Wizara ya Elimu: Shule za bweni shule za msingi zifungeni. Ni uzembe wa malezi

MchunguZI

JF-Expert Member
Jun 14, 2008
4,006
2,166
Baada ya ajali na kupoteza maisha ya watoto kule Kagera, shule nyingine mkoani Tabora imeungua. Mmoja katika waliohojiwa alionesha mashaka kwamba kwa nini kwa muda mfupi kiasi hiki na kwa nini zote za dini moja - alimaanisha za Kiislamu.

Binafsi nina tatizo na ubora na tabia ya kupeleka watoto wa primary shule za boarding. Hakuna sababu ya kumpeleka mtoto wa primary boarding maana hata walio yatima wanalelewa sehemu maalumu pia na siyo shuleni.

Umri wa miaka 6 hadi 13 ni umri wa kujifunza lugha mbalimbali na ni umri wa kupata tabia na ulinzi maalumu kutoka kwa wazazi. Vyote hivi hutavipata shuleni. Inapotokea ajali kama hiyo ya moto, hawa ni watoto wasioweza kujiokoa. Ni watoto ambao hata maisha ya kawaida, hata kuamka ni kitendo wanachohitaji msaada! Je, nani awaokoe kwa wingi wao?

Shule zimejengwa kama kambi za kutwa! Hazina miundombinu ya kuzima moto, hata maji ya kuoga ni kubahatisha tu! Kwa ujumla ni shule za mtaji mdogo wakati watoto wanahitaji makubwa zaidi ya hayo. Hakuna walezi waliosomea kulea watoto.

Tuachane na mikogo ya boarding kwa watoto wadogo kiasi hiki. Kama ni kiingereza watakifahamu tu kwa day schools.
 
Mkuu nakubaliana na wewe 100%.Niseme wazi bila kumung'unya maneno.

Ni ujinga wa hali ya juu kumpeleka mtoto wa chini ya miaka 13 boarding school,kwa kuwa this is the time when his/her character is being molded.

Mzazi mwenye akili anapenda tabia ya mtoto wake ifanane na yake,and this can only be achieved by staying with him/her and mold his character.

Wazazi please note this,ukimlea mtoto kama utakavyo wewe, hata akikua hataiacha tabia uliyo impart kwake.

So unataka mtoto awe shoga, mtumia unga, mvuta bangi na mwenye tabia za kishenzi za mtaani? Mpeleke boarding kabla ya miaka 13, nakuhakikishia atakuwa na tabia za kishenzi.
 
areafiftyone,

Boss! Ukibahatika kufika shule ya msingi ya boarding, inasikitisha. Siku wanayoita visiting, wazazi utawaona kama mabwege fulani. Wengi watahangaika kuzungumza kiingereza na watoto wao badala ya kuangalia nini watoto wao wanakikosa kwa wazazi.

Kilichonishangaza, shule ya Kagera, kuna wazazi walihojiwa na kusema wanaishi karibu na shule na hata walisaidia kuokoa watoto wakati moto unawaka. Kwa umbali huo ni nini kilichowafanya wasiishi na watoto wao?

Umaskini una sura nyingi sana! Kuna watu wanaona ni sifa na nyongeza ya ufahali kumuweka kijana wa miaka 6 boarding school!
 
areafiftyone,

Boss! Ukibahatika kufika shule ya msingi ya boarding, inasikitisha. Siku wanayoita visiting, wazazi utawaona kama mabwege fulani. Wengi watahangaika kuzungumza kiingereza na watoto wao badala ya kuangalia nini watoto wao wanakikosa kwa wazazi.

Kilichonishangaza, shule ya Kagera, kuna wazazi walihojiwa na kusema wanaishi karibu na shule na hata walisaidia kuokoa watoto wakati moto unawaka. Kwa umbali huo ni nini kilichowafanya wasiishi na watoto wao?

Umaskini una sura nyingi sana! Kuna watu wanaona ni sifa na ufahali kumuweka kijana wa miaka 6 boarding school!
Hakuna kitu kibaya mkuu kama umaskini wa fikra.Huu ni umaskini wa fikra per se!Kupeleka watoto wadogo shule za bweni Waswahili wanasema ni "sifa za kijinga." Ni kweli mkuu,kama huwezi kumlea mtoto ni heri ukaacha kumzaa.
 
Hao wazazi wanaopeleka watoto wadogo shule wanaohitaji malezi ndio wana matatizo na hawana huruma kwa watoto waliowazaa wenyewe, dah nilisikitika wale watoto waliokufa kagera wazazi kama hatuwezi kulea ni Bora kuacha kuzaa sasa.
 
Naunga mkono hoja. Mtoto apelekwe boarding school angalau kuanzia form 2 au form 1. Tena ni pale tu inapolazimu, ili mtoto apate malezi bora ili hata atakapokwenda boarding awe tayari na misimamo ya malezi ya wazazi
Mimi nasema mtoto aende boarding akiwa advance sikuhizi watoto Wana maliza mapema ni vizuri wazazi tuwalee watoto mpaka wapevuke ndio tuwapeleke boarding.
 
