Wizara ya Afya tunaomba ufafanuzi wa hili upesi kwani moja haikai wala mbili

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Jul 13, 2013
56,052
107,537
Kwanza kabisa nitangulize Shukrani zangu za dhati kabisa kwa Uongozi wa JamiiForums na hasa Moderators wake kwa ' kuninyoosha ' kwa kunipiga BAN ya ' Kutukuka ' ya siku Gwala / Tano ambazo nisifiche kusema zimenitesa kwa kiasi kikubwa kwani nina mapenzi ya JamiiForums kuliko hata ' Mbunye ' zilizopo na zile zitakazokuja. Naahidi kubadilika ila taratibu taratibu hivyo nanyi mnivumilie lakini mjue nabadilika.

Baada ya utangulizi huo ' mujarab ' kabisa sasa nianze kwa kutiririka na kuserereka kwa kile nilichonacho ambacho kiukweli kimenishtua na kinaniogopesha hadi muda kwani kimenifanya nianze kuwaza kwamba huenda muda wowote nami Israeli akafanya yake kutokana na hicho Kitu chenyewe.

Inasemekana kwamba kumbe ukila nyama ya Nguruwe ( Kitimoto ) halafu muda huo huo isizidi kati ya dakika 60 hadi120 ukaenda kupima VVU / UKIMWI ( Dally Kimoko ) basi vipimo vyako vitaonyesha kuwa huna ' maambukizi ' hata kama kiukweli umeshaanza kulipiga / kulikung'uta vizuri Gitaa la Dally Kimoko ( umeathirika na HIV / AIDS )

Najua wengi mtashangaa na kujiuliza ni kwanini GENTAMYCINE analisemea hili ila ukweli ni kwamba nimekuwa na kawaida ya kila ninapompata Mwanamke / Demu na kabla sijaenda Kungonoka / Kubanduana / Kubaiolojiana nae basi huwa namuandaa ili twende kupima damu hivyo baada ya kupata hii taarifa nahisi kwamba kuna uwezekano pengine hawa ' Warembo ' ambao nilikuwa nawaandaa kwenda kupima hii mbinu ya kula Nyama ya Nguruwe ( Kitimoto ) dakika 60 hadi 120 walishakuwa nayo hivyo Mimi nikipima nao na kuona tumepona kimbe kiuhalisia tayari ' Nyuzi ' za Dally Kimoko nimeshaanza kuzipiga ( nimeathirika )

Na kibaya zaidi ni kwamba hii taarifa nimesikia kutoka kwa Madaktari fulani wa Hospitali moja iliyopo jirani na Fukwe na wengine wa Hospitali iliyopo katikati ya Bungoni na Boma nilipogongana nao mahala fulani hivi wote tukiwa tunaburudika na kusahau Shida zetu za ' ukazaji wa vyuma ' nchini wakati nao walipokuwa wanapiga stori zao mbili tatu. Sasa kama Madaktari wenyewe wameliongelea hili jambo unadhani hapa hakuna haja ya Mamlaka husika kulifanyia hili jambo utafiti wa haraka ili tujue moja?

Naamini kwamba hata humu humu JF kuna Madaktari tena wabobezi kabisa hivyo watanipa ushirikiano wao juu ya hili ili wanitoe hofu / wasiwasi Mimi GENTAMYCINE kwani kiukweli tokea niwasikie hawa Madaktari wakisema hili ( sasa sijui walikuwa wanatania tu au wanamaanisha ) nimekosa amani na raha kabisa kwani kwa utiririkaji na usererekaji wangu wa ' Mbunye ' baada ya kutoka Kupima yawezekana tayari nimeshaanza kulikung'uta vizuri mno Gitaa mahiri la Dally Kimoko ( nimeshaukwaa Umeme )

Msaada wa haraka jamani Madaktari na Wizara ya Afya.

Nawasilisha.
 
Pole Sana kwa ban naamini sasa utaacha kutukana matusi ovyo. Pia jifunze kuheshimu wengine humu jukwaani.
 
Kuna mambo mengine ni ujinga tu, we unajua ligonjwa lenyewe halina tiba wala kinga af unataka upime... unapima ili iweje.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom