Wizara ya habari ili sio la kulifumbia hata kidogo

Konseli Mkuu Andrew

JF-Expert Member
May 10, 2013
740
855
Moja kati ya wizara ambazo kwa kipindi cha kwanza cha awamu ya tano binafsi naona haijaleta mabadiliko basi ni Wizara ya Habari, Sanaa na Michezo chini ya Dr H Mwakyembe na naibu wake Mh Juliana Shonza.

Wakati wa awamu yao tuliona wazi wamiliki wa tv na radio stations waliitisha press conference na kutoa matamko na kuwataka wafanyakazi wa hivo vituo kutocheza kazi za sanaa za hawa wanasanaa lakini sikuona Mawaziri hawa wakikemea vitendo hivi walikuwa bussy tuu kuhakikisha akina Konk Liquid anatafutiwa tiket iya kwenda kuangalia mechi tuu.

Tunafahamu fika hawa wasanii wengi wao ni vijana waliokosa nafasi katika ofisi mbali mbali na serikali wakaamua kujiajiri katika sanaa sasa kuona kituo X kinatoa tamko la kutocheza kazi za msanii fulani ni sawa na kumnyima nafasi ya kukuza ajira yake.

Leo hii EFM, ETV, CLOUDS FM, CLOUDS TV hawachezi kazi za msanii Diamond na wengine kwa sababu ambazo hazieleweki ila serikali kupitia wizara husika imefumbia macho suala ili kana kwamba kuna sheria inayoruhusu mmiliki wa radio kwa sababu zake mwenyewe tuu kutocheza kazi za msanii fulani.

Ni matumaini yangu kuwa Waziri mpya na naibu wake wakishirikiana katibu wa wizara suala ili hawatalifumbia mdomo wala macho. Kuacha huu uozo kuendelea ni kuruhusu vijana wetu kuendelea kupata misongo ya mawazo tu.
 
Babu Tale juzi kahojiwa clouds fm akasema wao wenyewe wa wcb ndio wali omba nyimbo zao zisipigwe clouds fm

Sasa wewe una taka umsumbue waziri. Bashungwa kwanini ?
 
Sidhani kama Wizara usika ina nguvu ya kukiingilia kituo cha redio kipige wimbo flani na wa flani.
 
Babu tale juzi kahojiwa clouds fm akasema wao wenyewe wa wcb ndio wali omba nyimbo zao zisipigwe clouds fm

Ss ww una taka umsumbue wqz. Bashungwa kwann ?
Mkuu unakumbuka wakati ule wamiliki walitoa matamko wazi wazi.Unakumbuka issue ya 20% na clouds? Je unakumbuka issue ya Ruby na Clouds?
 
Sidhani kama Wizara usika ina nguvu ya kukiingilia kituo cha redio kipige wimbo flani na wa flani.
Mkuu lakini kumbuka wasanii wengi wamepotea kwenye sanaa kutokana na hii hali?
Wengine mpaka wakawa mateja kwa msongo ya mawazo
 
Mbona hamuulizi kwa nini redio na tv hawapigi nyimbo za ndugu yetu deo kisandu?
 
media nayo ni biashara kama zingine

kuna mambo huwezi nipangia katika
biashara yangu, yani unanilazimisha
kwenye duka langu niuze sigara....

hayo ni mambo ya kukaa meza moja
kuongea kibinadamu sidhani kama
ni sheria kwamba media lazima
ipige nyimbo ya kila msanii
 
media nayo ni biashara kama zingine

kuna mambo huwezi nipangia katika
biashara yangu, yani unanilazimisha
kwenye duka langu niuze sigara....

hayo ni mambo ya kukaa meza moja
kuongea kibinadamu sidhani kama
ni sheria kwamba media lazima
ipige nyimbo ya kila msanii
Na je kuna sheria inayo ruhusu kituo fulani kutoa tamko la wazi kuwa kuanzia muda fulani hawatacheza kazi za msanii fulani kwa sababu zao binafsi?
 
Back
Top Bottom