Wizara ya Elimu izibadilishe shule za msingi za Serikali ziwe English Medium. Soko kubwa sana, Serikali ipate hela ya ada yanayovunwa na watu binafsi

FRESHMAN

JF-Expert Member
Sep 29, 2011
8,822
33,515
Habari wadau

Naona kuna soko kubwa sana la wazazi wanaopenda watoto wao wasome English Medium. Nawashauri Serikali, kila wilaya nchii hii wawe na shule za msingi za Serikali za English Medium kama Olimpio na Diamond. Wazazi watashukuru sana na sana.

Hizo pesa ambazo shule binafsi wanazivuna ni bora zivunwe na Serikali zijenge nchi. Maana industry ya Private Schools ina mzunguko wa matrilioni kwa mwaka
 
Ni kweli kabisa itasidia sanaa na serikali itapata mapato mengi ,mm sijasoma English medium Nina kingereza sio kibaya sanaa ilaa ilaa nichakuminyana mno na ndo kinapima mambo mengi sahivi hata kwenye usaili Mara nyingi kiingereza kinahusika na sio kiswahili ,

Nikipata hela siwezi mpeleka mwanangu st .kayumba .
 
Pita pembeni na zako ukiona una visenti siyo wote wanazo.

Tulia acha maisha yetu tunayajua wenyewe.

Sijasema shule zote.. ndio maana nikatoa mfano wa olimpion na diamond...mbona hizo zipo na hazijaharibu elimu bure.

Katika shule za msingi za serikali 1000 wanatakiwa waweke 250 za english medium za kulipa ada na 750 za kayumba kiswazi za elimu bure.. sasa wazazi waamue wenyewe walipe ada ama elimu bure
 
Sanaa ipi unayoizungumzia
Ni kweli kabisa itasidia sanaa na serikali itapata mapato mengi ,mm sijasoma English medium Nina kingereza sio kibaya sanaa ilaa ilaa nichakuminyana mno na ndo kinapima mambo mengi sahivi hata kwenye usaili Mara nyingi kiingereza kinahusika na sio kiswahili ,

Nikipata hela siwezi mpeleka mwanangu st .kayumba .
 
Hili wazo lingefanyiwa kazi naamini msongamano uliopo katika Shule za Olimpio na Diamond ungepungua kwa kiwango cha juu pamoja na kufanyika English medium lakini shule hizi hazikidhi vigezo ukilinganisha na shule za Tusime na Kaizirege
 
Habari wadau

Naona kuna soko kubwa sana la wazazi wanaopenda watoto wao wasome English Medium. Nawashauri Serikali, kila wilaya nchii hii wawe na shule za msingi za Serikali za English Medium kama Olimpio na Diamond. Wazazi watashukuru sana na sana.

Hizo pesa ambazo shule binafsi wanazivuna ni bora zivunwe na Serikali zijenge nchi. Maana industry ya Private Schools ina mzunguko wa matrilioni kwa mwaka
Halafu mwalimu aliyesoma kiswahili na kupata division 3 point 25 au division 4 ndiye afundishe watoto kingereza.
:D:D:D
 
halafu ikasomeshe walimu wa shule250 ili kuendana na mtaala wa kiingereza kwa hela gani?
 
Kwa waalimu hawa ninao wajua waliopo shule za msingi waalimu gani. Elimu yetu ipo centralized usisahau ilo. Serikali ikiamuakufanya biashara ya elimu tutakuwa tunazidi kuligawa taifa la kesho kuliko hivi sasa jinsi ilivyo. Tutazidi kuinua lugha ya kiingereza na kuacha lugha yetu ya Taifa ya Kiswahili. Nachopendekeza iwepo mamlaka ya udhibiti yakinifu juu ya gharama za ada. Maana ada zinazotozwa kwenye private school hazipo realistic na huduma wanayopata watoto. Shule hizi zipo kibiashara. Nimefundisha private school nyingi ni chache nilizoona zina nia ya kumsaidia mzazi na mtoto.
 
Back
Top Bottom