Wizara ya elimu kwa hili hapana

b191

JF-Expert Member
Jul 24, 2016
742
1,030
Habari wanajamvi.

Hivi karibuni Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ilipiga marufuku kwa Shule binafsi kuchuja (Screening). Binafsi siungi mkono tamko hili. Labda nitoe sababu chache;

1. Mchujo katika shule za Setikali, hata Serikali imekuwa ikifanya mchujo katika Shule zake (Screening). Mfano, mtihani wa Kidato cha pili huwaondoa wale wote walio chini ya Alama 30. Hapa ni kwa shule zote binafsi na zile za Serikali.

2. Makundi, Serikali imekuwa ikiwagawanya wanafunzi kulingana na viwango vyao vya ufaulu. Baadhi ya shule ni maalumu kwa wale wenye DARAJA LA KWANZA na baadhi ni maalumu kwa wale wenye DARAJA LA PILI pia DARAJA LA TATU wana-shule zao. Mfano, huwezi kukuta mwanafunzi mwenye DARAJA LA TATU akienda kusoma SHULE kama MZUMBE ai ILBORU.

3. Mkataba, FOMU za kujiunga na shule ni mkataba kati ya MZAZI, MWANAFUNZI na SHULE. Mzazi akienda Shule kabla ya kufanya jambo lolote hupewa FOMU ambayo ina maelekezo ya Shule ikiwa ni pamoja na ALAMA ZA UFAULU. Mzazi anao wajibu wa kukubali au kukataa masharti ya shule. Hapa Mzazi anaweza kukataa kwa kutompeleka mwanae katika shule husika. Hata katika shule za Serikali kuna masharti ambayo mzazi au mwanafunzi akikiuka huondolewa shuleni.

Binafsi siwaungi mkono wazazi wanaolalamika kuhusiana na watoto wao kufanyiwa mchujo kwani wao wenyewe kwa hiari yao walikubaliana na masharti ya shule husika. Serikali pia iziache hizi shule binafsi ziendelee kuendesha Elimu kwa ufanisi mkubwa bila kukiuka sheria za nchi kwa sababu yanayofanyika kwenye shule binafsi hufanyika pia kwa shule za Serikali.

Nawasilisha.
 
Elimu yenye maslahi ya Taifa lazima Ichuje wanafunzi ili wapatikane wanafunzi wanahitajika.
Elimu yenye maslahi binafsi itasomesha wanafunzi wote kuanzia mwanzo hadi mwisho.

NI NANI ALIEIACHIA LAANA HII NCHI MASIKINI..? rudi utusamehe tunaangamia wanao.
 
Elimu yenye maslahi ya Taifa lazima Ichuje wanafunzi ili wapatikane wanafunzi wanahitajika.
Elimu yenye maslahi binafsi itasomesha wanafunzi wote kuanzia mwanzo hadi mwisho.

NI NANI ALIEIACHIA LAANA HII NCHI MASIKINI..? rudi utusamehe tunaangamia wanao.
Asante Mkuu kwa kunisaidia.
 
hapo sasa wanakwenda sipo! Shule za binafsi wanataka shule zao zijenge jina halafu umwambie asichuje!
 
Ukiona watu wanafanya mambo ya kusadikika ujue uwezo wao nao ni wa kusadikika na wanatoka taifa la kusadikika as well...
Hahhaaaa.. Lafing but deeply crying
 
Kuna vitu vinashangaza kwa kweli, hivi km mwanafunzi hana uwezo wa kuvuka darasa anawahishwa aende wapi?
Muheshimiwa fikiri kwa mara nyingine tena, unachotaka kukifanya hakimsaidii mwnf zaidi ya kumdidimiza.
 
Mbona wao government wana mchujo wa special school. Shule ya vipaji uchwala!
 
