mwanamwana
JF-Expert Member
- Aug 1, 2011
- 1,076
- 4,113
Watanzania wametakiwa kuchukua tahadhari kufuatia mlipuko wa ugonjwa wa homa ya uti wa mgongo ulijitokeza katika nchi ya Jamhuri ya Kidemokrasia Congo (DRC).
Kwa mujibu wa Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt.Aifelo Sichwale amesema ugonjwa huo wa mlipuko husababishwa na bakteria wanaojulikana kama 'Neisseria Meningitides'.
Taarifa ya Dkt.Sichwale kwa vyombo vya habari ianeleza kuwa ni vyema tahadhari kuendelea kuchukua kwani magonjwa hayana mipaka, hususani mikoa inayopakana na DRC.
Aidha Vimelea vya ugonjwa huu huambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya hewa au kukaa na mtu mwenye maambukizi, kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa Septemba 8, 2021 na Shirika la Afya Duniani (WHO) kanda ya Afrika, mlipuko huo unaoambukiza ni tishio kwa sasa Barani Afrika.
Kwa mujibu wa Mganga Mkuu wa Serikali, Dkt.Aifelo Sichwale amesema ugonjwa huo wa mlipuko husababishwa na bakteria wanaojulikana kama 'Neisseria Meningitides'.
Taarifa ya Dkt.Sichwale kwa vyombo vya habari ianeleza kuwa ni vyema tahadhari kuendelea kuchukua kwani magonjwa hayana mipaka, hususani mikoa inayopakana na DRC.
Aidha Vimelea vya ugonjwa huu huambukizwa kutoka kwa mtu mmoja kwenda kwa mwingine kwa njia ya hewa au kukaa na mtu mwenye maambukizi, kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa Septemba 8, 2021 na Shirika la Afya Duniani (WHO) kanda ya Afrika, mlipuko huo unaoambukiza ni tishio kwa sasa Barani Afrika.