Wizara ya Kilimo kimya: Mahindi Kusini, bei imeporomoka, soko limedoda na msimu wa mvua unakaribia

Kididimo

JF-Expert Member
Sep 20, 2016
3,791
3,360
Waziri wetu wa Kilimo ninamjua ni mchapakazi. Alipita nchi nzima kuhamasisha wakulima walime kukabiliana na baa la upungufu wa chakula ulioashiria mwanzoni. Pia ilitangazwa asiyelima hakuna msaada wa chakula toka mamlakani.

Matokeo Kusini mwa Tanzania hasa Ruvuma, Mbeya, Rukwa nk wamefanikiwa kuvuna mahindi mengi. Soko lake linasuasua sana. Bei ni ndogo, siyo ya motisha. Wengi wameamua kuhifadhi hadi bei iwe nzuri. Haijajulikana bei itabadilika lini na kwa msukumo upi!

Baadhi ya wakulima hawana maghala imara pia uharibifu wa wadudu umeanza kwa kasi. Mvua nazo zinakaribia watu waanze msimu mwingine. Nini msukumo wa Wizara kuona soko lenye bei ya motisha linapatikana? Kimya kimekuwa kingi,yawezekana tafsiri ya PM kuwa mahindi yasindikwe,bado haijaeleweka kwa Wakulima. Huenda wanasubiri ufafanuzi zaidi kutoka Wizara yenye dhamana na mazao?
 
Bei ya mahindi imeshuka, wakati huohuo serikli INA ruhusu mahindi toka Zambia yaingie Tanzania sasa hiyo ndo nini kuna mkulima atakaye faidika kweli na sekita hiyo?
 
Sio Huko tu mkuu hata Huku kas. Hali ni hyoyo mahind Bado mustakabali haujulikan Kama yatapanda au la
 
Bei ya mahindi imeshuka, wakati huohuo serikli INA ruhusu mahindi toka Zambia yaingie Tanzania sasa hiyo ndo nini kuna mkulima atakaye faidika kweli na sekita hiyo?
Hilo nami nimelisikia. Ila mengi ya Zambia yanakuwa "ontransit" kwenda Kenya na Burundi. Wamepiku maeneo yale Watz walikuwa wakiuza!
 
Bei ya mahindi imeshuka, wakati huohuo serikli INA ruhusu mahindi toka Zambia yaingie Tanzania sasa hiyo ndo nini kuna mkulima atakaye faidika kweli na sekita hiyo?
Kwahiyo ulitaka wazuie tununue debe efu 30?
 
Naombea bei ishuke zaidi ili maisha yawe nafuu, ningependa yadode mpaka bei ya unga iwe 300 aliyoiacha mkapa
Kumbuka , biashara nyingine nazo zitakwama. Purchasing power kwa commercial na domestic goods ya watu wa maeneo hayo hutegemea " wingi" na "bei" ya nafaka na mazao mengine!
 
Mkuu kusema tu bei Ni ndogo bila details Na data Ni jambo lisilokubalika!
Hebu shusha data hapa!
Gunia/ au debe moja bei yake ikoje??
Ukilinganisha Na bei za mwezi kama huu mwaka jana!!
Kuna baadhi ya maeneo mahindi kwa wakati huu Ni dili sana!!

Baadhi ya maeneo ya maeneo mkoani Njombe, debe limeshuka toka sh. 15,000 mwakajana mpaka sh. 3,000.
 
Back
Top Bottom