Wizara ya Afya: Watanzania endeleeni kuchukua tahadhari dhidi ya COVID-19

Yani mambo ni Magumu sana Unateua mawaziri badala ya kusimamia ukwelii wanakaa kukutukuzaa hata pale unapokoseaa...! Aibu sana yani.. Nasema bora uvuliwe madaraka lakini utakuwa umeokoa nafsi za watanzania zilizotakiwa kupotea kisa Siasa tala majii.

Haya leo Rais anakiri kuna Covid wizara ndo inaanza kuandika maujingaa yani upuuzi wa hali ya juu. Chama cha Madoctor nao akilii kizibooo yanii. Wasomi wakianza kuitukuza siasa jua nchi imepotezaa dira
 
Mzee alishatoa neno mwaka jana kwenye mkutano wa CWT.

 
Tatari WHO imeanza kutukalia kooni dunia yote inajua kuwa tz ndo inayozorotesha juhudi za mapambano dhidi ya C19/21
 
Mburura wakubwa nyie! Achaneni na kubwa la maadui, tumieni taaluma zenu kuokoa watu, jamii itawakumbuka kwa kuokoa roho zao. Kubwaa maadui ni mmoja ila anawaburuza, mnataka awakumbuke kwa lipi?
 
Wizara ya Afya yawashukuru Watanzania wote kwa kutekeleza agizo la Rais Dk. Magufuli la maombi ya siku tatu kuliombea taifa dhidi ya janga la corona, na imewasisitizia Watanzania kuendelea kuchukua tahadhari ya magonjwa mbalimbali yakiwemo ya mlipuko.
IMG_20210221_123732.jpg

IMG_20210221_123734.jpg
 
Jiwe mambo yanemshinda sasa anatafuta pa kutokea.

Gwajima ni waziri wa afya wa hovyo tangu kuundwa kwa nchi hii yupo tayari kuficha ukweli mradi abakie waziri,sijui kwa tamko hili kajificha wapi
 
Hivi hii ni barua kutoka wizara ya Afya au ni Barua ya Propaganda na mwendo ule ule wakupongezana na kusifiana ?

Hayo mambo ya uchumi wa kati na Magufuli yanaingiaje katika statement ya Afya ya wananchi? Story nyingi but in the end hakuna sehemu wamesema Corona ipo Tanzania, sababu tunaweza kujilinda na Ebola wakati Ebola haipo nchini?

Waache Siasa na kutoa miongozo straight bila ukakasi..., hapo wangeweza kutoa paragraph nyingi tu, bora hata wangewakumbusha watu jinsi ya kutungeneza hio kachumbari yao (ambayo kwa mujibu wao inatibu Corona)
 
Hii vita ya kuvaa/kutovaa barakoa Magu angeicha tu. “Kuwaponda” watu hadharani tena mbele ya altare sio sawa kabisa.

Kama yeye havai kwa kuwa ana shida ya kupumua vizuri, asiwadiscourage wanaovaa. Ukiwa Rais wa Nchi unapaswa kuchunga ulimi wako
 
Hilo tangazo limejaa unafiki mtupu.

Ujumbe muhimu ni kwamba tatizo la Corona ni kubwa. Tuchukue tahadhari. Serikali haieleweki. Imekuwa ni serikali ya kinafiki ambapo kila mtu anahangaika namna ya kumsifia Rais.
 
Tamko la Wizara husika ni pamoja na maombi! Hatujasikia chochote juu ya mpango kazi wa Wizara kuhusu tiba sahihi, upatikanaji wa dawa, vifaa tuba na PPE kwa watoa huduma kama Madaktari, Manesi, Wataalam wa Maabara ni Hatujasikia tamko la kitaalam kuhusu chanjo zinazotumika Duniani au hata zile dawa za Madagascar.

Wizara ya Afya inatoa tamko kwa Ku quote hotuba ya Rais!
 
Tanzania kuna korona? Tunaomba takwimu za maambukizi na vifo. Nyambafu!
Mkuu tupeane moyo tu,kwa kweli hali ni mbaya hasa mkoa wa Arusha corona iko.

Tuombe tu Baba alainike chanjo ije mapema.ila mdogomdogo naona anaanza kulegea soon atalamba ndala za mabeberu watuokoe.
 
Ndo maana nawakubali Wakenya kwenye kutetea haki zao, Ila sisi Watanzania ni bure kabisa tupo Kama bendera hata kama tunaumia ni kutetea ujinga tuu!!
Ni bendera fuata upepo. ni waoga kiasi kwamba uoga huo umepelekea tumekuwa waanfki.

leo hii kwa wingi wetu tunashindwa kuihoji serikal why haiko serious kwenye hili suala.. kida mtu mmoja tu.

Ndio maana taifa mengine yanatudharau. sometimes naona tunawachukia majirani zetu for nothing
 
Tamko “linawasihi na kuwasisitiza” watu wajichukilie hatua muhimu wao wenyewe.

Serikali inatamka wazi kwamba kila mtu abebe msalaba wake. Wao hawana mpango wa kuwabana wageni kuja wamepima wala kuongeza PPEs na Ventilators huko hospitalini..
Mna uhakika hili siyo tamko la viongozi wa dini? Nchi ipo sehemu mbaya sana. Serikali inachukuwa sehemu ya viongozi wa dini. Wamekaa mpaka wakasikia kwanza ''waliyemkabidhi ubongo wao'' anasema nini na wao wanakariri.
 
Back
Top Bottom