Wizara ya habari kuchunguza tukio la DED wa Temeke kuwaweka chini ya ulinzi waandishi kwa kufika kwenye kikao chake bila mwaliko

Miss Zomboko

JF-Expert Member
May 18, 2014
4,495
9,275
Mwakabibi.jpg

Wanahabari Christopher James wa ITV&RADIO ONE na Dickson Billikwija wa Island TV waliwekwa chini ya ulinzi kwa saa 3 kwa maagizo ya Mkurugenzi Manispaa ya Temeke Lusabilo Mwakabibi, baada ya wanahabari hao kufika kwenye kikao cha wafanyabiashara wa soko la Mbagala Rangi Tatu na Mkurugenzi huyo bila mwaliko.

"Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo tunafuatilia malalamiko ya wadau wa Tasnia ya Habari juu ya DED wa Manispaa ya Temeke,Mwakabibi, kuweka chini ya ulinzi Wanahabari, tunaomba Wanahabari wawe na subira wakati allegations hizi za kusikitisha zinafanyiwa kazi”-BASHUNGWA

Pia soma > Mkurugenzi wa Temeke, Mwakabibi awasweka ndani waandishi wa habari ili wasihudhurie kikao chake na wafanyabiashara
 
Hawa jamaa bado wana style ile ile ya uongozi ya Mwendazake!!

Rais Samia una kazi ngumu - roho za kikatili na kutofuata sheria na kanuni zimewajaa hawa watu
Hii ishu ya muda..kipindi JPM akiwa hai bado
 
Niliona jana nikashangaa sana, watu wamejisahau sio?
 
Ikibainika kuwa niyeye Lusabilo Mwakabibi ndie aliamrisha basi awajibishwe kwa kuvuliwa nyadhifa na Waandishi wadai fidia za kudhalilishwa kama Wahalifu.
 
Bashungwa ni sound tu he can not effect anything, yuko kati ya 60% ya Prof Assad!
 
Back
Top Bottom