Wizara ya elimu yapandisha ada ya vyuo vya ualimu serikali kuwa kama vyuo binafsi

LTN USU WA MADOSO

JF-Expert Member
Sep 14, 2016
1,193
859
Wizara ya elimu sayansi na tekonolojia imepandisha karo na michango kwa vyuo vya ualimu vya serikali kuwa kama vyuo binafsi miaka ya nyuma vyuo hivi wanafunzi walikuwa wakichaguliwa na vyuo vya serikali vya ualimu walikuwa wanalipia elfu sabini kwa mwaka (70,000/=) lakini sasa hivi serikali imepandisha karo hii ghafla kufikia laki sita (600,000) kwa mwaka hii ni karo tu jumla na michango inafika million Moja na sehemu .

Hii inapelekea watoto wa masikini washindwe kujilipia hivi vyuo lilikuwa kimbilio la watoto wa wakulima watanzania ambao hawawezi kulipa vyuo binafsi sasa hivi vyuo vya ualimu vya serikali na binafsi vinalingana hivyo watoto wa masikini wanachaguliwa vyuo na kushindwa kuripoti vyuoni kutokana na gharama hizi kuwa kubwa sana .


Pia naiomba serikali iwape ufadhili wanafunzi watakaochaguliwa kusomea ualimu wa sayansi ngazi ya stashahada mfano chuo cha kleruu, monduli nk kwa sekondari kwenye vyuo vya serikali mwaka huu wasilipie karo wawe wanasainisha mikataba baada kumaliza masomo yao wafanye kazi serikalini ili kuziba pengo la uhaba wa walimu wa sayansi pia wanafunzi hawa wanashindwa kufika chuoni kufatana na gharama kubwa za vyuo vya serikali hivyo kupelekea kukoswa walimu wa sayansi .

Mwisho niwaombe serikali ipunguze karo na gharama za vyuo vya ualimu ili kuwasaidia watoto wa wakulima kupata fursa ya kusoma kama ilivyokuwa zamani .
 
Wizara ya elimu sayansi na tekonolojia imepandisha karo na michango kwa vyuo vya ualimu vya serikali kuwa kama vyuo binafsi miaka ya nyuma vyuo hivi wanafunzi walikuwa wakichaguliwa na vyuo vya serikali vya ualimu walikuwa wanalipia elfu sabini kwa mwaka (70,000/=) lakini sasa hivi serikali imepandisha karo hii ghafla kufikia laki sita (600,000) kwa mwaka hii ni karo tu jumla na michango inafika million Moja na sehemu .

Hii inapelekea watoto wa masikini washindwe kujilipia hivi vyuo lilikuwa kimbilio la watoto wa wakulima watanzania ambao hawawezi kulipa vyuo binafsi sasa hivi vyuo vya ualimu vya serikali na binafsi vinalingana hivyo watoto wa masikini wanachaguliwa vyuo na kushindwa kuripoti vyuoni kutokana na gharama hizi kuwa kubwa sana .


Pia naiomba serikali iwape ufadhili wanafunzi watakaochaguliwa kusomea ualimu wa sayansi ngazi ya stashahada mfano chuo cha kleruu, monduli nk kwa sekondari kwenye vyuo vya serikali mwaka huu wasilipie karo wawe wanasainisha mikataba baada kumaliza masomo yao wafanye kazi serikalini ili kuziba pengo la uhaba wa walimu wa sayansi pia wanafunzi hawa wanashindwa kufika chuoni kufatana na gharama kubwa za vyuo vya serikali hivyo kupelekea kukoswa walimu wa sayansi .

Mwisho niwaombe serikali ipunguze karo na gharama za vyuo vya ualimu ili kuwasaidia watoto wa wakulima kupata fursa ya kusoma kama ilivyokuwa zamani .

Safi sana hadhi ya waalimu nayo itapanda, halafu mzigo kwa serikali utapungua. Halafu wajinga wataongezeka na nguvu kazi kuongezeka mtaani.
 
