Wizara ya Elimu yaja na "Samia Schorlaship" kuinua masomo ya sayansi

benzemah

JF-Expert Member
Nov 19, 2014
1,504
3,032
Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Profesa Adolf Mkenda, akizungumza na wahariri wa vyombo vya habari Jijini Dar es Salaam kueleza mikakati ya wizara yake ambayo ikiwemo utekelezaji wa bajeti ya mwaka 2022/23 iliyopitishwa bungeni amesema Serikali imetenga shilingi Bilioni 3 kwa mwaka huu kwa ajili ya kuwezesha ufadhili kwa wanafunzi ambao wamepata ufaulu mkubwa katika elimu ya juu kupitia masomo ya sayansi

“Kigezo cha atakayepatiwa ufadhili huo ambao wengi wanataka uitwe Samia Scholar ni kufaulu vizuri katika masomo ya sayansi na upo tayari kuendelea na kusoma masomo ya uhandisi,elimu tiba.Kwa sasa tunatoa udhamini huo kwa vyuo vya ndani tu,”amesema Prof.Mkenda.

Amesema wataweka dirisha kwa wanafunzi wenye mahitaji maalumu ili nao waweze kunufaika na ufadhili huo ambao utakuwa unatolewa bila kujali huyu katoka wapi au familia gani, ilimradi awe amefaulu vizuri sayansi na afahamu kuwa, anasoma kwa kodi ya Watanzania, hivyo anapaswa kuonesha bidii ili aje kuwahudumia kupitia taaluma yake.
 
Profesa anaendekeza sifa za kijinga kama wale wahuni wa uvccm. Badala ya Profesa kuja na mikakati inayoeleweka kwa umma, anaingiza siasa za kijinga za kumtukuza rais. Nchi hii kuna tofauti ndogo sana kati ya aliyesoma na ambaye hajasoma.
 
Pelekeni Vijana Ulaya, Marekani na Australia wakasome engineering achaneni na hivi vyuo vya ndani. Wakimaliza waombeeni Internship kwenye makampuni makubwa duniani huko wasambae msiwape limitations wakipata kazi wapotelee huko huko in 100yrs tutabadiri hizi akili huku.

Iwe engineering, IT na course za science tumieni hela ya nchi kwa vitu kama hivyo na sio hizi siasa za hovyo hovyo.
 
Hivi vyuo vya ndani vikiongozwa na baba yao pale Mlimani city achaneni navyo kwa sasa vitasaidia baadaye huko tukipata akili.

Pelekeni maelfu ya vijana kila kona ya dunia wakasome macourse yakueleweka huko duniani muachane na hizi elimu za siasa kama Sociology, Public administration, social science, political science, sheria nk hawa wapiga poroja waacheni wasome hapa kule ughaibuni pelekeni watu wakasome science and technology.
 
Kama fedha ni za umma( kodi za watanzania),Kwanini jina liwe samia na sio Tanzania scholarship?
 
Back
Top Bottom