Kuna shule moja iko Moshi, jaman ni shule huwa ina performance nzuri sana kimkoa na kitaifa, nilichukuaga form mwanangu akasome hapo day darasa la kwanza na nafasi alipata, ila ile siku kaenda kwenye intervyuu nilimpeleka mwenyewe, niliwakuta watoto jamani jamani wachafuuuu hao, wako peku peku, kwasababu shule ina day na boarding, mbona niliondoka na nafasi nikawaambie wauze tu!

Nilirudisha mwanangu shule ile ile aliyosomea chekechea sikutaka makuu! Aiseee hapana!

Wazazi amkeni! Mungu akinipa uzima, wanangu watasoma day, ntawapeleka mpaka nikiona wanaweza kujisimamia. Ile siku nilitoa machozi kwa huzuni.
 
Wazazi hawajui tu ila wanawafelisha sana watoto kuwabwaga boarding school katika umri mdogo.

Alafu shule nyingine + wazazi bila hata aibu utawasikia, "Darasa la nne na la saba ni lazima." Ukiwauliza huo ulazima unatokana na nini. Eti bila hivyo matokeo yatakuwa mabaya. Kweli uache kumkomalia mtoto kusoma darasa la I, II, III ukitarajia kwamba boarding school ndo itafanya muujiza darasa la IV au VII?🤔🤔

Mi ndo maana huwa nasema sitopelekeshwa na shule hata siku moja. Maadam ada inalipwa basi ikibidi ntamuhamisha dogo kadri inavyobidi ili asije akakumbana na mbwembwe za kipuuzi.
 
Namfikilia mtoto wa miaka 6, 7 ambaye hata kuoga anakumbushwa. Anafundishwa kutumia sabuni, kunawa mikono, kupenga kamasi, hata homa anaambiwa na mzazi/mlezi, nk. leo anapelekwa boarding ambako kuna watoto 100 wanaohitaji huduma kama hiyo, akalelewe na mtu kwa mshahara tu, na siyo upendo.

Tuache ulimbukeni! Ni bahati mbaya inapelekea kupoteza maisha ya watoto.
 
Baada ya ajali na kupoteza maisha ya watoto kule Kagera, shule nyingine mkoani Tabora imeungua. Mmoja katika waliohojiwa alionesha mashaka kwamba kwa nini kwa muda mfupi kiasi hiki na kwa nini zote za dini moja - alimaanisha za Kiislamu.

Binafsi nina tatizo na ubora na tabia ya kupeleka watoto wa primary shule za boarding. Hakuna sababu ya kumpeleka mtoto wa primary boarding maana hata walio yatima wanalelewa sehemu maalumu pia na siyo shuleni.

Umri wa miaka 6 hadi 13 ni umri wa kujifunza lugha mbalimbali na ni umri wa kupata tabia na ulinzi maalumu kutoka kwa wazazi. Vyote hivi hutavipata shuleni.

Inapotokea ajali kama hiyo ya moto, hawa ni watoto wasioweza kujiokoa. Ni watoto ambao hata maisha ya kawaida, hata kuamka ni kitendo wanachohitaji msaada! Je, nani awaokoe kwa wingi wao?

Shule zimejengwa kama kambi za kutwa! Hazina miundombinu ya kuzima moto, hata maji ya kuoga ni kubahatisha tu! Kwa ujumla ni shule za mtaji mdogo wakati watoto wanahitaji makubwa zaidi ya hayo. Hakuna walezi waliosomea kulea watoto.

Tuachane na mikogo ya boarding kwa watoto wadogo kiasi hiki. Kama ni kiingereza watakifahamu tu kwa day schools.


Natamani Wizara ya Elimu wangesikia hoja hii na kuchukua hatua ya kupiga marufuku shule za Msingi za Bweni.


Maisha ya Bweni kwa watoto wadogo yaani shule za awali na Msingi zina madhara mtambuka kwa watoto na jamii hasa nyakati za baadae wanapokuwa watu wazima:

1. Hupoteza mshikamano na familia
2. Hukosa maarifa ya nyumbani
3. Hukosa kujifunza tabia na hulka
4. Hujifunza ushoga, usagaji, madawa, sigara nk
5. Hukosa kujifunza maarifa ya kimungu
6. Hukosa upendo na kuwa watu katili
7.Huonewa na wenzao, walezi nk
8....
9.....
Na mengine mengi

Shule za Bweni kwa sasa zinapatikana barani Afrika kwa wingi. Kwingineko hakuna shule za Bweni hata ngazi ya High School/Adavanced au ni kwa nadra sana kupatikana mabara mengine.

Ni bora basi angalau shule zetu za Msingi na za Awali zisiwe za Bweni.
 
Hii ni sehemu ya mpango mkubwa na mpana wa kuharibu familia na hatimaye jamii uliobuniwa na Shetani a.k.a NWO.Kwa mtu makini ataona hili likiendea wazi kabisa.Zipo taarifa za kuaminika kabisa kwamba katika shule za bweni wapo agents walio penyezwa kwa siri wakiwa kama wanafunzi au waalimu kwa nia moja tu:kuharibu maadili ya watoto.Sasa kama wazazi hatutakuwa makini,tutaishia kuvuna mabua.Link ifuatayo inaonyesha uhalisia wa uharibifu na vita inayoendelea dhidi ya familia na jamii.

We are at war. The very foundation and stability of the traditional family,is being formidably attacked from every direction
 
Back
Top Bottom