Wizara ya Elimu imeshindwa kuandaa audio na video ya vipindi vya masomo mbalimbali?

Wizara haimaanishi watu waliopo kwenye makao makuu ya wizara ya elimu pekee, wizara ya elimu ni kubwa kuliko hapo. Wizara inainclude taasisi nyingi ikiwemo vyuo vikuu vya serikali, VETA , taasisi ya elimu, NECTA n.k. Kabla ya kuhamishiwa TAMISEMI hata shule zote za serikali pia zilikuwa sehemu ya wizara ya elimu.

Kwa sasa hivi wizara bado inasimamia shule kwenye mambo mengi ikishirikiana na TAMISEMI ikiwemo mitaala na viwango na nadhani hapo ndipo mtoa mada anataka wizara kuplay part. Wanaweza kufanya kazi na walimu kuandaa media resources za kufundishia wanafunzi na kuanza na mahali kutumika mahali ambapo kuna miundimhinu ya msingi kama umeme na internet na kuendelea kuongeza network hadi kufikia shule zote.

Si lazima ifanyike yote kwa pamoja lakini inaweza kuchukua hata miaka kumi, ila la muhimu ni kuanza. Wakati itapofikia vijiji ambavyo kwa sasa hakuna internet/umeme tutakuwa tumeshaboredha media resources zenyewe, kutakuwa na walimu wenye uzoefu wanaoweza kufundisha na ku-share uzoefu na wezao na pia kutakuwa na wanafunzi wengu ambao walipata elimu bora kutokana na improvements za jinsi ya kufundisha.
Sasa mkuu, unataka Wizara na taasisi zake, watoe video na audio kusomesha wanafunzi wa Feza kwa mfano?

Nafikiri utakuwa hujanielewa, Jukumu la kusomesha mwanafunzi sio la Wizara, ni la MWALIMU.
 
Ni wangapi watafikiwa na huo mfumo? tutaingia kwenye janga lingine la kuwatenga wengine.
 
Sasa mkuu, unataka Wizara na taasisi zake, watoe video na audio kusomesha wanafunzi wa Feza kwa mfano?

Nafikiri utakuwa hujanielewa, Jukumu la kusomesha mwanafunzi sio la Wizara, ni la MWALIMU.
Naona sote hatujaelewana. Sijamtoa mwalimu kwenye equation ya kufundisha lakini tufahamu kwamba mwalimu ni mtekelezaji tu wa kile kinachoandaliwa na wizara.
 
Naona sote hatujaelewana. Sijamtoa mwalimu kwenye equation ya kufundisha lakini tufahamu kwamba mwalimu ni mtekelezaji tu wa kile kinachoandaliwa na wizara.
Wizara ya Elimu imeshatoa Syllabus, Wizara ime sha certified izo shule. It is up to those school to teach the students. HAwahitaji Wizara ya Elimu kuwapa amri shule watoe audio au wafundishe via videos. Wizara ikashatoa Syllabus ni kazi ya mwalim kufundisha na kujua jinsi gani atafundisha.
 
Ulitakiwa uwaambie before corona ili na wewe usionekane mtu wa gubu, kujishaua, mnafiki na mpenda kulaumu wengine...

Umejua kuwa kuna online teaching lini??
Nilikuwa nawawaza wanafunzi wangu ambao umeme wanauona shule tena wa generator wakati wa usiku. Hii mambo ya digital wataiweza kweli.
 
Nonsense! mwanafunzi akiwa na swali atamuulizaje mfunzi wake? Akiwa hajafahamu mfunzi atajuaje? au vipi wanajua kama hata wanasikiliza ama kutizama icho kipindi?

Na vipi shule za private nazo? Hata wao pia Wizara ya Elimu iwafanyie hio kazi? Comeon! Tuwe wahalisia wanandugu.
Umeongea kitaalamu zaid tatizo lq nchi yetu watu wanabaka fani hiv unamtumia assignment mtoto utajuaje kama kafanya yeye au mzazi.
Kibongo bongo online teaching & learning ni ngumu hasa kwa level za chini.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Karne hii ya kidigitali wizara hii inafanya ? Vifaa vipo, walimu wapo wa kurekodi, nini shida?

Kwa kila topiki tena na nyenzo za kufundishia

Hii Wizara iamke usingizini
Naona unaamini kwamba shule zote zipo hapo mbezi beach na msasa sio? Hebu toka kidogo hata wilaya ya mkuranga hapo nadhan unaweza kuja na wazo mbadala
 
Kwani zile PC na mil50 tulishapewaga ili ndo zitusaidie kununua hata projector wanafunzi wawe wanasoma kwa shift
 
una akili sana, bahati mbaya watu wenye akili katika nchi zetu huwa hawapewi vyeo au nafasi yeyote


Sent using Jamii Forums mobile app
Usimpake mafuta kwa mgongo wa chips.
Kwa Wanafunzi gani mlio nao? Sio University, middle colleges ,secondary hata primary.
Kwa wazazi gani waliopo wanao tazama series kutwa kucha
Kwa mitaa ipi inayopiga kelele kutwa
Kwa maisha gani ya chini ya Dola moja?
Soksi ya 1000/ ya shule ni mtihani.
Acheni kujichanganya.
 
Back
Top Bottom