Serikali ishakosa ajenda ya makusudi zaidi ya kulikia hili mara lile hasa wizara ya elimu nadhan ndo wizara inayoongoza mpk sasa kwa matamko
 
Ni kweli bila kuchuja wanafunzi watabweteka na hivyo kufanya wanafunzi wengi kufeli mitihani yao ya mwisho
 
hua sioni umuhimu wa special schools aisee....afute na special schools
 
Ni kweli bila kuchuja wanafunzi watabweteka na hivyo kufanya wanafunzi wengi kufeli mitihani yao ya mwisho
Kujituma ni siri ya mafanikio, shule nyingi ambazo huwa zinachuja wanafunzi hufanya vizuri sana kwa sababu hujituma. Mfano katika shule za Seminari wanafunzi wanajituma sana kwa kujisomea wakiogopa kuchujwa. Hata nidhamu pia huwa ni nzuri.
 
Kuna vitu vinashangaza kwa kweli, hivi km mwanafunzi hana uwezo wa kuvuka darasa anawahishwa aende wapi?
Muheshimiwa fikiri kwa mara nyingine tena, unachotaka kukifanya hakimsaidii mwnf zaidi ya kumdidimiza.
Wanataka akapate ZERO ili wamwite kilaza.
 
Habari wanajamvi.

Hivi karibuni Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ilipiga marufuku kwa Shule binafsi kuchuja (Screening). Binafsi siungi mkono tamko hili. Labda nitoe sababu chache;

1. Mchujo katika shule za Setikali, hata Serikali imekuwa ikifanya mchujo katika Shule zake (Screening). Mfano, mtihani wa Kidato cha pili huwaondoa wale wote walio chini ya Alama 30. Hapa ni kwa shule zote binafsi na zile za Serikali.

2. Makundi, Serikali imekuwa ikiwagawanya wanafunzi kulingana na viwango vyao vya ufaulu. Baadhi ya shule ni maalumu kwa wale wenye DARAJA LA KWANZA na baadhi ni maalumu kwa wale wenye DARAJA LA PILI pia DARAJA LA TATU wana-shule zao. Mfano, huwezi kukuta mwanafunzi mwenye DARAJA LA TATU akienda kusoma SHULE kama MZUMBE ai ILBORU.

3. Mkataba, FOMU za kujiunga na shule ni mkataba kati ya MZAZI, MWANAFUNZI na SHULE. Mzazi akienda Shule kabla ya kufanya jambo lolote hupewa FOMU ambayo ina maelekezo ya Shule ikiwa ni pamoja na ALAMA ZA UFAULU. Mzazi anao wajibu wa kukubali au kukataa masharti ya shule. Hapa Mzazi anaweza kukataa kwa kutompeleka mwanae katika shule husika. Hata katika shule za Serikali kuna masharti ambayo mzazi au mwanafunzi akikiuka huondolewa shuleni.

Binafsi siwaungi mkono wazazi wanaolalamika kuhusiana na watoto wao kufanyiwa mchujo kwani wao wenyewe kwa hiari yao walikubaliana na masharti ya shule husika. Serikali pia iziache hizi shule binafsi ziendelee kuendesha Elimu kwa ufanisi mkubwa bila kukiuka sheria za nchi kwa sababu yanayofanyika kwenye shule binafsi hufanyika pia kwa shule za Serikali.

Nawasilisha.
Kwa asilimia fulani,naweza kukubaliana na wewe,ila nijibu haya;-
1. Serikali imeweka kiwango cha ufaulu kwa form two kuwa wastani wa maksi 30. Nyie shule binafsi mmeweka standard marks ngapi? Huoni kwa kila shule binafsi kujipangia kiwango,ndo mwanzo wa vurugu na uonevu?
2. Hayo madaraja ya ubora wa shule binafsi hupangwa kwa vigezo gani na nani?
3. Kuna utafiti wowote uliofanyika kujustify kuwa wanafunzi waliohitimu katika madaraja ya juu kutoka shule binafsi ndio haohao wanaoperfom vyema serikalini au taasisi nyingine?
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom