Mwezi Septemba 2011 Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi ilifanya Uteuzi wa Wakuu wapya wa Vyuo nchi nzima-Tanzania Bara na kuwabadilisha vituo wengine ambapo miongoni mwa Wateule wapya ni Bw. MATHIAS MVULA ambaye ameteuliwa kuwa Mkuu Mpya wa Chuo cha Diploma za Ualimu TUKUYU, MBEYA lakini pamoja na Uteuzi huo, kumekuwa na maneno ya chini kwa chini kuhusu Sifa na Uadilifu wa Bw.Mathias Mvula kama ifuatavyo:-
- Elimu ya Bw.Mvula ni Diploma ya Ualimu lakini pia kuna maelezo kwamba alijiendeleza kwa kusoma Open University of Tanzania(OUT) Shahada ya Ualimu ambapo kuhitimu kwake kuna Giza kutokana na maneno kuwa wakati huo (2008) Open University kulikuwa na Udanganyifu wa Mitihani, malalamiko ya Usahihishaji na mengine mengi.Hivyo hili linatia kiwingu juu ya uwezo wake Kitaaluma Bw.Mvula.
- Serikali haifanyi Biashara lakini kazi yake kubwa ni kutoa Huduma kwa Umma/Wananchi wake.Katika kipindi cha 2009-2011 Bw.Mvula alikuwa Chuo cha Ualimu Dakawa ,Morogoro ambapo akiwa hapo kulikuwa na malalamiko ya kuingiza chuoni Wanafunzi (Admissions) kwa Upendeleo nje ya Utaratibu wa Wazi wa Wizara ya Elimu na Wanafunzi wengine wakisikika wakisema waliombwa HELA ili kuingizwa Chuono.Hili suala linatia wasiwasi juu ya Uadilifu wa Bw.Mvula kwa Umma ikiwa atakuwa Muaminifu na mwadilifu katika Chuo cha Ualimu TUKUYU,MBEYA akiwa PRINCIPAL MPYA.
- Pia kwa mujibu wa Waraka wa MUUNDO wa Utumishi wa Wakufunzi katika Miundo ya Utumishi ya kazi zilizo chini ya Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Ufundi, toleo jipya la tarehe 10/8/2011 unaelekeza kuwa ili Mtu awe PRINCIPAL / Mkuu wa Chuo cha Diploma za Ualimu ni lazima awe Mkufunzi wa Chuo Daraja la I mwenye Shahada ya Uzamili (Masters) na Utendaji mzuri wa kazi kulingana na OPRAS lakini Bw. Mathias Mvula HANA SIFA HIZO zilizotajwa katika waraka ili kupewa Madaraka hayo.