Tunaomba huo waraka wa badiliko la karo. Kama kweli tunakokwenda siko kuzuri. Mungu tubariki watanzania wanyonge
 
Huo ualimu ni wa levo gani ulikua ukilipiwa elfu 70? Pia umesema zamani ni zamani mwaka gani?

Nimesoma chuo cha serikali na ada ya ualimu ukitoa michango mingine ilikua laki tisa (9) kwa levo ya shahada.
Stashahada na cheti kwa vyuo vya serikali ambavyo vipo chini ya necta mfano ,butimba ttc ,kleruu ttc ,tabora ttc nk karo yake mwaka 2014 ilikuwa elfu 70000 ,sasa hivi ni laki sita plus michango ni million Moja point
 
Tunaomba huo waraka wa badiliko la karo. Kama kweli tunakokwenda siko kuzuri. Mungu tubariki watanzania wanyonge
Yaani ndugu hii nchi imefikia pabaya sana hivi serikali inafikri mkulima anaweza pata wapi laki sita kwa mwaka plus michango million na point
 
Hao watoto wa mskini uzuri baba zao na ndugu walichagua chichiemu sasa waache wajikaange kwa mafuta yao wenyewe
 
Stashahada na cheti kwa vyuo vya serikali ambavyo vipo chini ya necta mfano ,butimba ttc ,kleruu ttc ,tabora ttc nk karo yake mwaka 2014 ilikuwa elfu 70000 ,sasa hivi ni laki sita plus michango ni million Moja point
Kwakua nilikua sijui ada yao imebidi nitafute taarifa husika nimeipata ikiwa kama hivi;

1479978457593.png



1479978515133.png


Umetembeza chai katika baadhi ya facts mkuu.
 
Hapo zamani vyuo vya serikali walikuwa wanalipa karo elfu sabini (70,000/=) kwa mwaka lakini sasa hivi imepanda na kufikia laki sita kwa mwaka (600,000/=) jumla na michango yote millioni Moja kwa mwaka.

Watoto wa masikini hawawezi kusoma tena kutoka na kukoswa hii karo kubwa kwao hivi vyuo vya serikali ndoo lilikuwa kimbilio la watoto wa wakulima naomba serikali ipunguze karo ili kuwapa nafasi watoto wa masikini kusoma na kupata maarifa kwenye vyuo hivi.

Naomba serikali itoe ufadhili kwa kuwasomesha wanafunzi watakaopata nafasi ya kwenda kusoma stashahada ya ualimu wa masomo ya sayansi kwa vyuo vya serikali kama kleruu ttc ,monduli ttc ili waweza kuhitimu masomo yao na kupunguza pengo la uhaba wa walimu wa sayansi na ufundi nchini serikali kupitia wizara ya elimu ingewaruhusu hawa wanafunzi watakao chaguliwa kwenda kusomea ualimu kwa upande wa sayansi kwa ngazi ya diploma iwalipie karo ili waweze kusoma wengi huwa wanachaguliwa vyuo hivi vya serikali lakini wanashindwa kuripoti chuoni kufatana na gharama kuwa kubwa wizara ya elimu ingefanya kama inavyofanya wizara ya Afya kusomesha wataalamu wa Afya ili kuziba uhaba na hivyo hivyo wizara ya elimu ingefanya hivyo ili kupata walimu wa sayansi ,ufundi na maabara.

Mwisho naiomba serikali ipunguze gharama na karo ili iwawezeshe watoto wa masikini kusoma.

Serikali punguzeni gharama hizi hapa chini

414a3be7832d25f3a4eab7ae3a34df84.jpg
0265794fbb09e3a103c4957b7bb58a4d.jpg
 
Bajeti ya mwaka huu ya mikopo ya elimu imekwisha, vijana wote waliokosa mikopo waliambiwa waende JKT
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom