakayochangia kukuza uchumi wa nchi na kuongeza ajira” alisisitiza Waziri Hasunga.
Waziri Hasunga amebainisha kwamba sera mpya inatakiwa kukamilika kabla ya mwisho wa mwaka huu ili kutoa fursa kwa Bunge kutunga sheria na kanuni za kilimo.
Lengo la mkutano huu wa siku mbili unaofanyika katika ukumbi wa wizara Jijini Dodoma ni kujadili maandalizi ya sera mpya ya kilimo ya mwaka 2019 na kuondoa mapungufu yaliopo katika sera ya mwaka 2013.
Akiongea katika kikao kazi hicho Waziri Hasunga ameeleza umuhimu wa kuwa na sera mpya ya kilimo ni kufanya kilimo kuwa na tija na cha kibiashara ,hivyo kuleta maendeleo makubwa katika sekta ya kilimo
“Tunataka sera mpya ya kilimo ilenge kukifanya kilimo kuwa shughuli kuu ya kiuchumi itakayochangia kukuza uchumi wa nchi na kuongeza ajira” alisisitiza Waziri Hasunga.
Waziri Hasunga amebainisha kwamba sera mpya inatakiwa kukamilika kabla ya mwisho wa mwaka huu ili kutoa fursa kwa Bunge kutunga sheria na kanuni za kilimo.