JAYJAY
JF-Expert Member
- Oct 31, 2008
- 7,509
- 7,540
leo asubuhi nilikuwa naangalia habari ya channel10 kuhusu kusakwa kwa matapeli watatu wa viwanja, kamanda Kova alisema kwamba hawa jamaa wanauwezo wa kutengeneza hati bandia ambayo ina taarifa sahihi kama ile halisi iliyopo wizarani.mwanzoni hii habari nilipoiskia tbc hawakueleza kwa urefu jinsi watu wanavyoweza kutapeliwa na hawa jamaa kiasi kwamba nikawalaumu wanaotapeliwa kwa uzembe wa kushindwa hata kufika wizarani kuulizia uhalisi wa hati hizo.lakini sasa nimegungua kuwa hata mimi ningeweza kuwa mwathirika.hii inaonesha jinsi gani hii wizara ilivyooza, yaani lazima kutakuwa na mfanyakazi au wafanyakazi wanaoshirikiana na matapeli hao.kazi kwelikweli inabidi ifanyike kuisafisha hii wizara, ndio maana migogoro ya viwanja haiishi.hawa jamaa sasa wanasakwa na kifuta jasho cha shilingi milioni tano kimeahidiwa na kamanda Kova, hapo nadhani ni baada ya kigogo mmoja kupigwa hela nyingi ndio wanashtuka sasa maana siku zote hizi kilele zimekuwepo na hakuna aliyejali. tuombe wadakwe, labda mengi yatajulikana.